Saturday, May 4, 2013

TUZO 70 ATWAA RONALDO DE LIMA KATIKA ULIMWENGU WA SOKA

Ronaldo de lima katika soka
Taarifa kuhusu yeye
Full name
Ronaldo Luís Nazário de Lima
Date of birth
18 September 1976 (age 36)
Place of birth
Height
1.82 metres (6 ft 0 in)
Playing position
Timu za ujana academi
1986–1989
Tennis Club Valqueire
1989–1990
Social Ramos Club
1990–1993
Timu za ukubwa
Years
Team
mechi
(Goli 
1993–1994
34
(34)
1994–1996
46
(42)
1996–1997
37
(34)
1997–2002
68
(49)
2002–2007
127
(83)
2007–2008
20
(9)
2009–2011
52
(29)
Total
384
(280)
Timu ya taifa
1993
7
(5)
1996
8
(6)
1994–2006, 2011
98
(62

MATAJI ALIYO TWAA  NA VILABU
Cruzeiro
·         Campeonato Mineiro (1): 1994
·         Copa do Brasil (1): 1993
PSV Eindhoven
·         KNVB Cup (1): 1996
·         Johan Cruijff-schaal (1): 1996
Barcelona
·         Copa del Rey (1): 1997
·         UEFA Cup Winners' Cup (1): 1997
·         Supercopa de España (1): 1996
Inter Milan
·         UEFA Cup (1): 1998
Real Madrid
·         La Liga (1): 2002–03
·         Intercontinental Cup (1): 2002
·         Supercopa de España (1): 2003
Corinthians
·         Campeonato Paulista (1): 2009
·         Copa do Brasil (1): 2009

TIMU YA TAIFA
·         FIFA World Cup (2): 1994, 2002
·         FIFA World Cup (1): Runners-up (2nd Place) 1998
·         Copa América (2): 1997, 1999
·         Copa América (1): Runners-up (2nd Place) 1995,
·         FIFA Confederations Cup (1): 1997
·         Summer Olympic Games (1): Bronze Medal (3rd Place) 1996

