Sunday, May 19, 2013

WALIMU MASHULENI WATAKIWA KUHIMIZA NIDHAMU KWA WANAFUNZI

WALIMU wa michezo katika shule za msingi, sekondari na vyuo wametakiwa kuhamasisha suala la nidhamu kwa wanafunzi ili kuwajengea msingi ilio bora utakaowafanya wafike mbali.
Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Tabora, Joyce Ndonda, aliyekuwa mgeni rasmi katika bonanza maalumu la mchezo wa netiboli, lililofanyika kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini  humo.
Akizungumza na wanamichezo mbalimbali walioshiriki katika bonanza hilo, Ndonda ameipongeza Chaneta Tabora kwa kuanzisha bonanza hilo na kuwataka kuendelea na utaratibu huo, kwani ni chachu ya kukuza vipaji kwa vijana na kuinua hamasa ya michezo.
Aidha kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli Mkoa wa Tabora, Kulwa Kavula, amesema lengo la bonanza hilo ni kuhamasisha wasichana na wadau wengine kuupenda mchezo huo.
Hata hivyo amewaomba wadau katika halmashauri zote za Mkoa wa Tabora kuwapa ushirikiano ili waweze kufanikisha harakati za kuinua michezo huo nchini.