Friday, April 18, 2014

PAZIA VPL LAFUNGWA, AZAM KUKABIDHIWA KOMBE CHAMAZI

Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inafikia tamati kesho (Aprili 19 mwaka huu) kwa timu zote 14 kuwa viwanjani, huku mabingwa wapya Azam wakikabidhiwa kombe lao Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam katika mechi yao dhidi ya JKT Ruvu.

Mechi zote saba zitachezwa kuanzia saa 10 kamili jioni ambapo Yanga na Simba zitakuwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa mechi ambayo viingilio vyake ni sh. 7,000 kwa viti vya bluu na kijani, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 20,000 kwa VIP C na B wakati VIP A itakuwa sh. 30,000.

Tayari tiketi zimeanza kuuzwa leo (Aprili 18 mwaka huu) katika vituo saba vya; Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Kariakoo (Kidongo Chekundu), Buguruni Shell, mgahawa wa Steers uliopo Mtaa wa Ohio na Samora, Ubungo OilCom, Dar Live Mbagala na Uwanja wa Taifa.

Mechi nyingine zitakuwa kati ya Tanzania Prisons na Ashanti United (Uwanja wa Jamhuri, Morogoro), Rhino Rangers na Ruvu Shooting (Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora), Mbeya City na Mgambo Shooting (Uwanja wa Sokoine, Mbeya), Oljoro JKT na Mtibwa Sugar (Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha) na Coastal Union na Kagera Sugar (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga).
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1 
Azam FC
25
17
8
0
50
15
35
59
2 
Young Africans
25
16
7
2
60
18
42
55
3
Mbeya City
25
12
10
3
32
20
12
46
4
Simba SC
25
9
10
6
40
26
14
37
5
Kagera Sugar
25
8
11
6
22
20
2
35
6
Ruvu Shooting
25
9
8
8
26
32
-6
35
7
JKT Ruvu
25
10
1
14
23
39
-16
31
8
Mtibwa Sugar
25
7
9
9
29
30
-1
30
9
Coastal Union
25
6
11
8
16
19
-3
29
10
Mgambo JKT
25
6
8
11
18
34
-16
26
11
Tanzania Prisons
25
5
10
10
25
33
-8
25
12
Ashanti United
25
6
7
12
20
38
-18
25
13
JKT Oljoro
25
3
9
13
18
36
-18
18
14
Rhino Rangers
25
3
7
15
18
37
-19
16
MICHUANO YA BEACH SOCCER KUANZA JUMAPILI
Michuano ya mpira wa miguu ya ufukweni (Beach Soccer) inazinduliwa rasmi keshokutwa (Aprili 20 mwaka huu) kwenye ufukwe wa Escape One uliopo Mikocheni, Dar es Salaam na kushirikisha timu 13.

Uzinduzi huo utaanza saa 5 asubuhi na mechi zitachezwa hadi saa 11 jioni. Michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya kwanza nchini inashirikisha timu 13 kutoka vyuo mbalimbali vya jijini Dar es Salaam.

Vyuo hivyo ni Chuo Kikuu cha Ardhi (AU), Chuo Kikuu cha St. Joseph Tanzania (SJUIT), Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam (TUDARCO), Chuo cha Ustawi wa Jamii (ISW), Chuo cha Uandishi wa Habari Dar es Salaam (DSJ) na Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.

Vingine ni Chuo cha Utumishi wa Umma Magogoni, Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Chuo cha Utawala wa Kodi (ITA) na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).

Michuano hiyo itakuwa inachezwa Jumamosi na Jumapili kwenye fukwe za Escape One na Gorilla Beach iliyopo Kigamboni, Dar es Salaam.

WAZOEFU TAIFA STARS KUTAJWA KESHO
Wachezaji wazoefu wa Taifa Stars watakaoungana na wale 16 waliopatikana katika mpango wa maboresho wa timu hiyo watatangazwa kesho (Aprili 19 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itapiga kambi kwenye hoteli ya Kunduchi Beach kujiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Burundi itakayochezwa Aprili 26 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Wachezaji waliopatikana katika mpango wa maboresho ya Stars wanatarajiwa kuwasili leo (Aprili 18 mwaka huu), na kwenda moja kwa moja kambini kuwasubiri wenzao watakaotajwa kesho (Aprili 19 mwaka huu).

