Monday, March 31, 2014

WANACHAMA TFF KUANDALIWA KATIBA MFANO YA MAREKBISHO.

TFF_LOGO12Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF imekutana Machi 30 mwaka huu kujadili utekelezaji wa maagizo ya TFF kwa wanachama wake kurekebisha Katiba zao ili ziendane na Katiba ya TFF pamoja na ile ya FIFA kabla ya Machi 30 mwaka huu.
Vyama vya mikoa Lindi na Dar es Salaam na Chama cha Mpira wa Miguu cha Wanawake (TWFA) viliomba kuongezewa muda wakati vingine vimeomba Katiba mama kama angalizo lao la mabadiliko hayo.  Klabu ya Simba Sports ndiye mwanachama pekee aliyewasilisha mabadiliko ya Katiba.  TFF inawapongeza viongozi na wanachama wa klabu hiyo kwa kufanya mkutano wao kwa utulivu.
Kamati itatangaza nyongeza ya muda wa kufanya mabadiliko hayo baada ya kuviandalia vyama vya mikoa na vyama shiriki katiba mfano kwa ajili ya kurahisisha shughuli hiyo.
Baada ya kupitia uamuzi wa wanachama  wa Simba S.C. Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji imeamua ifuatavyo:
(i)           Kwa kuwa pendekezo la wanachama wa Simba kubadili kipengele na 26 kuhusu sifa za mgombea kinapingana na kipengele na 29 (4)  cha Katiba ya TFF, hivyo basi Kamati imeagiza kipengele cha Katiba ya Simba kibaki vilevile bila kubadilishwa.
(ii)         Vipengele vingine vyote vimepitishwa na vitapelekwa kwa Msajili wa Klabu na  Vyama vya Michezo kwa ajili ya kusajiliwa.
(iii)       Mchakato wa uchaguzi wa Klabu ya Simba uendelee kama ulivyopangwa wakizingatia uamuzi huu wa Kamati.  TFF inaitakia Klabu ya Simba uchaguzi mwema.
Pia Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji imeshauri TFF kuwasiliana na FIFA kupata mwongozo kuhusu katazo la watu wenye rekodi ya kifungo kugombea.
TFF imepokea ushauri huo na itaufanyia kazi na kama kuna mabadiliko yoyote kiutaratibu yataanzia katika Katiba ya TFF kupitia Mkutano Mkuu.
RAMBIRAMBI MSIBA WA DK HEMED MZIRAY
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha daktari wa tiba ya michezo, Dk. Hemed Mziray kilichotokea juzi jijini Dar es Salaam.
Dk. Mziray ambaye alikuwa mfanyakazi wa Hospitali ya Manispaa ya Temeke na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Tiba ya Michezo Tanzania (TASMA) amesafirishwa kwenda kwao mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya mazishi.
Msiba huo ni mkubwa katika fani ya mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti Dk. Mziray ameshirikiana na TFF na wadau wengine wa mpira wa miguu katika masuala ya tiba na uongozi.
Alikuwa kiungo kati ya Uwanja wa Taifa ambapo mechi za kimataifa, za ligi na za kirafiki zimekuwa zikichezwa na Hospitali ya Temeke kwa wagonjwa wanaohitaji huduma zaidi, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Dk. Mziray, TASMA na wafanyakazi wa Hospitali ya Temeke na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito. Pia TFF inatoa ubani wa sh. 200,000 kwa familia ya marehemu kama rambirambi zake.
Bwana alitoa, Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe. Amina
MECHI YA AZAM, SIMBA YAINGIZA MIL 26/-
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Azam na Simba iliyochezwa jana (Machi 30 mwaka huu) Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam imeingiza sh. 26,455,000.
Watazamaji 4,741 walikata tiketi kushuhudia pambano hilo ambapo Azam iliibuka na ushindi wa mabao 2-1. Viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.
Mgawanyo kwa mapato ulikuwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 4,035,508.47, gharama za kuchapa tiketi sh. 3,908,686 wakati kila klabu ilipata sh. 5,460,687.63.
Uwanja sh. 2,776,620.83, gharama za mechi sh. 1,665,972.50, Bodi ya Ligi sh. 1,665,972.50, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 832,986.25 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 647,878.19.

Sunday, March 30, 2014

VPL:YANGA SC YAPINGWA 2-1 MKWAKWANI AZAM FC AILAMBA SIMBA 2-1

Jumamosi Machi 29
Ashanti United 2 JKT Oljoro 1
Jumapili Machi 30
Azam FC 2 Simba 1
Mgambo JKT 2 Yanga 1
Mbeya City 1 Tanzania Prisons 0
Kagera Sugar 0 v Ruvu Shooting 0
Mtibwa Sugar 3 v Coastal Union 1
JKT Ruvu 3 v Rhino Rangers 1
MABINGWA Watetezi Yanga Leo huko katika dimba la Mkwakwani Tanga walifungwa Bao 2-1 na Mgambo JKT iliyokuwa ikicheza Mtu 10 baada ya Mchezaji wao Mohamed Neto kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu katika Dakika ya 30 kwa kile kilichodaiwa kukutwa na Hirizi na kipigo hicho inaelekea kinapeleka Ubingwa kwa Azam FC ambao Leo wameichapa Simba Bao 2-1.
Huko Mkwakwani, Mgambo JKT walipata Bao lao la Kwanza Dakika ya Kwanza tu Mfungaji akiwa Fully Maganga na Yanga kusawazisha katika Dakika ya 50 kwa Penati ya Nadir Haroub "Cannavaro" lakini Penati nyingine iliyopigwa na Malima Busungu katika Dakika ya 69 iliwapa ushindi Mgambo JKT.
Jijini Dar es Salaam, Azam FC waliichapa Simba Bao 2-1 kwa Bao za Hamisi Mcha, Dakika ya 16, na John Bocco, Dakika ya 56 wakati Bao la Simba lilifungwa na Joseph Owino katika Dakika ya 45.
Matokeo haya yanaifanya Azam FC izidi kupaa kileleni wakiwa na Pointi 53 kwa Mechi 23 na kubakiza Mechi 3 huku Yanga wakiwa Nafasi ya Pili wakiwa na Pointi 46 kwa Mechi 22 na kubakisha Mechi 4.
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
PTS
1
Azam FC
23
15
8
0
31
53
2
Yanga SC
22
13
7
2
26
46
3
Mbeya City
23
12
9
2
13
45
4
Simba SC
23
9
9
5
15
36
5
Kagera Sugar
22
8
9
5
3
33
6
Mtibwa Sugar
22
7
8
7
1
29
7
Coastal Union
23
6
11
6
0
29
8
Ruvu Shooting
21
7
8
6
-4
29
9
JKT Ruvu
23
9
1
13
-13
28
10
Prison fc
22
3
10
9
-10
22
11
Mgambo JKT
22
5
6
11
-18
22
12
Ashanti united
22
5
6
11
-17
19
13
JKT Oljoro
23
2
9
12
-18
15
14
Rhino Rangers
23
2
7
14
-19
13
 
VPL-LIGI KUU VODACOM
RATIBA:
Jumamosi Machi 29
VPL_2013-2014-FPAshanti United v JKT Oljoro
Jumapili Machi 30
Mbeya City v Tanzania Prisons
Kagera Sugar v Ruvu Shooting
Mtibwa Sugar v Coastal Union
JKT Ruvu v Rhino Rangers
Azam FC v Simba
Mgambo JKT v Yanga