Thursday, January 29, 2015

WAANGALIZI WA SIRI KUSIMAMIA MECHI ZA MWISHO FDL

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litatuma waangalizi wa siri kwenye mechi za raundi ya 21 na 22 ambazo ni za mwisho kwa makundi yote ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) zitakazoanza kuchezwa  Februari 10 mwaka huu.
Mwangalizi huyo (match assessor) atatumwa na Katibu Mkuu ambapo baada ya mechi atatuma ripoti kwake kwa hatua zaidi.
TFF-LOGO-NEW
Mechi za raundi ya 21 kundi A zitachezwa Februari 10 mwaka huu kati ya KMC na African Lyon (Uwanja wa Mkwakwani), Kurugenzi FC na African Sports (Uwanja wa Mufindi), Majimaji na JKT Mlale (Uwanja wa Majimaji), Kimondo FC na Friends Rangers (CCM Vwawa, Mbozi), Ashanti United na Villa Squad (Uwanja wa Karume) na Polisi Dar na Lipuli FC (Uwanja wa Azam Complex).
Raundi ya 22 itachezwa Februari 16 mwaka huu kwa kuzikutanisha African Lyon na Polisi Dar (Uwanja wa Karume), Kurugenzi na Lipuli FC (Uwanja wa Mufindi), Kimondo FC na Majimaji (CCM Vwawa, Mbozi), JKT Mlale na Ashanti United (Uwanja wa Majimaji), Friends Rangers na African Sports (Uwanja wa Taifa), na Villa Squad na KMC (Uwanja wa Azam Complex).
Kundi B raundi ya 21 ni Februari 17 mwaka huu kati ya Burkina Faso na JKT Kanembwa (Uwanja wa Jamhuri), Mwadui na Polisi Tabora (Uwanja wa Mwadui), Polisi Dodoma na Green Warriors (Uwanja wa Jamhuri), Rhino Rangers na JKT Oljoro (Ali Hassan Mwinyi), Panone na Polisi Mara (Uwanja wa Ushirika), Geita Gold na Toto Africans FC (Geita).
Februari 22 mwaka huu ni JKT Kanembwa na Green Warriors (Lake Tanganyika), Mwadui na Burkina Faso (Mwadui), Polisi Tabora na JKT Oljoro (Ali Hassan Mwinyi), Polisi Dodoma na Panone (Uwanja wa Jamhuri), Toto Africans na Rhino Rangers (CCM Kirumba) na Geita Gold na Polisi Mara (Geita).
Mechi za viporo za Polisi Mara zitachezwa Februri Mosi dhidi ya JKT Kanembwa, na Februari 5 mwaka huu dhidi ya Polisi Tabora. Mechi zote zitachezwa kwenye Uwanja wa Karume mjini Musoma.
FIFA YACHUNGUZA TUHUMA ZA UPANGAJI MATOKEO
Ujumbe wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) upo nchini kuchunguza tuhuma za upangaji matokeo.
Waamuzi waliosimamishwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu  Tanzania (TFF) pamoja na watu wengine watahojiwa na ujumbe huo. Matokeo ya uchunguzi huo yatatangazwa na FIFA baada ya shughuli hiyo kukamilika.
Tunaendelea kuwahimiza wanafamilia wa mpira wa miguu wazidi kuzingatia kanuni za maadili za TFF, Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) na FIFA katika utendaji wao. FIFA itahakikisha kuwa haki inatendeka katika uchunguzi ambao inaufanya.
TFF YAHADHARISHA MGOGORO WA ZFA KORTINI
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)l imepokea kwa masikitiko taarifa za kuwepo tena kortini kwa kesi dhidi ya uongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA), jambo ambalo linaweza kuathiri ushiriki wa timu za Zanzibar kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, na Kombe la Shirikisho.
Mwishoni mwa mwaka jana, TFF ilihadharisha juu ya masuala ya mpira wa miguu kupelekwa mahakamani, kwani kwa mujibu wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kitendo hicho ni kinyume cha taratibu za uendeshaji mpira wa miguu ambazo zinakataza masuala ya mchezo huo kupelekwa katika mahakama za kawaida.
Kutokana na hali hiyo, TFF iliiandikia barua ZFA kutaka mgogoro huo uondolewe kortini na yenyewe kuridhia kuwa tayari kupeleka ujumbe Zanzibar ili ukutane na pande zinazohusika.
Pia TFF ilisema timu za Tanzania Bara zisingeruhusiwa kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi 2015 iwapo kesi hiyo ingeendelea kuwepo kortini na kutaka iondolewe bila masharti yoyote.
ZFA iliithibitishia TFF kuwa kesi hiyo imeondolewa kortini bila masharti, hivyo timu za Tanzania Bara kuruhusiwa kushiriki katika michuano ya Kombe la Mapinduzi. Ni muhimu suala hilo likashughulikiwa haraka ili kutohatarisha ushiriki wa timu za KMKM na Polisi kwenye michuano hiyo ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Monday, January 26, 2015

