Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa
Stars) itacheza mechi ya kirafiki na Burundi (Intamba Mu Rugamba) Aprili 26
mwaka huu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya muungano wa Tanganyika
na Zanzibar.
Taifa
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari ipo kambini Tukuyu
mkoani Mbeya ikijiandaa kwa ajili ya mechi hiyo ikiwa na wachezaji
waliopatikana katika programu maalumu ya kusaka vipaji.
Baadaye
wachezaji wengine wa Taifa Stars ambao wapo nje ya programu ya kusaka vipaji
wataungana na wenzao kabla ya kutengeneza kikosi cha mwisho kitakachoivaa
Burundi.
Mechi
hiyo itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itachezeshwa na waamuzi wanaotambuliwa
na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kutoka nchini Kenya.
TIMU
YA WATOTO WA MITAANI YACHACHAFYA BRAZIL
Timu
ya Watoto wa Mitaani ya Tanzania imefanikiwa kuingia nusu fainali ya mashindano
ya Kombe la Dunia yanayofanyika Rio de Janeiro nchini Brazil baada ya jana
kuifunga Indonesia kwa jumla ya mabao 5-3.
Hadi
muda wa kawaida wa mchezo huo unamalizika timu hizo zilikuwa zimefungana mabao
2-2 ndipo ikatumia mikwaju ya penalti kuamua mshindi. Tanzania ilipata penalti
tatu dhidi ya moja ya wapinzani wao.
Kwa
matokeo hayo, Tanzania sasa itacheza mechi ya nusu fainali leo dhidi ya
Marekani ili kupata timu zitakazocheza mechi za fainali na kutafuta mshindi wa
tatu. Mechi za fainali na kutafuta mshindi wa tatu zitachezwa kesho (Aprili 6 mwaka
huu).
Timu
nyingine zilizoingia nusu fainali na mechi zake zinachezwa leo (Aprili 5 mwaka
huu) ni Burundi itakayocheza na Pakistan.
Katika
mechi zilizopita, Tanzania ilitoka sare ya mabao 2-2 na Burundi, ikaitandika
Argentina mabao 3-0 ikailaza Nicaragua mabao 2-0 na ikafungwa na Philippines
mabao 2-0.
BONIFACE
WAMBURA
OFISA
HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO
LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)