Monday, June 10, 2013

MMOJA APOTEZA MAISHA KATIKAMICHUANO YA LANGALANGA YA CANADIAN.

MASHINDANO ya langalanga ya Canadian Grand Prix jana yalimalizika kwa Majonzi makubwa baada ya mmoja wa wafanyakazi mwenye umri wa miaka 38 kufariki baada ya kukanyagwa na winji. Ajali hiyo ilitokea wakati gari la dereva Esteban Gutierrez wa timu ya Sauber lilipokuwa likiondolewa barabara za Montreal baada ya kupata ajali.

Mashuhuda wanasema wakati winji hilo likijaribu kuliondoa gari hilo ndipo mfanyakazi huyo aliangusha radio yake na wakati akiiokota ndipo alipokanyagwa kwasababu dereva wa winji hakumuona. Katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter Gutierrez alituma salamu zake za rambirambi kwa familia ya mfanyakazi huyo kwa kumpoteza mtu wao karibu. Mbali na Gutierrez madereva wengine waliotoa rambirambi zao ni pamoja na Sebastian Vettel wa Red Bull aliyeshinda mbio hizo pamoja na Fernando Alonso wa Ferrari aliyeshika nafasi ya pili. Hilo ni tukio la pili kutokea katika mashindano hayo kwani mwaka jana katika michuano ya Grand Prix ya Italia mfanyakazi wa kujitolea wa zimamoto Paolo Ghislimberti alifariki kutoka na amejraha aliyopata kichwani na kifuani baada ya kupigwa na tairi lililochomoka kutoka katika gari la Heinz-Harald Frentzen wa timu ya Jordan.