Wachezaji hao ni kipa Benedicto Tinoko Simwanda (Mara), Emma Namwondo Simwanda (Temeke), Joram Nason Mgeveje (Iringa), Omari Ally Kindamba (Temeke), Edward Peter Mayunga (Kaskazini Pemba), Shiraz Abdallah Sozigwa (Ilala), Yusuf Suleiman Mlipili (Temeke) na Said Juma Ally (Mjini Magharibi).

Wengine ni Abubakar Ally Mohamed (Kusini Unguja), Hashim Ramadhan Magona (Shinyanga), Omari Athumani Nyenje (Mtwara), Chunga Said Zito (Manyara), Mohammed Seif Saidi (Kusini Pemba), Ayoub Kasim Lipati (Ilala), Abdurahman Othman Ally (Mjini Magharibi) na Paul Michael Bundara (Ilala).

BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Thursday, April 17, 2014

WACHEZAJI MABORESHO TAIFA STARS 16 WATAJWA

WACHEZAJI MABORESHO STARS WATAJWA
Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Salum Mayanga ametangaza majina ya wachezaji 16 waliochaguliwa katika maboresho ya timu ya Taifa Taifa Stars kwenye hoteli ya Hill View jijini Mbeya.
TFF_LOGO12Wachezaji hao ni kipa Benedicto Tinoko Simwanda (Temeke), mabeki wa kati; Emma Namwondo Simwanda (Temeke) na Joram Nason Mgeveje (Iringa). Walinzi wa pembeni ni Omari Ally Kindamba (Temeke), Edward Peter Mayunga (Kaskazini Pemba) na Shiraz Abdallah Sozigwa (Ilala).
Viungo ni Yusuf Suleiman Mlipili (Temeke), Said Juma Ally (Mjini Magharibi), Abubakar Ally Mohamed (Kusini Unguja), Hashim Ramadhan Magona (Shinyanga), Omari Athumani Nyenje (Mtwara) na Chunga Said Zito (Manyara).
Washambuliaji ni Mohammed Seif Saidi (Kusini Pemba), Ayoub Kasim Lipati (Ilala), Abdurahman Othman Ally (Mjini Magharibi), Paul Michael Bundara (Ilala). Wachezaji wa U 20 ni Mbwana Mshindo Musa (Tanga) na Bayaga Atanas Fabian (Mbeya).
Alisema mpango huu wa kuboresha timu ya Taifa ambayo inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ni endelevu na kusisitiza kuwa hata wale 18 walioachwa watafuatiliwa na TFF na kuitwa panapokuwa na mahitaji.
“Hawa wote wapo kwenye database ya TFF na hawataachwa tu hivi hivi wapotee,” alisema kocha Mayanga.
Wachezaji ha0 waliingia kambini mjini Tukuyu, Machi 21 mwaka huu na wamefanya mazoezi kwa pamoja kwa karibu wiki nne sasa kabla ya kuchujwa.
Wachezaji 16 waliochaguliwa wanatarajiwa kuondoka Tukuyu kesho (Aprili 18 mwaka huu) na kwenda kwenye kambi ya Taifa Stars katika Hoteli ya Kunduchi ambapo wataungana na wachezaji wa Taifa Stars wa siku zote.
Baadaye watachujwa tena ili ipatikane timu moja ya Taifa iliyoboreshwa.
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Kilimanjro Premium Lager inaunga mkono utaratibu huu wa maboresho ya Taifa na imewekeza zaidi ya dola milioni 2 kwa mwaka kudhamini Taifa Stars. Huu ndio udhamini mkubwa zaidi ambao Stars imewahi kupata tangu kuanzishwa kwa TFF.
LIGI YA MABINGWA WA MIKOA KUANZA MEI 10
Michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) itakayochezwa kwa ligi ya mkondo mmoja katika vituo vitatu vya timu tisa kila kimoja inatarajia kuanza Mei 10 mwaka huu.
Timu ya kwanza kutoka katika kila kituo ndiyo itakayopanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu wa 2014/2015. Kwa vile ligi hii haina mdhamini, hivyo timu zitajigharamia kwa kila kitu.
Vituo vitakavyotumika kwa ajili ya RCL, kanuni pamoja na ratiba vitatangazwa kabla ya kuanza kwa ligi hiyo. Pia kituo kitakachoteuliwa kwa ajili ya ligi hiyo, timu yake haitapangwa katika kituo husika ikiwa ni moja ya njia ya kuhakikisha kanuni ya mchezo wa kiungwana (fair play) inazingatiwa.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Tuesday, April 15, 2014

