Sunday, February 16, 2014

TAMBWE JEZI NAMBA 17 NA MABAO 17 MSIMBAZI SIMBA SC


Amisi Tambwe, raia wa Burundi ni moja kati ya washambiliaji mahiri mwenye kujitambua akiwa uwanjani ambapo amedhihirisha kuwa yeye ni mkali wa mabao
kutokana katika mechi 23 alizoichezea Simba SC hadi sasa za mashindano yote na kirafiki, amefunga mabao 17.
Kwa sasa, Tambwe ndiye mchezaji anayeongoza kwa mabao katika Ligi Kuu, akiwa amefunga mabao 15 na anafuatiwa kwa mbali na mshambuliaji wa AzamFC, Kipre Herman Tchetche raia wa Ivory Coast, mwenye mabao 10.
Tambwe amekuwa kipenzi cha wana Msimbazi kutokana na kuweza pia kutikisa nyavu za mahasimu, Yanga SC katika mechi mbili mfululizo baina ya timu hizo.
Tambwe alikuja Simba SC kwa pamoja na Mrundi mwenzake, beki Gilbert Kazewakitokea wote Vital’O msimu huu, baada ya kung’ara katika Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame nchini Sudan wakiiwezesha klabu yao kutwaa taji la michuano hiyo kwa mara ya kwanza katika historia yake.

Hata hivyo, Kaze amepoteza namba katika kikosi cha kwanza tangu ujio wa kocha Mcroatia, Zdravko Logarusic, ambaye amekuwa akimpanga beki Mkenya, Donald Mosoti aliyetokea naye Gor Mahia ya Kenya.