Thursday, June 13, 2013

LIONEL MESSI NA MZAZI WAKE WA KIUME WAINGIA MATATANI.

Mshambuliaji nyota  wa Barcelona  na timu ya Taifa ya Argentina Lionel Messi na babake wanatuhumun kwa tuhuma za kukwepa kulipa kodi nchini Hispania huivyo serikali ya nchi hiyo ipo katika zaidi ambapo inasadikika kuwa na deni la paundi milioni tatu nukta nne.

Mchezaji huyo kutoka Argentina na babake, Jorge wanatuhumiwa kuibia serikali ya nchi hiyo, kwa kujaza fomu zisizokuwa za ukweli za marejesho ya kodi kati ya mwaka wa 2007 na 2009.Hata hivyo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 hajasema lolote kuhusiana na madai hayo.
Messi hulipwa Euro milioni kumi na sita kila mwaka na ndiye mchezaji anayelipwa kiasi cha juu zaidi duniani.Lakini mwendesha mashtaka Raquel Amado, aliwasilisha nyaraka za mahakama nyumbani kwa mchezaji huyo katika mtaa wa kifahari wa Gava mjini Barcelona.
Jaji mjini humo ni sharti waidhinisha malalamishi dhidi ya mshukiwa yeyote kabla hajafunguliwa mashtaka.Messi na babake wanashukiwa kutumia kampuni katika mataifa ya ng’ambo, mjini Belize na Uruguay kuuza haki za kutumia picha ya mchezaji huyo.
Mchezaji huyo na babake wanatuhumiwa kutumia kampuni hizo zilizoko nje ya Hispania, ambako anaishi na kucheza soka ya kulipwa, kukwepa kulipa kodi inayokisiwa kuwa paundi milioni tatu na nusu.