FDL KUSIMAMA KUPISHA VIPORO VYA POLISI MARA

Mechi za raundi ya 20, 21 na 22 za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kwa makundi yote zimesimamishwa ili kupisha Polisi Mara imalize mechi zake za viporo, na timu zote zicheze mechi zao za raundi zilizobaki kwa pamoja.
Polisi Mara ilifungiwa kutumia Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma kutokana na vurugu zilizojitokeza kwenye mechi zake, hivyo kusababisha kuwepo kwa mechi hizo za viporo dhidi ya JKT Kanembwa na Polisi Tabora.
Tayari Polisi Mara tumeiruhusu itumie tena Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume kwa mechi zake za nyumbani baada ya kuipa onyo kali kutokana na vurugu hizo. Lakini pia mechi zake kwenye uwanja huo zitachezwa chini ya uangalizi.
Uamuzi wa kupisha Polisi Mara imalize mechi zake za viporo una lengo la kuhakikisha mechi zote za raundi tatu za mwisho zinachezwa pamoja ili kuepuka uwezekano wa kupanga matokeo.
Pia klabu za FDL zenyewe ziliwasilisha ombi la kutaka mechi hizo za mwisho zichezwe kwa wakati mmoja.
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) wakati wowote kuanzia kesho (Januari 27 mwaka huu) itatoa ratiba ya mechi za viporo za Polisi Mara, pamoja na tarehe mpya za mechi za raundi ya 20, 21 na 22.

Sunday, January 25, 2015

MATOKEO NA MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA,VPL AZAM JUU

VPL-TFF-KLABU-LOGOMATOKEO:
Jumapili Januari 25
Azam FC 1 Simba 1
Stand United 0 Coastal Union 1
Mbeya City 2 Tanzania Prisons 2
Ruvu Shooting 2 Mtibwa Sugar 1
JKT Ruvu 1 Mgambo JKT 1
Kagera Sugar 1 Ndanda FC 2 [CCM Kirumba, Mwanza]


 MSIMAMO:

