Thursday, August 28, 2014

USAJIL LIGI KUU VODACOM TZ BARA BADO WADUNDADUNDA WAPINGWA KALENDA TENA.

Baada ya tarehe 17 baada ya hapo ukaja tarehe 27 na sasa usajili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa wachezaji wa ndani umesogezwa mbele kwa masaa 48 kuanzia jana, kutokana na timu kushindwa kukamilisha usajili katika muda husika jana. Hayo ni kwa mujibu wa Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Selestine Mwesigwa ambapo amesema sababu za kusogeza mbele ni klabu zote za Ligi Kuu kushindwa kukamilisha usajili jana.
Mwesingwa amesema kilichopelekea vilabu vimeshindwa kuutumia huu mfumo wetu mpya wa elektroniki, sasa tumewapa Saa 48 zaidi warekebishe, zikiisha hizo, hapo hakuna nafasi tena, tunasonga mbele. Amesema kwamba hadi muda wa kufunga usajili jana Saa 6:00 usiku, ni timu moja ya Kimondo FC ya Daraja la Kwanza ndiyo iliyokuwa imefanikiwa kukamilisha usajili wake katika mfumo huo.
Mwesingwa amesema tff inapenda kuchukua fursa hii kuwapongeza Kimondo kwa kumudu kuutumia mfumo huu na kuwasilisha usajili wao ndani ya muda. Hata hiyo Mwesigwa amesema kwamba dirisha la usajili kwa wachezaji wa kigeni litafungwa Septemba 6, mwaka huu. “Hili dirisha la wachezaji wa kigeni likifungwa, hakuna nyongeza ya muda tena, kwa kuwa hili lipo katika mfumo wa kimataifa chini ya FIFA, likifungwa, limefungwa dunia nzima, hivyo nawasihi viongozi wa klabu wahakikishe hawafanyi makoasa.