Monday, January 26, 2015

FDL KUSIMAMA KUPISHA VIPORO VYA POLISI MARA

Mechi za raundi ya 20, 21 na 22 za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kwa makundi yote zimesimamishwa ili kupisha Polisi Mara imalize mechi zake za viporo, na timu zote zicheze mechi zao za raundi zilizobaki kwa pamoja.
Polisi Mara ilifungiwa kutumia Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma kutokana na vurugu zilizojitokeza kwenye mechi zake, hivyo kusababisha kuwepo kwa mechi hizo za viporo dhidi ya JKT Kanembwa na Polisi Tabora.
Tayari Polisi Mara tumeiruhusu itumie tena Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume kwa mechi zake za nyumbani baada ya kuipa onyo kali kutokana na vurugu hizo. Lakini pia mechi zake kwenye uwanja huo zitachezwa chini ya uangalizi.
Uamuzi wa kupisha Polisi Mara imalize mechi zake za viporo una lengo la kuhakikisha mechi zote za raundi tatu za mwisho zinachezwa pamoja ili kuepuka uwezekano wa kupanga matokeo.
Pia klabu za FDL zenyewe ziliwasilisha ombi la kutaka mechi hizo za mwisho zichezwe kwa wakati mmoja.
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) wakati wowote kuanzia kesho (Januari 27 mwaka huu) itatoa ratiba ya mechi za viporo za Polisi Mara, pamoja na tarehe mpya za mechi za raundi ya 20, 21 na 22.

Sunday, January 25, 2015

MATOKEO NA MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA,VPL AZAM JUU

VPL-TFF-KLABU-LOGOMATOKEO:
Jumapili Januari 25
Azam FC 1 Simba 1
Stand United 0 Coastal Union 1
Mbeya City 2 Tanzania Prisons 2
Ruvu Shooting 2 Mtibwa Sugar 1
JKT Ruvu 1 Mgambo JKT 1
Kagera Sugar 1 Ndanda FC 2 [CCM Kirumba, Mwanza]


 MSIMAMO:

NA
TIMU
P
W
D
L
F
 A
 
GD
PTS
1
Azam FC
11
6
3
2
15
8
 
7
21
2
Yanga
10
5
3
2
12
7
 
5
18
3
JKT Ruvu
12
5
3
4
12
11
 
1
18
4
Mtibwa Sugar
10
4
5
1
13
7
 
6
17
5
Coastal Union
11
4
4
3
10
8
 
2
16
6
Polisi Moro
12
3
6
3
9
9
 
0
15
7
Ruvu Shooting
12
4
3
5
7
9
 
-2
15
8
Kagera Sugar
12
3
5
4
9
10
 
-1
14
9
Mgambo JKT
11
4
2
5
6
10
 
-4
14
10
Simba
10
2
7
1
10
8
 
2
13
11
Ndanda FC
12
4
1
7
12
17
 
-5
13
12
Mbeya City
10
3
3
4
6
8
 
-2
12
13
Stand United
12
2
5
5
7
14
 
-7
11
14
Tanzania Prisons
11
1
6
4
8
10
 
-2
9

Friday, January 23, 2015

LIGI KUU TANZANIA BARA KUWAKA MOTO DIMBANI KESHO NA JUMAPILI MBEYA CITY VS TZ PRISON

Timu za mikoa sita tayari imepata tiketi za kucheza robo fainali ya michuano ya Kombe la Taifa la Wanawake itakayoanza Januari 26 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati nyingine mbili zinajulikana leo (Januar
i 23 mwaka huu).
Mikoa ambayo timu zake tayari zina tiketi za robo fainali ya michuano hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya Proin ni Ilala, Kigoma, Mwanza, Pwani, Tanga na Temeke.
Matokeo ya mechi za leo kati ya Iringa na Ruvuma, na ile kati ya Mbeya na Katavi ndiyo yatakayoamua ni timu zipi mbili kati ya hizo zinakwenda Dar es Salaam kucheza robo fainali.
Timu zote zilizofuzu hatua ya robo fainali zinatakiwa kuripoti Dar es Salaam keshokutwa (Januari 25 mwaka huu). Fainali ya michuano hiyo itachezwa Februari Mosi mwaka huu.
TIMU YA BEACH SOCCER ZANZBAR YAWASILI DAR
Timu ya beach soccer ya Zanzibar imewasili Dar es Salaam leo mchana, tayari kwa kambi ya pamoja na Tanzania Bara kwa ajili ya kuunda kikosi cha Tanzania kitakashiriki mechi za mchujo za michuano ya Afrika.
Tanzania imepangwa kucheza mechi ya kwanza ya raundi ya kwanza dhidi ya Kenya itakayofanyika kati ya Februari 13 na 15 mwaka huu jijini Mombasa. Mechi ya marudiano itachezwa wiki moja baadaye nchini.
Zanzibar imewasili na kikosi cha wachezaji 14 na viongozi watatu ambacho kitaungana na kile cha Tanzania Bara. Timu hizo zitacheza jumla ya mechi nane kwenye ufukwe wa Escape One uliopo Mikocheni, Dar es Salaam.
Mechi hizo zitachezwa mbili asubuhi na mbili jioni kesho (Januari 24 mwaka huu), na nyingine nne kwa utaratibu huo huo keshokutwa (Januari 25 mwaka huu) kabla ya Kocha John Mwansasu kutaja kikosi cha mwisho Januari 26 mwaka huu.
VPL KUTIMUA VUMBI WIKIENDI
Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaingia raundi ya 12 wikiendi hii kwa mechi saba. Kesho (Januari 24 mwaka huu) kutakuwa na mechi kati ya Polisi Morogoro na Yanga kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Mechi za Jumapili ni kati ya Azam na Simba (Uwanja wa Taifa), Kagera Sugar na Ndanda (Uwanja wa CCM Kirumba), Stand United na Coastal Union (Uwanja wa Kambarage),, Mbeya City na Tanzania Prisons (Uwanja wa Sokoine), Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar (uwanja wa Mabatini), na JKT Ruvu na Mgambo Shooting (Uwanja wa Azam Complex).
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Monday, January 5, 2015

MENEJA WA LIVERPOOL ASEMA HENDERSON NDIYE MRITHI WA VIATU VYA GERRARD.

MENEJA wa klabu ya Liverpool, Brendan Rodgers amempigia chapuo Jordan Henderson kuziba nafasi ya Steven Gerrard wakati nahodha huyo wa timu hiyo atakapoondoka mwishoni msimu huu. 
Gerrard mwenye umri wa miaka 34 amethibitisha Ijumaa iliyopita kuwa hataongeza mkataba mwingine na ataondoka katika majira ya kiangazi huku akihusishwa na kwenda kucheza soka Marekani. 
Henderson amekuwa akionyesha kiwango kizuri chini Rodgers akicheza sambamba na Gerrard na maneja huyo anaamini kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24 ataw
eza kuziba vyema nafasi ya mkongwe huyo atapoondoka.
Akihojiwa Rodgers amesema anadhani Henderson ana haiba ya uongozi na hiyo ndiyo sababu kubwa iliyomfanya kumpatia unahodha msaidizi na pindi Gerrard atakapoondoka anadhani atakuja kuwa kiongozi mzuri kutokana na uzoefu aliopata.