Sunday, February 16, 2014

AZAM FC NJE YALALA 2-0 MBELE YA WAMAKONDE WA MSUMBIJI:

Wawakilishi wa Tanzania,katika michuano ya Kombe la Shirikisho.  Barani afrika Azam FC wabwagwa katika michuano hiyo.
Azam FC imefungwa mabao 2-0 na wenyeji wake Ferreviario ya Msumbuji maarufu kama Wamakonde katika mechi iliyopigwa hii leo mjini Beira.
Katika mechi ya kwanza Azam FC ilishinda bao 1-0 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamzi jijini Dar. Mfungaji akiwa Kipre Tchetche.

Kutokana na kipigo cha leo, maana yake Azam FC imetolewa kwa jumla ya mabao 2-1 na kuifanya kutoka mapema zaidi katika michuano hiyo ndani ya misimu mitatu.