Tuesday, July 23, 2013

FC BARCA YATARAJI KUMTANGAZA MARTINO KUWA KOCHA MPYA

Gerardo Martino ambaye ni raia wa Argentina,Kocha wa Newell’s Old Boys ya huko Argentina, anatarajiwa kutangazwa kuwa Kocha mpya wa FC Barcelona kuchukua nafasi iliyoachwa wazi Tito Vilanova kutokana na sababu za  kiafya.
Martino, mwenye Miaka 50, anategemewa kusaini Mkataba wa Miaka mitatu na kutangazwa rasmi baadae Wiki hii.
WASIFU WAKE:
JINA: Gerardo Daniel Martino
KUZALIWA: Novemba 20, 1962 (Miaka 50), Rosario, Argentina
TIMU ya VIJANA: Newell's Old Boys
KLABU:
1980–1990  Newell's Old Boys Mechi 392  Magoli: 35
1991 Tenerife Mechi 15 Goli: 1
1991–1994  Newell's Old Boys Mechi: 81 Goli: 2
1994–1995   Lanús Mechi 30 Goli 3
1995 Newell's Old Boys Mechi 15
1996 Barcelona SC Mechi 5
ARGENTINA: Mechi 1
UMENEJA:
1998 Brown de Arrecifes
1999 Platense
2000 Instituto
2002–2003   Libertad
2003–2004   Cerro Porteño
2005 Colón
2005–2006   Libertad
2006–2011   Paraguay
2012–2013   Newell's Old Boys
2013-           Barcelona FC
Gerardo Martino akiwa Fc Barcelona atakuwa pamoja na Wasaidizi wake mwenyewe ambao ni Elvio Paolorrosso, Kocha wa Viungo, na Msaidizi Jorge Pautasso.
Awali ilitegemewa Kiungo wa zamani wa Barca, Luis Enrique, ndie atatwaa madaraka Nou Camp lakini tatizo kubwa ni kuwa Enrique alijiunga na Klabu ya La Liga Celta Vigo Mwezi uliopita tu na ukaja utata wa Mkataba.
Martino, au ‘Tata’ kama alivyo maarufu, anakuwa Muargentina wa nne kuwa Kocha wa Barcelona wengine ni Helenio Herrera, Roque Olsen na Cesar Luis Menotti na anatua Nuo Camp kuungana na Supastaa wa Argentina Lionel Messi ambae amemsifia sana Kocha huyu.
Jumatano, Barcelona inacheza Mechi ya Kirafiki na Mabingwa wa Ulaya, Bayern Munich na itakuwa chini Jordi Roura kwenye Mechi hiyo iatakayochezwa huko Allianz Arena, Munich.

CHELSEA YAJIPANGA KUTUMA DAU LA PILI KUHUSU ROONEY

CHINI ya kocha mpya Jose mourinho club ya Chelsea ipo tayari kutuma ofa ya pili ya kumsajili Wayne Rooney. 
Kocha wa Stamford Bridge, Jose Mourinho bado anakaza masuli kumpata mshambuliaji wa Manchester United na ananiandaa kulipa Pauni 30 kukamilisha dili hilo. 
Chelsea iliwasilisha ofa ya awali wiki iliyopita, lakini ikakataliwa na klabu ya Old Trafford.

Jamaa huyu hatabiriki yupo mbioni kutimka
United ilikataa pofa ya Pauni Milioni 23 taslimu jumlisha Milioni 2.5 malipo ya ziada ikisistiza Rooney, mwenye umri wa miaka 27, hauzwi.
Chelsea inafurahi kumpa mshahara wa Pauni 240,000 Rooney kwa wiki anazolipwa United na watampa Mkataba wa miaka mitano kama atafanikiwa kulazimisha kuondoka kwa mabingwa hao wa England.
Rooney ambaye mambo yake hayajaeleweka anafanya mazoezi viwanja vya mazoezi vya United, Carrington baada ya kurejea kutoka kwenye kambi ya klabu kujiandaa na msimu kwa sababu ya kuumia nyama.
Lengo kuu: Jose Mourinho anataka kumnasa Wayne Rooney ili kuimarisha safu ya ushambuliai ya Chelsea
Kazi kweli: Mustakabali mzito wa Rooney unampa wakati homa David Moyes katika siku zake za mwanzo kazini United
 
Kocha wa United, David Moyes ameendelea kusistiza Rooney, ambaye amebakiza miaka miwili katika mkataba wake Old Trafford, hauzwi.
Lakini anaweza kupambana sana kumbakiza mchezaji huyo, kwqa sababu Mourinho anamtaka kweli Rooney na anapambana kumpata.