Tuesday, July 23, 2013

CHELSEA YAJIPANGA KUTUMA DAU LA PILI KUHUSU ROONEY

CHINI ya kocha mpya Jose mourinho club ya Chelsea ipo tayari kutuma ofa ya pili ya kumsajili Wayne Rooney. 
Kocha wa Stamford Bridge, Jose Mourinho bado anakaza masuli kumpata mshambuliaji wa Manchester United na ananiandaa kulipa Pauni 30 kukamilisha dili hilo. 
Chelsea iliwasilisha ofa ya awali wiki iliyopita, lakini ikakataliwa na klabu ya Old Trafford.

Jamaa huyu hatabiriki yupo mbioni kutimka
United ilikataa pofa ya Pauni Milioni 23 taslimu jumlisha Milioni 2.5 malipo ya ziada ikisistiza Rooney, mwenye umri wa miaka 27, hauzwi.
Chelsea inafurahi kumpa mshahara wa Pauni 240,000 Rooney kwa wiki anazolipwa United na watampa Mkataba wa miaka mitano kama atafanikiwa kulazimisha kuondoka kwa mabingwa hao wa England.
Rooney ambaye mambo yake hayajaeleweka anafanya mazoezi viwanja vya mazoezi vya United, Carrington baada ya kurejea kutoka kwenye kambi ya klabu kujiandaa na msimu kwa sababu ya kuumia nyama.
Lengo kuu: Jose Mourinho anataka kumnasa Wayne Rooney ili kuimarisha safu ya ushambuliai ya Chelsea
Kazi kweli: Mustakabali mzito wa Rooney unampa wakati homa David Moyes katika siku zake za mwanzo kazini United
 
Kocha wa United, David Moyes ameendelea kusistiza Rooney, ambaye amebakiza miaka miwili katika mkataba wake Old Trafford, hauzwi.
Lakini anaweza kupambana sana kumbakiza mchezaji huyo, kwqa sababu Mourinho anamtaka kweli Rooney na anapambana kumpata.