KLABU ya Arsenal
imekubali kutoa kitita cha paundi milioni 42.4 kwa ajili ya kumsajili
kiungo Mesut Ozil kutoka Real Madrid ya Hispania. Ozil
mwenye umri wa miaka 24 naye amefikia makubaliano binafsi na klabu hiyo
lakini anatakiwa kufanyiwa vipimo vya afya kabla Arsenal
hawajakamilisha usajili huo ambao utavunja rekodi ya klabu hiyo. Kwasasa Ozil yuko katika majukumu ya kimataifa hivyo vipimo vya afya atafanyiwa nchini kwao Ujerumani. Arsenal
pia wako katika mazungumzo na Chelsea kwa ajili ya kumsajili kwa mkopo
mshambuliaji Demba Ba huku wakiwa tayari wamekamilisha usajili mwingine
wa mkopo kwa kipa wa Palermo Emiliano Viviano.
Monday, September 2, 2013
ILALA, KASKAZINI UNGUJA ZAANZA COPA KWA SARE
Timu
za Ilala na Kaskazini Unguja zimetoka sare ya mabao 3-3 katika moja ya
mechi za ufunguzi za michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri
chini ya miaka 15 iliyoanza leo (Septemba 2 mwaka huu) katika vituo
mbalimbali nchini.
Wafungaji
wa Ilala katika mechi hiyo iliyochezwa asubuhi Uwanja wa Tamco ulioko
Kibaha, Pwani yalifungwa na Ally Shaban (mawili) wakati lingine
lilifungwa na Haruni Said. Mabao ya Kaskazini Unguja yalifungwa na Jecha
Ally (mawili) na Shehe Ally.
Katika
kituo cha Mbeya, Njombe imeanza vizuri baada ya kuifunga Katavi mabao
2-1. Mabao ya washindi yalifungwa na Rackson Mligo dakika ya 13 wakati
lingine lilifungwa na Kelvin Gama dakika kumi kabla ya filimbi ya
mwisho.
Bao la Katavi katika mechi hiyo iliyochezwa uwanja wa Sekondari ya Iyunga lilifungwa dakika ya 15 kupitia Joseph Edward.
Wenyeji
Mbeya wameitandika Ruvuma mabao 3-0 katika mechi iliyochezwa Uwanja wa
Iyunga. Mabao ya washindi yalifungwa na Joel Mwasambungu dakika 9 wakati
mengine yalifungwa na Jackson Mwaibambe dakika ya 18 na 55.
Kesho
(Septemba 3 mwaka huu) katika kituo hicho kutakuwa na mechi kati ya
Rukwa na Katavi itakayochezwa saa 4 asubuhi wakati Iringa na Ruvuma
zitaumana kuanzia saa 2 asubuhi.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
HENRY JOSEPH AITWA TAIFA STARS
Kocha
Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen amemjumuisha mchezaji Henry Joseph wa
Simba kwenye kikosi chake kinachojiandaa kwa mechi ya mchujo ya Kombe la
Dunia dhidi ya Gambia itakayochezwa Septemba 7 mwaka huu jijini Banjul.
Tayari
Joseph amesharipoti kwenye kambi ya timu hiyo iliyoko hoteli ya
Accomondia jijini Dar es Salaam. Taifa Stars ambayo iko chini ya
udhamini wa Kilimanjaro Premium Lager imeingia kambini tangu Agosti 29
mwaka huu, na leo jioni itafanya mazoezi yake kwenye Uwanja wa
Kumbukumbu ya Karume.
Programu
ya timu hiyo inaonesha kuwa kesho (Septemba 3 mwaka huu) itafanya
mazoezi yake asubuhi na jioni kwenye uwanja huo huo wa Kumbukumbu ya
Karume.
Wakati huo huo, kesho (Septemba 3 mwaka huu) saa 6 kamili mchana Kocha Kim Poulsen atakuwa na Mkutano na Waandishi wa Habari.
LIUNDA KUTATHMINI WAAMUZI CL
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limemteua Leslie Liunda wa Tanzania kuwa
mtathmini wa waamuzi kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya
Coton Sport ya Cameroon na Esperance ya Tunisia.
Mechi
hiyo ya kundi B itachezwa Septemba 21 mwaka huu kwenye Uwanja wa
Omnisport Roumdeadjia mjini Garoua, Cameroon. Kamishna atakuwa Bema
Doumbia wa Ivory Coast.
Waamuzi
wanatoka Madagascar wakiongozwa na Hamada Nampiandraza. Wasaidizi wake
ni Jean Eric Pierre Andrivoavonjy, Ferdinand Velomanana Linoro na Bruno
Marie Andrimiharisia.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Subscribe to:
Posts (Atom)