Wednesday, July 3, 2013

KUNANI HAPO?BOLOVIA MIAKA 17 IJAYO VIJANA KUITWA NEYMAR"

Katika taarifa za takwimu za ofisi ya msajili jijini La paz, Bolivia miaka 17 ijayo vijana wengi wa kiume wanaoishi katika mji huo watakuwa wakiitwa jina la mshambuliaji mpya wa fc barca Neymar. Katika taarifa iliyotolewa na gazeti moja nchini humo watoto 20 kati ya 100 wanaozaliwa katika mji mkuu huo wan chi hiyo wamepewa jina la nyota huyo mpya wa Barcelona ambaye amewateka mashabiki dunia nzima kutokana na kiwango cha hali ya juu alichokionyesha katika michuano ya Kombe la Shirikisho. Ofisa mmoja aliyetambulika kwa jina la Remigio Condori amesema wazazi wengi katika mji huo wanachagua jina la Neymar kwakuwa ndio liko katika fasheni ambapo miaka 17 ijayo vijana wengi wa kiume watakuwa wakiitwa jina hilo. Neymar ambaye amsajili na Barceona kwa ada ya euro milioni 57, alifunga mabao mawili katika ushindi wa mabao 4-0 iliyopata Brazil dhidi ya Bolivia April mwaka huu.