Thursday, June 13, 2013

TAFAKARI YA LEO BARCA ILIVYOFANYA JEURI KUMTAFUTIA MESSI COMBINATION JE KWA NEYMA ITAKUWAJEEEE??

Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Barcelona imetumia jumla ya Euro 205 milioni kwa ajili ya kusaka mshambuliaji ambaye anaweza kumpunguzia Messi mzigo wa ustaa alioubeba kwa muda mrefu klabuni hapo.
Hivyo kuwasili kwa mshambuliaji wa Santos na timu ya taifa ya Hispania, Neymar, katika kikosi cha Barcelona, inamaanisha kuwa Barcelona imeendelea kutumia fedha nyingi kusaka mshambuliaji ambaye anaweza kung’ara vyema kwa pamoja na staa wao, Lionel Messi.

Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Barcelona imetumia jumla ya Euro 205 milioni kwa ajili ya kusaka mshambuliaji ambaye anaweza kumpunguzia Messi mzigo wa ustaa alioubeba kwa muda mrefu klabuni hapo.
Thierry Henry
Katika msimu wake wa kwanza tu ndipo Henry alifikia matarajio ya mashabiki wa Barcelona. Baadaye kuibuka kwa kinda wa Kihispaniola, Pedro Rodriguez, kulimfanya Henry apate nafasi finyu ya kucheza katika kikosi cha kwanza na mwisho aliamua kutimkia Marekani katika klabu ya New York Bulls.
Hata hivyo Henry hakufikia kiwango alichokuwanacho wakati anachezea Arsenal chini ya Arsene Wenger ingawa katika kipindi chake na Barcelona alishinda mataji kadhaa.
Zlatan Ibrahimovich
Ukitazama hapa katika hali ya kawaida kilikuwa kipindi kibaya katika harakati za maisha ya soka ya Ibrahimovich. Tofauti na matarajio ya wengi, licha ya kusajiliwa kwa Euro 46 milioni huku pia Barcelona wakimtoa  Samuel Eto’o kwenda Inter Milan, bado Ibrahimovich hakutamba sana Nou Camp.
Mwishowe alijikuta akiingia katika mgogoro mkubwa na kocha wa wakati huo, Pep Guardiola. Ibrahimovich alimshutumu Guardiola kwamba alikuwa anampendelea zaidi Messi huku wakati mwingine akimchezesha nafasi ya kati wakati yeye yuko benchi.
Baada ya msimu mmoja tu, Zlatan aliondoka akarudi Italia ambako alijiunga na AC Milan.
David Villa
Alionekana mmoja kati ya wachezaji ambao wangeweza kumpunguzia mzigo wa mabao staa huyu wa Argentina. Alianza vema, lakini baadaye aliumia katika michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia, ilikuwa Desemba 2011.
Mbali na hilo tangu hapo kasi yake imepungua uwanjani na sasa inasemekana ataondoka zake Barcelona katika kipindi hiki cha uhamisho wa wachezaji.