Friday, December 5, 2014

TFF YASEMA WACHEZAJI WATAKAO CHEZA NANI MTANI JEMBE LAZIMA WAWE WAMESAJILI RASMI

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limetangaza wachezaji watakaotumika katika mechi ya Bonanza ya Nani Mtani Jembe kati ya Simba dhidi ya Yanga lazima wawe wale waliosajiliwa kwa mujibu wa kanuni.
Yanga au Simba hazitaruhusiwa kumtumia mchezaji yoyote ambaye hayuko kwenye usajili wakati wa mechi hiyo ya Oktoba 13 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.
Maana yake, Simba haitaweza kumtumia kiungo wake Mgambia, Omar Mboob hadi hapo itakapomsajili.
Kama itamsajili, itawakosa mmoja kati ya Amissi Tambwe au Pierre Kwizera ambao italazimika kuwatema.
Hadi sasa inaonekana Simba bado inamjaribu, hivyo haitakuwa rahisi kupata uhakika wa kumsajili hadi Desemba.
Hata hivyo, Mboob atapata nafasi nyingine ya kuonyesha uwezo wake, kesho kwenye Uwanja wa Taifa wakati Simba itakapoivaa Express ya Uganda.