TUZO BINAFSI ALIZOTWAA"
     1.    Supercopa Libertadores Top Scorer (1): 1993–94
    2. Supercopa Libertadores Team of The Year (1): 1993-04
  3.  Campeonato Mineiro Top Scorer (1): 1993–94
  4        Campeonato Mineiro Team of The Year (1): 1994
  5.         Eredivisie Top Scorer (1): 1994–95
 6.       La Liga Foreign Player of the Year (1): 1996
 7.     European Golden Boot (1): 1996–97
 8.    Don Balón Award La Liga Foreign Player of the Year (1): 1996–97
 9.         Copa América Final Most Valuable Player (1): 1997
10.      Copa América Most Valuable Player (1): 1997
11.         Confederations Cup All-Star Team (1): 1997
12.       Cup Winners Cup Final Most Valuable Player (1): 1997
13.     Cup Winners Cup Top Goal Scorer (1): 1996–1997
14.         IFFHS World's Top Goal Scorer of the Year (1): 1997
15.         UEFA Most Valuable Player (1) 19981
16.        European Sports Media ESM Team of the Year (2) 1996–97, 1997–98
17.         UEFA Most Valuable Player (1): 1997–98
18.       Serie A Footballer of the Year (1): 1997–98
19.         Serie A Foreign Footballer of the Year (1): 1997–98
20.     UEFA Best Forward (1): 1997–98
21.       Bravo Award (3): 1996, 1997, 1998
22.     FIFA World Cup Golden Ball (1): 1998
23.       FIFA World Cup Best player (1): 1998
24.         UEFA Cup Final Most Valuable Player (1): 1998
25.       UEFA Club Footballer of the Year (1): 1997 - 1998
26.         Copa América Top Scorer (1): 1999
27.     Copa América All-Star Team (2): 1997, 1999
28.         Ballon D'or (2): 1997, 2002
29.     Ballon D'or (1): 1996 Ballon d'Or recipients 2nd
30.         Ballon D'or (1): 1998 Ballon d'Or recipients 3nd
31.         World Soccer Magazine World Player of The Year (3): 1996, 1997, 2002
32.       Onze d'Or (2): 1997, 2002
33.         Onze d'Argent (1): 1998
34.        FIFA World Cup Silver Ball (1): 2002
35.         FIFA World Cup All-Star Team (2): 1998, 2002
36.        FIFA World Cup Final Most Valuable Player (1): 2002
37.         FIFA World Cup Dream Team – 2002
38.       FIFA World Cup Golden boot (1): 2002
39.       FIFA World Cup Top Scorer (1): 2002
40        Intercontinental Cup Most Valuable Player (1): 2002
41         Intercontinental Cup Man of the Match (1): 2002
42.         UEFA Club Team of The Year (1): 2002
43.         Laureus World Sports Awards Comeback of the Year (1): 2002
44.         Strogaldo De Legendary Award (1): 2002
46.         FIFA World Cup All-Star Team (2): 1998, 2002
48.         FIFA World Player of the Year (3): 1996, 1997, 2002
49.         FIFA World Player of the Year (1): 1998 2nd
50.         FIFA World Player of the Year (1): 2003 3rd
53.        Trofeo EFE La Liga Ibero-American Player of the Year (2): 1996–97, 2002–03
55.      Pichichi Trophy (2) 1996–1997, 2003-2004
56.      FIFA 100 (2004)
57.         FIFA World Cup All-Time Leading Scorer, 2006
58.       FIFA World Cup Bronze Boot (2): 1998,2006
59.        Brazil national football team Hall of Fame: 2006
60.         Golden Foot award (1): 2006
61.         Serie A Player of the Decade: 1997–2007
62.         France Football (Magazine): Starting eleven of all-time (2007)
63.         Real Madrid Team of the century
64.       Campeonato Paulista Best Player (1): 2009
65.         Honor of Brazilian Football Confederation: 2010
66.         Real Madrid Hall of fame: 2011
67 .        Marca Leyenda: 2011
68.         World Soccer (magazine):Players' All-time ranking (3) 1st Place
69.       World Soccer (magazine): The Greatest Players of the 20th Century (Published December 1999)
70.         Goal.com: Player of a decade: Winner 2000–2010

RAIS WA ZAMANI WA BARKA AFUNGUKA KUHUSU VILANOVA

RAIS wa zamani wa klabu ya Barcelona, Joan Laporta anaamini kuwa klabu hiyo ilifanya uamuzi usiokuwa sahihi kumteua Tito Vilanova kama kocha mkuu mwanzoni mwa msimu wa 2012-2013. Vilanova mwenye umri wa miaka 44 alitajwa kuchukua nafasi ya Pep Guardiola na kupewa mkataba wa mwaka mmoja lakini Laporta anafikiri Vilanova hakuwa tayari kwa nafasi hiyo kwa kipindi kile. Laporta amesema walimteua Vilanova kwasababu walikuwa wanaogopa kuwa nani ataweza kuchukua nafasi ya Guardiola lakini ilikuwa mapema sana kufanya uamuzi huo. Laporta aliendelea kusema kuwa Barcelona walipaswa kutafuta mbadala wa kocha mwingine wakati Vilanova alipokuwa ameondoka kwa matibabu ya kansa nchini Marekani ingawa alikiri ungekuwa uamuzi mgumu kufanya hivyo ila kulikuwa hakuna jinsi.

COSAFA CUP 2013: KUANZA KUTIMUA VUMBI JULAI 6 TAIFA KATIKA MAKUNDI


Kwa mujibu wa Listi ya Ubora ya FIFA iliyotolewa Aprili 11 mwaka huu Waandaaji wa michuano hii  ndio imetumika kuamua Nchi zipi zitaanzia hatua ya Makundi na zipi zitaanza kucheza hatua ya Raundi ya Mtoano ya Robo Fainali.

