Thursday, July 11, 2013

DROGBA ATANGAZA KUJENGA HOSPITAL 5 ZA KINA MAMA NA WATOTO"NCHINI IVORY" COAST


Didier Drogba mshambuliaji nyota wa zamani wa Chelsea ametangaza kuwa atajenga Hospitali 5 ili kuwasaidia wakina Mama na Watoto huko Nchini Ivory Coast kwa gharama ya Dola Milioni 5.
Uamuzi huu umetangazwa huko Mjini Abidjan na Katibu wa Didier Drogba Foundation, Guy Roland Tanoh, ambae amesema itajengwa Hospitali moja katika Miji mitano ya Ivory Coast ambayo ni Abidjan, Yamoussoukro, Man, Korhogo na San Pedro.
Kwenye Tafrija huko London tulichangisha na kukusanya Dola Milioni 4 na zilizobaki si tatizo ili kukamilisha Mradi huu ambao uko moyoni kabisa mwa Drogba.”
Tanoh pia ametoboa pia kuwa Taasisi hiyo ya Drogba imeshatoa misaada kwa Watoto yatima na wale ambao wapo kwenye mazingira magumu.
Taasisi ya Didier Drogba ilianzishwa Mwaka 2007 na ilipanga kujenga Hospitali yenye gharama ya Pauni Milioni 3 lakini hadi leo ilikuwa haijajengwa na Tanoh hakufafanua kama Hospitali hiyo ni moja ya hizo tano zitakazojengwa.
Wakati huo, Drogba, mwenye Miaka 35 hivi sasa na ambae anachezea Klabu ya Turkey Galatasaray, alisema ujenzi wa Hospitali hiyo utatokana na malipo ya Picha na Matangazo yake na Kampuni ya Pepsi.