DRFA YAIPA HONGERA AZAM FC KUTWAA UBINGWA

CHAMA Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) kimeipongeza timu ya Azam FC kwa kufanikiwa kwa mara ya kwanza kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2013/2014.

Azam FC ili

jihakikishia kutwaa ubingwa huo Jumapili baada ya kuifunga timu ya Mbeya City mabao 2-1 katika mchezo wa ligi hiyo uliochezwa kwenye Uwanja wa Sokoine.

Ofisa Habari wa DRFA Mohamed Mharizo alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa ubingwa huo wa Azam ni kielelzo cha kujituma kwao na kuwa na ushirikiano na walistahili kutwaa taji hilo.

“Kwa niaba ya DRFA nachukua fursa hii kuwapongeza wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wa timu ya Azam FC kwa ujumla, kwa kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
“Ni imani yetu DRFA kuwa timu hiyo itawakilisha vyema nchi katika michuano ya Klabu Bingwa barani Afrika, tunawatakia kila la kheri katika michuano hiyo.
“Lakini pia tunaipongeza Yanga kwa kushika nafasi ya pili katika ligi hiyo, nao tunawatakia kila la kheri katika michuano ya Kombe la Shirikisho. Sisi Mkoa tunafarijika sana kuona timu zetu za Mkoa wa Dar es Salaam zinavyofanya vizuri,” alisema.

Monday, April 14, 2014

KATIBU MKUU FIFA JEROME VALCKE KUFUNGUA SEMINA DAR

KATIBU MKUU WA FIFA KUFUNGUA SEMINA DAR

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Jerome Valcke atawasili nchini Mei 1 mwaka huu ambapo atafungua semina ya mawasiliano itakayoshirikisha viongozi wa vyama wanachama wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).
Akizungumza Dar es Salaam leo (Aprili 14 mwaka huu), Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amesema Valcke ambaye hii ni mara yake ya kwanza kuja Tanzania atafuatana na maofisa wengine wa saba wa FIFA.
Amesema semina hiyo iliyoandaliwa na FIFA itafanyika kwa siku mbili (Mei 1 na 2 mwaka huu) ambapo vilevile Valcke atapata fursa ya kuzungumza na waandishi wa habari wa ndani na wa kimataifa.
TFF_LOGO12Rais Malinzi amesema washiriki wa semina hiyo ni marais, makatibu wakuu na wakuu wa mawasiliano wa wanachama 12 wa CECAFA ambao ni Burundi, Djibouti, Eritrea, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Somali, Sudan, Sudan Kusini, Tanzania na Uganda.
Naye Mwenyekiti wa CECAFA, Leodegar Tenga ambaye alifuatana na Katibu Mkuu wake Nicholas Musonye amemshukuru Rais wa TFF kwa kukubali kuwa mwenyeji wa semina hiyo kwani itasaidia katika maendeleo ya mpira wa miguu katika ukanda huu.
RAMBIRAMBI MSIBA WA JOSEPHAT MAGAZI
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha Mwenyekiti wa Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu (FRAT) Mkoa wa Singida, Josephat Magazi kilichotokea jana mkoani Kilimanjaro.
Magazi ambaye pia aliwahi kuwa mwamuzi na kamishna wa mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) alikuwa amelazwa katika Hospitali ya KCMC. Mazishi yatafanyika kesho (Aprili 15 mwaka huu) saa 5 asubuhi kwao Ushirombo mkoani Shinyanga.
Msiba huo ni mkubwa katika fani ya mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti Magazi alishirikiana na TFF na wadau wengine wa mpira wa miguu katika masuala ya uamuzi na uongozi, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Magazi, FRAT na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Singida (SHIREFA) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Bwana alitoa, Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe. Amina
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Sunday, April 13, 2014

