Katika taarifa za takwimu za
ofisi ya msajili jijini La paz, Bolivia miaka 17 ijayo vijana wengi wa
kiume wanaoishi katika mji huo watakuwa wakiitwa jina la mshambuliaji mpya wa fc barca Neymar. Katika
taarifa iliyotolewa na gazeti moja nchini humo watoto 20 kati ya 100
wanaozaliwa katika mji mkuu huo wan chi hiyo wamepewa jina la nyota huyo
mpya wa Barcelona ambaye amewateka mashabiki dunia nzima kutokana na
kiwango cha hali ya juu alichokionyesha katika michuano ya Kombe la
Shirikisho. Ofisa
mmoja aliyetambulika kwa jina la Remigio Condori amesema wazazi wengi
katika mji huo wanachagua jina la Neymar kwakuwa ndio liko katika
fasheni ambapo miaka 17 ijayo vijana wengi wa kiume watakuwa wakiitwa
jina hilo. Neymar
ambaye amsajili na Barceona kwa ada ya euro milioni 57, alifunga mabao
mawili katika ushindi wa mabao 4-0 iliyopata Brazil dhidi ya Bolivia
April mwaka huu.