Samatta au ‘Sama Goal’ aliifungia bao muhimu la ugenini Jumapili iliyopita Mazembe ikifungwa 2-1 mjini Abidjan na leo wakiwa nyumbani watahitaji japo ushindi wa 1-0 ili kusonga mbele.
Kumbuka mwaka jana Mazembe ilitolewa katika hatua hii ya 16 Bora na Orlando Pirates ya Afrika Kusini iliyofika hadi fainali na kufungwa na Al Ahly ya Misri.
Mazembe iliangukia kwenye Kombe la Shirikisho ambako pia ilifika fainali na kufungwa na CS Sfaxien ya Tunisia.
![]() |
Mbwana Samatta |
Timu
hiyo ya Moise Katumbi safari hii imepania kurudi kwenye hatua ya
makundi ya Ligi ya Mabingwa na imejiandaa kiasi cha kutosha kujaribu
kufuzu mtihani huo mgumu. Kila la heri Samatta na Ulimwengu pamoja na TP
Mazembe.
Mechi
nyingine za leo ni kati ya mabingwa watetezi, Al Ahly ya Misri dhidi ya
Ahly Benghazi ya Libya itakayochezwa mjini Cairo, CS Sfaxien ya Tunisia
itakayokuwa mwenyeji wa Horoya ya Guinea, Kaizer Chiefs ya Afrika
Kusini itaikaribisha AS Vita ya DRC.
Michuano hiyo itaendelea kesho wakati Zamalek ya Misri itakapokuwa mwenyeji wa Nkana ya Zambia, Coton Sport ya Cameroon na ES Setif ya Algeria, Esperance ya Tunisia na AS Bamako ya Mali, Al-Hilal ya Sudan na AC Leopards ya Kongo.
Michuano hiyo itaendelea kesho wakati Zamalek ya Misri itakapokuwa mwenyeji wa Nkana ya Zambia, Coton Sport ya Cameroon na ES Setif ya Algeria, Esperance ya Tunisia na AS Bamako ya Mali, Al-Hilal ya Sudan na AC Leopards ya Kongo.