VPL: AZAM FC YATWAA UBINGWA, YAVUNJA MWIKO WA TANGU 2000

AZAM FC wakiWA katika dimba la Uwanja wa Sokoine, Mbeya, wamefanikiwa kutangaza ubingwa wakiwa na mechi moja mkononi baada kuichalaza mbeya city bao 2-1 na  kuvunja rekodi ya muda mrefu kwa timu zinazoshiriki VPL kutotwaa Ubingwa kwa Klabu nyingine mbali ya Yanga na Simba wa tangu Mwaka 2000.
Azam FC imefuta USIMBA NA UYANGA ambapo Yanga na Simba tangu Mwaka 2001 ambapo, baada ya Mtibwa kuutwaa Mwaka 2000 na kuutetea Mwaka 2001, Yanga na Simba zimekuwa zikipishana kwa kuubeba.
MSIMAMO-Timu za Juu:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
GF
PTS
1
Azam FC
25
17
8
0
35
50
59
2
Yanga SC
25
16
7
2
42
60
55
3
Mbeya City
25
12
10
3
12
31
46
4
Simba SC
25
9
10
6
14
40
37
Katika Mechi nyingine zilizochezwa Leo, Yanga waliichapa JKT Oljoro Bao 2-1 hukO Arusha na Jijini Dar es Salaam, Simba ilitunguliwa Bao 1-0 na Ashanti United.
VPL itakamilika Wikiendi ijayo Aprili 19 kwa Timu zote 14 kuwa Dimbani.
RATIBA/MATOKEO:
Jumapili Aprili 13
Simba 0 Ashanti United 1 (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam)
Mbeya City 1 Azam 2 (Sokoine, Mbeya)
JKT Oljoro 1 Yanga 2 (Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha).
Mgambo Shooting 1 vs  1 Kagera Sugar (Mkwakwani, Tanga),
MABINGWA WALIOPITA:
1965 Sunderland (Sasa ni Simba SC)
1966 Sunderland
1967 Cosmopolitan
1968 Young Africans
1969 Young Africans
1970 Young Africans
1971 Young Africans
1972 Young Africans
1973 Simba SC
1974 Young Africans
1975 Mseto SC
1976 Simba SC
1977 Simba SC
1978 Simba SC
1979 Simba SC
1980 Simba SC
1981 Young Africans
1982 Pan Africans
1983 Young Africans
1984 Simba SC
1985 Young Africans
1986 Tukuyu Stars
1987 Young Africans
1988 Coastal Union
1989 Young Africans
1990 Simba SC
1991 Young Africans
1992 Young Africans
1993 Young Africans
1994 Simba SC
1995 Simba SC
1996 Young Africans
1997 Young Africans
1998 Young Africans
1999 Mtibwa Sugar
2000 Mtibwa Sugar
2001 Simba SC
2002 Young Africans
2003 Simba SC
2004 Simba SC
2005 Young Africans
2006 Young Africans
2007 Simba SC
2007/08 Young Africans
2008/09 Young Africans
2009/2010 Simba SC
2010/2011 Young Africans
2011/2012 Simba SC
2012/2013 Young Africans

Friday, April 11, 2014

UCL UEFA: SI MCHEZO NUSU FAINALI REAL VS BAYERN, ATLETI VS CHELSEA.

