Tuesday, February 18, 2014

VIDIC WA MAN UNITED AKUBALI KWENDA YAKE ITALY

BEKI Kisiki Nemanja Vidic wa Man united amekubali kujiunga na Inter Milan ya Italia. Nyota huyo wa kimataifa wa Serbia ambaye alitangaza Januari kuamua kuondoka Old Trafford mwishoni mwa msimu huu anatazamiwa kuasaini dili la  mkataba wa miaka miwili ambao utamuwezesha kulipwa kitita cha euri milioni tatu kwa mwaka. Kuna taarifa kuwa Vidic aliwafahamisha viongozi wake wa United kuhusu uamuzi wake wa kukubali kwenda nchini Italia baada ya kufikia makubaliano kwenye mchezo waliotoka sare ya bila ya kufungana na Arsenal katika uwanja wa Emirates Jumatano iliyopita. Ofisa mkuu wa Inter, Piero Ausilio amekuwa na mawasiliano ya karibu na nyota huyo toka Januari alipotangaza kutaka kuondoka. Toka atangaze kuondoka Vidic amekuwa akiwendwa na vilabu mbalimbali huku Monaco ya Ufaransa na Galatasaray ya Uturuki zikiwa mojawapo lakini nyota huyo ameamua kwenda Italia. Vidic alijiunga na United akitokea klabu ya Spartak Moscow ya Urusi mwaka 2006 na amefanikiwa kushinda mataji matano ya Ligi Kuu na moja la Ligi ya Mabingwa barani ULaya katika kipindi cha miaka nane aliyokaa Old Trafford.