Monday, June 10, 2013

TAIFA STAR YATUA NCHINI IKITOKEA NCHINI MORROCO.

TIMU ya taifa ya  Tanzania, Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imewasili  nchini leo asubuhi.
Taifa stars ilikuwa Morocco kucheza na wenyeji wao ambapo katika mchezo huo taifa star imefungwa bao 2-1 katika mechi ya Kundi C kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil.

Stars ambayo bado inashika nafasi ya pili katika kundi hilo ikiwa na pointi sita imewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Aidha katika kundi c kinara wa kundi hilo ni Ivory Coast yenye point kumi ambayo itacheza mchezo wa marudiano na Taifa Star wikiendi ijayo katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

Hata hivyo kwa upande wa kundi hilo nafasi ya tatu inashikiliwa na Morocco yenye point tano huku nafasi ya mwisho ikishiliwa na Gambia yenye point moja.
KUNDI C


Pos
Team
P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts
1
Ivory Coast
4
3
1
0
10
2
8
10
2
Tanzania
4
2
0
2
6
6
0
6
3
Morocco
4
1
2
1
6
7
-1
5
4
Gambia
4
0
1
3
2
9
-7
1