Monday, September 8, 2014

KOCHA PATRIC PHIRI ASEMA KIKOSI KIPO KAMALI KWA VPL

Kocha mkuu wa timu ya soka ya Simba  Patrick Phiri amesema amelizishwa na kiwango cha timu hiyo mara baada ya kuitandika timu ya Gor mahia kutoka Kenya  kwa mabao 3 kwa 0 katika mchezo uliopigwa katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam siku ya jumamosi.
Akizungumza na mkali wa dimba tz.blogspot.com Patrick Phiri  amesema kuwa wachezaji wake wanajituma katika michezo yao na kucheza vizuri katika mechi zote anazoziongoza.

Phiri amesema wanacheza vizuri uwanjani,uwezo umeongezeka,wamecheza na timu bora kutoka kenya,kwa hiyo naweza kusema hiki ni kipimo sahihi kwa timu yangu"alisema Patrick Phiri 

Patrick Phiri amesema maandalizi waliyoyafanya visiwani Zanzibar kumewafanya wachezaji wake wawe vizuri na anafuraha kuona kikosi chake kimeimalika.