
Klabu
hizi 3 zitasafiri n kuelekea Marekani kuumana zenyewe kwa wenyewe katika
Mechimbili za kirafiki huku Tottenham wakitua Visiwa vya Bahamas kucheza na
Jamaica.
ZIARA:
Mei 23: Man
City v Chelsea [St Louis]
Mei 25: Chelsea
v Man City [New York]
Mei 23: Tottenham
v Jamaica [Thomas A. Robinson National Stadium, Nassau Paradise Island,
Bahamas]
England
nayo inatarajiwa kucheza na Republic of Ireland, Uwanjani Wembley hapo Mei 29
na kisha kuruka kwenda Brazil kucheza Uwanja wa Maracana Jijini Rio De Janeiro na
Brazil hapo Juni 2.
Kikosi
cha Hodgson alichokiteua kuiwakilisha England katika Mechi hizo mbili kina
Wachezaji wanane toka Timu hizo tatu.
Chelsea
inasemekana imekubali kuwaruhusu Frank Lampard, Ashley Cole na Gary Cahill
kuondoka baada ya Mechi yao ya kwanza ya Tarehe 23 na Man City ili kurudi
London kujiunga na England.
Lakini
Hodgson amesema wao walipanga Mechi zao za Kimataifa kwa makusudi ili kuwapa
Wachezaji wote mapumziko ya Wiki moja baada ya Msimu wa Klabu zao kumalizika
kisha kuwachukua wao kwa Wiki moja na baada ya hapo kuwaachia kwenda Vakesheni
zao kabla kurudi Klabuni kwao kwa matayarisho ya Msimu mpya wa 2013/14.
Hogson
amesema Ziara hizo za Klabu zitawafanya wasafiri safari ndefu kuvuka Bahari ya
Atlantic na kurudi tena na hilo halitasaidia matayarisho yao.
Akimalizia
Hodgson alisema: “Hii ndio hali ambayo tumejikuta tunayo na hatuwezi
kulazimisha Klabu nini wafanye.”
KIKOSI
KAMILI:
MAKIPA: Ben
Foster, Joe Hart, Alex McCarthy.
MABEKI: Leighton
Baines, Gary Cahill, Ashley Cole, Phil Jagielka, Glen Johnson, Phil Jones,
Joleon Lescott, Kyle Walker.
VIUNGO: Michael
Carrick, Tom Cleverley, Frank Lampard, James Milner, Alex Oxlade-Chamberlain,
Theo Walcott.
MAFOWADI: Andy
Carroll, Jermain Defoe, Wayne Rooney, Daniel Sturridge, Danny Welbeck.