Sunday, March 16, 2014

SUAREZ AFUNGUKA KUWA INIESTA ALISTAHILI TUZO YA BALLON D"OR MWAKA 2010

Mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez anaamini kuwa Andres Iniesta alistahili kushinda tuzo ya Ballon d’Or mwaka 2010 zaidi kuliko mshindi wa tuzo hiyo Lionel Messi. Messi ambaye alishinda tuzo hiyo kwa miaka minne mfululizo, alinyakuwa tuzo hiyo mwaka 2010 mbele ya wachezaji wenzake wa Barcelona Iniesta na Xavi Hernandez pamoja na wenzake hao kunyakuwa taji la Kombe la Dunia wakiwa na timu ya taifa ya Hispania pamoja na taji La Liga wakiwa na klabu yao. Lakini Suarez ambaye ni Mhispania pekee kunyakuwa tuzo hiyo anadhani Xavi na Iniesta ambaye alifunga bao la ushindi katika mchezo wa fainali ya Kombe la Dunia alitakiwa kuwa mbele ya Messi aliyepewa tuzo hiyo. Suarez amesema katika miaka ya karibuni Hispania imeuwa ikifanya mambo mengi muhimu na mchezaji yoyote wan chi hiyo anastahili kushinda Ballon d’Or. Nguli huyo ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 78 aliedelea kudai kuwa La Liga pia ina wachezaji wawili wa kiwango cha juu kabisa Messi na Cristiano Ronaldo lakini anafikiri mwaka ambao Hispania walitawadhwa mabingwa wa dunia Iniesta au Xavi walistahili tuzo ya Ballon d’Or.