Kocha mkuu wa timu ya soka ya Simba Patrick Phiri amesema amelizishwa na kiwango cha timu hiyo mara baada
ya kuitandika timu ya Gor mahia kutoka Kenya kwa mabao 3
kwa 0 katika mchezo uliopigwa katika dimba la uwanja wa Taifa jijini
Dar es salaam siku ya jumamosi.
Akizungumza na mkali wa dimba tz.blogspot.com Patrick Phiri amesema kuwa wachezaji wake wanajituma katika michezo yao na kucheza vizuri katika mechi zote anazoziongoza.
Phiri amesema wanacheza
vizuri uwanjani,uwezo umeongezeka,wamecheza na timu bora kutoka
kenya,kwa hiyo naweza kusema hiki ni kipimo sahihi kwa timu
yangu"alisema Patrick Phiri
Patrick Phiri amesema maandalizi waliyoyafanya visiwani Zanzibar kumewafanya wachezaji wake wawe vizuri na anafuraha kuona kikosi chake kimeimalika.