Uamuzi huu umetangazwa huko Mjini
Abidjan na Katibu wa Didier Drogba Foundation, Guy Roland Tanoh, ambae
amesema itajengwa Hospitali moja katika Miji mitano ya Ivory Coast
ambayo ni Abidjan, Yamoussoukro, Man, Korhogo na San Pedro.
Kwenye Tafrija huko
London tulichangisha na kukusanya Dola Milioni 4 na zilizobaki si tatizo
ili kukamilisha Mradi huu ambao uko moyoni kabisa mwa Drogba.”
Taasisi ya Didier Drogba ilianzishwa
Mwaka 2007 na ilipanga kujenga Hospitali yenye gharama ya Pauni Milioni 3
lakini hadi leo ilikuwa haijajengwa na Tanoh hakufafanua kama Hospitali
hiyo ni moja ya hizo tano zitakazojengwa.
Wakati huo, Drogba, mwenye Miaka 35 hivi
sasa na ambae anachezea Klabu ya Turkey Galatasaray, alisema ujenzi wa
Hospitali hiyo utatokana na malipo ya Picha na Matangazo yake na Kampuni
ya Pepsi.