Kulingana na mfumo wa Mashindano haya, Timu ambazo zitafungwa Robo Fainali nazo zitasonga kwenye Nusu Fainali yao maalum hadi Fainali yao na Mshindi wake atatwaa Ngao.
hivyo Washindi wa Robo Fainali watasonga na Bingwa kwenye Fainali ndie atatwaa Kombe rasmi la 2013 COSAFA CASTLE CUP.

RATIBA:HATUA YA MAKUNDI
6 JULAI 2013
14:30 Tanzania v Mauritius Nkoloma Stadium, Lusaka
17:00 Namibia v  Seychelles Nkoloma Stadium, Lusaka
8 JULAI 2013
14:30 Mauritius v Namibia Nkoloma Stadium, Lusaka
17:00 Tanzania v Seychelles Nkoloma Stadium, Lusaka
10 JULAI 2013
15:00 Tanzania v Namibia Godfrey 'Ucar' Chitalu 107 Stadium, Kabwe
15:00 Mauritius v Seychelles Nkoloma Stadium, Lusaka
KUNDI B:
-Kenya
-Botswana
-Lesotho
-Swaziland
RATIBA:
7 JULAI 2013
13:00 Kenya v Lesotho Godfrey 'Ucar' Chitalu 107 Stadium, Kabwe
15:30 Botswana v Swaziland Godfrey 'Ucar' Chitalu 107 Stadium, Kabwe
9 JULAI 2013
13:00 Lesotho v Botswana Godfrey 'Ucar' Chitalu 107 Stadium, Kabwe
15:30 Kenya v Swaziland Godfrey 'Ucar' Chitalu 107 Stadium, Kabwe
11 JULAI 2013
15:00 Kenya v Botswana Nkoloma Stadium, Lusaka
15:00 Lesotho v Swaziland Godfrey 'Ucar' Chitalu 107 Stadium, Kabwe
RAUNDI YA MTOANO:
HATUA YA ROBO FAINALI:
13 JULAI 2013
13:00 Zimbabwe v Malawi Nkoloma Stadium, Lusaka
15:30 South Africa v Group A winner Nkoloma Stadium, Lusaka
14 JULAI 2013
13:00 Angola v Group B winner Godfrey 'Ucar' Chitalu 107 Stadium, Kabwe
15:30 Zambia v Mozambique Godfrey 'Ucar' Chitalu 107 Stadium, Kabwe
TAZAMA TIMU HIZI KATIKA LISTI  YA UBORA FIFA
*Zambia 45
*South Africa 62
*Angola 94
*Zimbabwe 101
*Mozambique 106
*Malawi 109
*Tanzania 116
*Kenya 122
*Botswana  22
*Namibia 125
*Lesotho 156
*Swaziland 183
*Mauritius 189
*Seychelles 199

