Saturday, March 29, 2014

KITENDALIWI BADO KIPO KUTWAA UBINGWA VPL NANI KATI YA AZAM au YANGA.

Utata wa klabu gani itatwaa Ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara msimu huu hakichateguliwa kwasasa, na hapo kesho kutakuwa na  mechi muhimu kwa timu zinazopigiwa upatu  wa kutwaa ubingwa, Yanga na Azam fc.Vinara Azam fc watakuwa uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kukabiliana na kikosi cha Simba, wakati mabingwa watetezi, Young Africans watakuwa na kibarua kizito mbele ya wapiga kwata wa Mgambo JKT, kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani, jijini Tanga.
SAM_2252
Mechi ya Azam fc dhidi ya Simba sc itakuwa ngumu kwa klabu zote, lakini kwa Wana Lambalamba ina uzito wa hali ya juu katika mbio zao za kutwaa ubingwa.
Kama watapoteza mechi hiyo, halafu Yanga wakapata ushindi jijini Tanga, Azam watajiweka mazingira magumu zaidi ya kubeba mwari wao wa kwanza tangu waingie  ligi kuu msimu wa 2008/2009.
SAM_2257Yanga nao watatakiwa kuwa na mipango mizuri ya uwanjani dhidi ya Magambo kesho, kwasababu rekodi ya nyuma inaonesha wapinzani wao wamekuwa wagumu kufungwa Mkwakwani.
Hukutakuwa na sababu yoyote kwa kikosi cha Yanga kuwadharau Mgambo kwakuwa wapo katika mstari mwekundu wa kushuka daraja.
Maskari hawa wa  Jeshi la kujenga Taifa wanahitaji ushindi kwa nguvu zote kwasababu ndio matokeo pekee yanayowafaa kwasasa.
VPL-LIGI KUU VODACOM
RATIBA:
Jumamosi Machi 29
Ashanti United v JKT Oljoro
Jumapili Machi 30
Mbeya City v Tanzania Prisons
Kagera Sugar v Ruvu Shooting
Mtibwa Sugar v Coastal Union
JKT Ruvu v Rhino Rangers
Azam FC v Simba
Mgambo JKT v Yanga 
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
PTS
1
Azam FC
22
14
8
0
30
50
2
Yanga SC
21
13
7
1
27
46
3
Mbeya City
22
11
9
2
12
42
4
Simba SC
22
9
9
4
16
36
5
Kagera Sugar
21
8
8
5
3
32
6
Coastal Union
22
6
11
5
2
29
7
Ruvu Shooting
20
7
7
6
-4
28
8
Mtibwa Sugar
21
6
8
7
-1
26
9
JKT Ruvu
22
8
1
13
-15
25
10
Prisons FC
21
3
10
8
-9
19
11
Ashanti United
21
4
6
11
-18
18
12
Mgambo JKT
21
4
6
11
-19
18
13
JKT Oljoro
22
2
9
11
-17
15
14
Rhino Rangers
22
2
7
13
-17

13