Saturday, April 5, 2014

BPL:CHELSEA YAKWEA KILELENI MWA LIGI HIYO:

MATOKEO:
Jumamosi 5 Aprili 2014
Man City 4 Southampton 1
Aston Villa 1 Fulham 2
Cardiff City 0 Crystal Palace 3
Hull 1 Swansea 0
Newcastle 0 Man United 4
Norwich 0 West Brom 1
Chelsea 3 Stoke 0
CLUB ya Chelsea imefanikiwa  kurudi kileleni mwa Ligi Kuu England baada ya hii Leo kuitandika Stoke City Bao 3-0 Uwanjani Stamford Bridge na kukalia nafasi hiyo wakiwa Pointi 1 mbele ya Liverpool na mbili mbele ya Man City walio Nafasi ya 3 lakini wao wamecheza Mechi 1 zaidi ya Liverpool na 2 zaidi ya City.
Goli la Kijana mahiri wa Misri, Mohamed Salah, ambae Leo ndio alianza Mechi ya Ligi kwa mara ya kwanza alipofunga katika Dakika ya 3.
Frank Lampard alifunga Bao la Pili katika Dakika ya 61 baada ya Penati yake kuokolewa na Kipa Begovic na mwenyewe kuitokea tena na kumalizia.
Penati hiyo ilitolewa kufuatia Mohamed Salah kuangushwa na Andy Wilkinson ndani ya Boksi.
Willian alipachika Bao tamu la 3 katika Dakika ya 72 kwa Shuti safi nje ya Boksi.
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA
[Saa za Bongo]
Jumapili 6 Aprili 2014
1530 Everton v Arsenal
1800 West Ham v Liverpool
Jumatatu 7 Aprili 2014
2200 Tottenham v Sunderland
MSIMAMO:
NA TIMU P W D L F A GD PTS
1 Chelsea 33 22 6 5 65 24 41 72
2 Liverpool 32 22 5 5 88 39 49 71
3 Manchester City 31 22 4 5 84 29 55 70
4 Arsenal 32 19 7 6 56 37 19 64
5 Everton 31 17 9 5 49 31 18 60
6 Manchester United 33 17 6 10 56 38 18 57
7 Tottenham Hotspur 32 17 5 10 40 44 -4 56
8 Southampton 33 13 9 11 50 44 6 48
9 Newcastle United 33 14 4 15 38 51 -13 46
10 Stoke City 33 10 10 13 37 48 -11 40
11 West Ham United 32 10 7 15 36 42 -6 37
12 Hull City 33 10 6 17 34 40 -6 36
13 Aston Villa 32 9 7 16 35 48 -13 34
14 Crystal Palace 32 10 4 18 23 39 -16 34
15 Swansea City 33 8 9 16 45 49 -4 33
16 West Bromwich Albion 32 6 14 12 37 48 -11 32
17 Norwich City 33 8 8 17 26 52 -26 32
18 Fulham 33 8 3 22 33 74 -41 27
19 Cardiff City 33 6 8 19 29 64 -35 26
20 Sunderland 30 6 7 17 28 48 -20 25

SIMBA YABANWA NA KAGERA,HUKU MBEYA CITY IKIVUTWA SHATI NA ASHANTI

MATOKEO
Jumamosi Aprili 5
Kagera Sugar 1 Simba 1
Ashanti United 0 Mbeya City 0
Katika Michezo miwiili pekee iliyopigwa ya VPL, Ligi Kuu Vodacom, zilizochezwa LEO, Kagera Sugar na Simba zilitoka Sare ya Bao 1-1 huko Kaitaba, Mjini Bukoba na huko Azam Complex, Chamazi, kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salaam, Ashanti United ilitoka 0-0 na Mbeya City.
Huko Kaitaba, Simba walitangulia kufunga katika Dakika ya 45 kwa Bao la Zahor Pazi na Kagera Sugar kusawazisha Dakika ya 51 kwa Bao la Themi Felix.
Ligi itaendelea hapo kesho na zipo Mechi 4 ikiwemo ile ya Yanga v JKT Ruvu Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.

VPL: LIGI KUU VODACOM
RATIBA:
Jumapili Aprili 6
Coastal Union v Mgambo JKT
JKT Oljoro v Tanzania Prisons
Rhino Rangers v Mtibwa Sugar
Yanga v JKT Ruvu
Jumatano Aprili 9
Ruvu Shooting v Azam FC
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
PTS
1
Azam FC
23
15
8
0
31
53
2
Yanga SC
22
13
7
2
26
46
3
Mbeya City
24
12
10
2
13
46
4
Simba SC
24
9
10
5
15
37
5
Kagera Sugar
23
8
10
5
3
34
6
Mtibwa Sugar
22
7
8
7
1
29
7
Coastal Union
23
6
11
6
0
29
8
Ruvu Shooting
21
7
8
6
-4
29
9
JKT Ruvu
23
9
1
13
-13
28
10
Ashanti United
23
5
7
11
-17
22
11
Mgambo JKT
22
5
6
11
-18
21
12
Prisons FC
22
3
10
9
-10
19
13
JKT Oljoro
23
2
9
12
-18
15
14
Rhino Rangers
23
2
7
14
-19
13

TAIFA STARS, BURUNDI KUCHEZA APRILI 26

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itacheza mechi ya kirafiki na Burundi (Intamba Mu Rugamba) Aprili 26 mwaka huu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari ipo kambini Tukuyu mkoani Mbeya ikijiandaa kwa ajili ya mechi hiyo ikiwa na wachezaji waliopatikana katika programu maalumu ya kusaka vipaji.
Baadaye wachezaji wengine wa Taifa Stars ambao wapo nje ya programu ya kusaka vipaji wataungana na wenzao kabla ya kutengeneza kikosi cha mwisho kitakachoivaa Burundi.
Mechi hiyo itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itachezeshwa na waamuzi wanaotambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kutoka nchini Kenya.
TIMU YA WATOTO WA MITAANI YACHACHAFYA BRAZIL
Timu ya Watoto wa Mitaani ya Tanzania imefanikiwa kuingia nusu fainali ya mashindano ya Kombe la Dunia yanayofanyika Rio de Janeiro nchini Brazil baada ya jana kuifunga Indonesia kwa jumla ya mabao 5-3.
STREET_CHILD
Hadi muda wa kawaida wa mchezo huo unamalizika timu hizo zilikuwa zimefungana mabao 2-2 ndipo ikatumia mikwaju ya penalti kuamua mshindi. Tanzania ilipata penalti tatu dhidi ya moja ya wapinzani wao.
Kwa matokeo hayo, Tanzania sasa itacheza mechi ya nusu fainali leo dhidi ya Marekani ili kupata timu zitakazocheza mechi za fainali na kutafuta mshindi wa tatu. Mechi za fainali na kutafuta mshindi wa tatu zitachezwa kesho (Aprili 6 mwaka huu).
Timu nyingine zilizoingia nusu fainali na mechi zake zinachezwa leo (Aprili 5 mwaka huu) ni Burundi itakayocheza na Pakistan.
Katika mechi zilizopita, Tanzania ilitoka sare ya mabao 2-2 na Burundi, ikaitandika Argentina mabao 3-0 ikailaza Nicaragua mabao 2-0 na ikafungwa na Philippines mabao 2-0.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)