AZAM FC NJE KATIKA MICHUANO YA CAF KWA BAO 2-1


Timu ya  Azam FC ya Tanzania imetolewa rasmi  katika Michuano ya CAF ya Kombe la Shirikisho kwa kufungwa Bao 2-1 na FAR Rabat katika Mechi ya Marudiano iliyochezwa Uwanja wa Complexe Sportif Moulay Abdallah, Jijini Rabat Nchini Morocco.
Katika Mechi ya Kwanza iliyochezwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam Wiki mbili zilizopita Timu hizi zilitoka sare ya 0-0.
Nahodha wa Azam, John Bocco, ndie aliefunga bao la kwanza katika Dakika ya 6 na FAR Rabat kusawazisha kwa Penati ya Abderrahim Achakhir na kunako Dakika ya 34 Abderrahim Achakhir huyo huyo alitolewa kwa Kadi Nyekundu kwa Rafu mbaya.
Licha ya kuwa 10 dimbani, FAR Rabat walipata Bao la pili katika Dakika ya 43 mfungaji akiwa Moustapha Allaoui.
Kipindi cha Pili, Azam FC walipata pigo pale katika Dakika ya 55 David Mwantika kupewa Kadi Nyekundu na Nyekundu nyingine kufuatia kwa Wazir Omar katika Dakika ya 74.
Hata hivyo, Azam FC walipata nafasi ya dhahabu katika Dakika ya 82 kwa kupewa Penati lakini John Bocco akakosa kufunga Bao la kusawazisha ambalo lingefanya Mechi iwe 2-2 na Azam kusonga kwa Bao za ugenini.
KIKOSI CHA AZAM:
Mwadini, Himidi, Waziri, Mwantika, Atudo, Bolou, Umony, Salum Abubakar, Bocco, Mieno, Kipre
Akiba: Aishi, Mwaipopo, Mwaikimba, Abdi Kassim, Mcha Viali, Jabir, Luckson
CAF KOMBE LA SHIRIKISHO
RAUNDI YA PILI YA MTOANO
RATIBA/MATOKEO:
Ijumaa Mei 3
[Kwenye Mabano Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili]
Al Ismaily – Egypt 0 FC Ahli Shandi – Sudan 0 [4-3]
Jumamosi Mei 4
[Kwenye Mabano Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili]
FAR Rabat – Morocco 2 Azam FC– Tanzania 1 [2-1]
Union Sportive Bitam – Gabon 0 Union Sportive Médina d'Alger – Algeria 3 [0-3]
Supersport United - South Africa 1 Enppi – Egypt 3 [1-3]
Lydia LB Académi – Burundi 2 ASEC Mimosas Abidjan - Ivory Coast 0 [2-1]
E.S. Sahel – Tunisia 6 Recreativo Da Caala - Angola 1[7-2]
Jumapili Mei 5
[Kwenye Mabano Matokeo ya Kwanza]
Wydad Athletic Club – Morocco v Liga Muculmana de Maputo – Mozambique [0-2]Diables Noirs – Congo v Club Sportif Sfaxien – Tunisia [1-3]

Friday, May 3, 2013

SEPP BLLATTER - AWEKA NIA YA KUGOMBEA TENA URAIS WA FIFA

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Sepp Blatter ametoa dondoo ya kwamba ana mpango wa kugombea tena nafasi hiyo kwa miaka minne mingine wakati wa hotuba yake mara baada ya mkutano na viongozi wa Shirikisho la Soka la Asia-AFC nchini Malaysia. Mapema Machi mwaka huu Blatter amesema ana mpango kwa kuachia ngazi wakati atakapomaliza kipindi chake cha miaka minne kitakapoisha mwaka 2015 lakini akaongeza kuwa ataachia nafasi hiyo pale atakapoamini kwamba atakayemwachia anaweza kulisongesha mbele gurudumu la shirikisho hilo. Blatter mwenye umri wa miaka 77 alirudia tena kauli ya katika mkutano wa AFC jijini Kuala Lumpur jana akidai kuwa yeye ni nahodha na hawezi kuachia meli yake izame wakati bado anaona ana nguvu za kuizuia isifanye hivyo. Kauli hiyo ya Blatter imewafanya wachambuzi wa mambo ya soka wadai kuwa rais huyo ana mpango wa kugombea urais kwa kipindi kingine baada ya kumaliza hiki cha sasa mwaka 2015. Rais wa Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA, Michel Platini ambaye alikuwepo katika mkutano huo ambao ulishuhudia Sheikh Salman Bin Ebrahim Al Khalifa wa Bahrain akiteuliwa kuwa rais wa AFC, ndiye anayepewa nafasi kubwa ya kushika nafasi ya Blatter atakapoacia madaraka. 

BENITEZ AWATAKA MASHABIKI WA CHELSEA KUMUHESHIMU


Rafael Benitez kocha wa muda wa chelsea amesema anastahili kuheshima kwa kuipeleka Chelsea kutinga Fainali ya EUROPA LIGI ambapo watakutana na Benfica huko Amsterdam ArenA hapo Mei 15.








