Friday, December 5, 2014

MTIBWA SUGAR YASEMA MAZUNGUMZO NA HASANI KESSI YANAKWENDA VIZURI.

Uongozi wa Klabu ya Mtibwa Sugar umeweka wazi kwamba upo katika hatua za mwisho za kumalizana na Simba kwa ajili wa beki  wao namba mbili Hassani Ramadhani Kessy licha ya kuripotiwa kuwepo  na ugumu wa mchakato huo wa usajili.
Hata hivyo kumekuwa na taarifa kwamba mazungumzo yako katika hatua nzuri sana na pande zote mbili, yaani Simba na Mtibwa Sugar zimekubali kwamba zimefanya mazungumzo.
Afisa Habari wa Mtibwa Sugar Tobias Kifaru ameweka wazi kuwa Simba wameonyesha nia ya kumtaka mchezajihuyo ambapo mazungumzo yanaendelea vizuri na kila kitu kinakwenda vizuri katika uwezekano wa kumsajili kukamilika ndani ya siku chache zijazo.