NA
TIMU
P
W
D
L
F
 A
 
GD
PTS
1
Azam FC
11
6
3
2
15
8
 
7
21
2
Yanga
10
5
3
2
12
7
 
5
18
3
JKT Ruvu
12
5
3
4
12
11
 
1
18
4
Mtibwa Sugar
10
4
5
1
13
7
 
6
17
5
Coastal Union
11
4
4
3
10
8
 
2
16
6
Polisi Moro
12
3
6
3
9
9
 
0
15
7
Ruvu Shooting
12
4
3
5
7
9
 
-2
15
8
Kagera Sugar
12
3
5
4
9
10
 
-1
14
9
Mgambo JKT
11
4
2
5
6
10
 
-4
14
10
Simba
10
2
7
1
10
8
 
2
13
11
Ndanda FC
12
4
1
7
12
17
 
-5
13
12
Mbeya City
10
3
3
4
6
8
 
-2
12
13
Stand United
12
2
5
5
7
14
 
-7
11
14
Tanzania Prisons
11
1
6
4
8
10
 
-2
9

Friday, January 23, 2015

LIGI KUU TANZANIA BARA KUWAKA MOTO DIMBANI KESHO NA JUMAPILI MBEYA CITY VS TZ PRISON

Timu za mikoa sita tayari imepata tiketi za kucheza robo fainali ya michuano ya Kombe la Taifa la Wanawake itakayoanza Januari 26 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati nyingine mbili zinajulikana leo (Januar
i 23 mwaka huu).
Mikoa ambayo timu zake tayari zina tiketi za robo fainali ya michuano hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya Proin ni Ilala, Kigoma, Mwanza, Pwani, Tanga na Temeke.
Matokeo ya mechi za leo kati ya Iringa na Ruvuma, na ile kati ya Mbeya na Katavi ndiyo yatakayoamua ni timu zipi mbili kati ya hizo zinakwenda Dar es Salaam kucheza robo fainali.
Timu zote zilizofuzu hatua ya robo fainali zinatakiwa kuripoti Dar es Salaam keshokutwa (Januari 25 mwaka huu). Fainali ya michuano hiyo itachezwa Februari Mosi mwaka huu.
TIMU YA BEACH SOCCER ZANZBAR YAWASILI DAR
Timu ya beach soccer ya Zanzibar imewasili Dar es Salaam leo mchana, tayari kwa kambi ya pamoja na Tanzania Bara kwa ajili ya kuunda kikosi cha Tanzania kitakashiriki mechi za mchujo za michuano ya Afrika.
Tanzania imepangwa kucheza mechi ya kwanza ya raundi ya kwanza dhidi ya Kenya itakayofanyika kati ya Februari 13 na 15 mwaka huu jijini Mombasa. Mechi ya marudiano itachezwa wiki moja baadaye nchini.
Zanzibar imewasili na kikosi cha wachezaji 14 na viongozi watatu ambacho kitaungana na kile cha Tanzania Bara. Timu hizo zitacheza jumla ya mechi nane kwenye ufukwe wa Escape One uliopo Mikocheni, Dar es Salaam.
Mechi hizo zitachezwa mbili asubuhi na mbili jioni kesho (Januari 24 mwaka huu), na nyingine nne kwa utaratibu huo huo keshokutwa (Januari 25 mwaka huu) kabla ya Kocha John Mwansasu kutaja kikosi cha mwisho Januari 26 mwaka huu.
VPL KUTIMUA VUMBI WIKIENDI
Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaingia raundi ya 12 wikiendi hii kwa mechi saba. Kesho (Januari 24 mwaka huu) kutakuwa na mechi kati ya Polisi Morogoro na Yanga kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Mechi za Jumapili ni kati ya Azam na Simba (Uwanja wa Taifa), Kagera Sugar na Ndanda (Uwanja wa CCM Kirumba), Stand United na Coastal Union (Uwanja wa Kambarage),, Mbeya City na Tanzania Prisons (Uwanja wa Sokoine), Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar (uwanja wa Mabatini), na JKT Ruvu na Mgambo Shooting (Uwanja wa Azam Complex).
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Monday, January 5, 2015

MENEJA WA LIVERPOOL ASEMA HENDERSON NDIYE MRITHI WA VIATU VYA GERRARD.

MENEJA wa klabu ya Liverpool, Brendan Rodgers amempigia chapuo Jordan Henderson kuziba nafasi ya Steven Gerrard wakati nahodha huyo wa timu hiyo atakapoondoka mwishoni msimu huu. 
Gerrard mwenye umri wa miaka 34 amethibitisha Ijumaa iliyopita kuwa hataongeza mkataba mwingine na ataondoka katika majira ya kiangazi huku akihusishwa na kwenda kucheza soka Marekani. 
Henderson amekuwa akionyesha kiwango kizuri chini Rodgers akicheza sambamba na Gerrard na maneja huyo anaamini kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24 ataw
eza kuziba vyema nafasi ya mkongwe huyo atapoondoka.
Akihojiwa Rodgers amesema anadhani Henderson ana haiba ya uongozi na hiyo ndiyo sababu kubwa iliyomfanya kumpatia unahodha msaidizi na pindi Gerrard atakapoondoka anadhani atakuja kuwa kiongozi mzuri kutokana na uzoefu aliopata.