Wakiwa katika dimba la uwanja wa Stamford Bridge katika Mechi ya Marudiano ya
Nusu Fainali ya EUROPA LIGI na FC Basel huku wakiwa wameshinda Bao 2-1
toka Mechi ya kwanza, Chelsea walitanguliwa Bao 1-0 hadi Mapumziko
 lakini Kipindi cha Pili waliisambaratisha Basel kwa kuitandika Bao 3 ndani ya
Dakika 9 kwa Bao za Torres, Moses na Luiz.
MAGOLI:
Chelsea 3
*Torres Dakika ya 50
*Moses 52
*Luiz 59
FC Basel 1
*Salah Dakika ya 45
Hii ni Fainali ya 10 kwenye himaya ya Mmiliki Roman Abramovic huku
 Chelsea wakitwaa  Mataji 11 na watakuwa wakiwania Rekodi ya kuwa
 Klabu ya 4 Barani Ulaya kuweza kutwaa Mataji yote makubwa ya Ulaya
yakiwemo UEFA CUP WINNERS CUP [Kombe la Washindi] na
UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Chelsea, ambao walitwaa Kombe ambalo sasa halipo, Kombe la Washindi,
mara mbili Miaka ya 1970/71 na 1997/98, pamoja na la Klabu Bingwa Ulaya Mwaka jana
, hawajawahi kutwaa UEFA CUP, ambalo sasa ndio EUROPA LIGI.
Klabu nyingine 3 ambazo zimefuzu kutwaa Mataji yote hayo makubwa ni Juventus, Ajax
 na Bayern Munich.
MAKOMBE ENZI ZA ABRAMOVICH:
*BPL 3
*FA CUP 3
*KOMBE LA LIGI 2
*UEFA CHAMPIONZ LIGI 1
*NGAO YA HISANI 2

LIEWIG AFUNGUKA KUHUSU MECHI NA WATANI ZAO WA JADI


Kocha Mkuu wa Wekundu wa msimbazi Simba, Patrick Liewig amesema kuwa silaha yake kubwa katika mechi dhidi ya Yanga  may 18 mwaka huu ni kasi ya wachezajiwake, ingawa amekiri wanatakiwa kuwa makini kwa dakika zote 90 za mchezo.

Mfaransa huyo alisema jijini Dar es Salaam kuwa tayari wamepoteza ubingwa wa ligi pamoja na nafasi ya pili ambayo
ingeweza kuifanya timu hiyo ishiriki Kombe la CAF mwakani.
aidha amesema hakuna  nafasi tena ya kushinda taji la ligi kwa msimu huu wala kumaliza katika nafasi ya pili ambayo ingetupa fursa ya kushiriki Kombe la CAF mwakani.

kubwa zaidi Kilichobaki ni kulinda heshima yetu kwa kuwafunga mabingwa (Yanga) katika mchezo wetu wa mwisho hiyo Mei 18. Timu yangu ya Simba ina wachezaji wengi vijana ambao wana kasi kubwa kuwazidi Yanga." alisema kocha huyo aliyerithi mikoba ya Mserbia Milovan Cirkovic aliyetupiwa virago na klabu hiyo mwaka jana.
Kocha huyo ameongeza na kusema kuwa Yanga ni timu nzuri hakuna mtu anayepinga hilo, lakini haiwezi kumudu kasi ya wachezaji wangu vijana.

hata hivyo liewing amesema Nimewaona katika mechi kadhaa za ligi, wanacheza vizuri ingawa sitaki kuaminikwamba watashinda mbele ya vijana wangu imara."
Liewig amesema katika kambi ya kujiwinda na mchezo huo ataongeza muda wa programu yake ya mazoezi kuhakikisha kikosi chake kinakuwa katika hali nzuri ya ufiti kabla ya kukutana na watani hao wa jadi katika soka la Tanzania Bara na kuharibu sherehe za ubingwa huo.