UEFA CHAMPIONZ LIGI Droo ya Mashindano makubwa ya Barani Ulaya imefanyika Leo huko Nyon, Uswisi, na Timu za Spain, Real Madrid na Atletico Madrid zimetenganishwa.
Mabingwa Watetezi Bayern Munich wataivaa Real Madrid na Vinara wa La Liga, Atletico Madrid, watapambana na Chelsea.
UEFA CHAMPIONZ LIGI
NUSU FAINALI:
-Real Madrid v Bayern Munich
-Atletico Madrid v Chelsea
Mechi ya Kwanza: 22 & 23 Aprili
Mechi ya Pili: 29 & 30 Aprili
-FAINALI: Estádio da Luz, Lisbon, Portugal 24 Mei 2014.
EUROPA LIGI:
Kwenye Droo ya Nusu Fainali ya EUROPA LIGI, Klabu za Spain, Sevilla na Valencia zimekutanishwa na Mechi nyingine ni kati ya Benfica ya Ureno na Mabingwa wa Italy, Juventus.
EUROPA LIGI:
NUSU FAINALI:
-Sevilla v Valencia
-Benfica v Juventus
Mechi ya Kwanza: Aprili 24
Mechi ya Pili: Mei 1
FAINALI: Jumatano Mei 14, Juventus Stadium, Turin, Italy

VPL: MOTO KUWAKA KESHOSIMBA, ASHANTI UTD KUVAANA TAIFA

CHACHA KUCHEZESHA MICHUANO YA AYG
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua mwamuzi msaidizi wa Tanzania anayetambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Ferdinand Chacha ameteuliwa kuchezesha michezo ya Vijana ya Afrika (AYG- African Youth Games).

Michezo hiyo ya kwanza ya Afrika itachezesha jijini Gaborone, Botswana kuanzia Mei 22-31 mwaka huu. Tanzania pia itashiriki katika mashindano hayo ya vijana wenye umri chini ya miaka 15.

SIMBA, ASHANTI UTD KUVAANA TAIFA
Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaendelea kesho(Aprili 12 mwaka huu)  katika raundi ya 25 ambapo Simba na Ashanti United zitapambana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.

Mechi nyingine zitakuwa kati ya Tanzania Prisons na Rhino Rangers (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, jijini Mbeya) wakati Coastal Union itakuwa mwenyeji wa JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Keshokutwa (Aprili 13 mwaka huu) kutakuwa na mechi nyingine nne za kukamilisha raundi hiyo. Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya wenyeji Oljoro JKT na Yanga.

Mtibwa Sugar itacheza na Ruvu Shooting (Uwanja wa Manungu, Morogoro), Mgambo Shooting na Kagera Sugar zitaoneshana kazi kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga huku Mbeya City ikiumana na Azam kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

TIMU YA WATOTO WA MITAANI YATAMBULISHWA BUNGENI
Timu ya Watoto wa Mitaani ya Tanzania iliyotwaa ubingwa wa Dunia wa Watoto wa Mitaani nchini Brazil baada ya kuifunga Burundi mabao 3-1 kwenye fainali imetambulishwa leo (Aprili 11 mwaka huu) katika Bunge Maalumu la Katiba mjini Dodoma.

Baadaye timu hiyo leo itapata chakula cha mchana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda. Saa 10 jioni itatembeza kombe hilo katika maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Dodoma katika gari za wazi.

Jioni imeandaliwa hafla maalumu ya chakula pamoja na burudani hapo hapo mjini Dodoma ambapo mgeni rasmi atakuwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara.

MWENYEKITI WA CECAFA KUZUNGUMZA NA WAANDISHI
Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Leodegar Tenga atakuwa na mkutano na waandishi wa habari Jumatatu (Aprili 14 mwaka huu).

Mkutano huo utafanyika kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) zilizopo Ghorofa ya 3, Jengo la PPF Tower mtaa wa Ohio/Garden Avenue kuanzia saa 5 kamili asubuhi.

BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)