KLABU ya Arsenal
imekubali kutoa kitita cha paundi milioni 42.4 kwa ajili ya kumsajili
kiungo Mesut Ozil kutoka Real Madrid ya Hispania. Ozil
mwenye umri wa miaka 24 naye amefikia makubaliano binafsi na klabu hiyo
lakini anatakiwa kufanyiwa vipimo vya afya kabla Arsenal
hawajakamilisha usajili huo ambao utavunja rekodi ya klabu hiyo. Kwasasa Ozil yuko katika majukumu ya kimataifa hivyo vipimo vya afya atafanyiwa nchini kwao Ujerumani. Arsenal
pia wako katika mazungumzo na Chelsea kwa ajili ya kumsajili kwa mkopo
mshambuliaji Demba Ba huku wakiwa tayari wamekamilisha usajili mwingine
wa mkopo kwa kipa wa Palermo Emiliano Viviano.