Wednesday, April 23, 2014

MTIBWA IPO MBIONI KUTOLEA MACHO WANANDINGA WAPYA

Timu ya soka ya Mtibwa Sugar Mabingwa wa zamani wa Tanzania kwa mwaka 1999 na 2000wamekiri kukumbana na changamoto kubwa msimu wa 2013/2014 wa ligi kuu Tanzania bara uliomalizika aprili 19 mwaka huu .
 Afisha habari wa klabu hiyo, Tobias Kifaru Lugalambwike ameueleza mtandao huu kuwa kitu kikubwa walichojifunza ni maandalizi makubwa ya baaadhi ya timu zinazoshiriki ligi kuu toafuti na wao.
“Sisi ni wakongwe katika ligi hii, lakini tumeshindwa kuonesha cheche kutokana na kuwepo kwa timu zenye kiwango kizuri. Mbeya City fc wametikisa kweli, sio kwetu tu hata Simba na Yanga wamekumbana na upinzani na ndio maana wamekosa ubingwa ”.
“Kikubwa tumebaini changamoto zetu ikiwemo kukosa wachezaji muhimu kikosini. Tunataka kufanya usajili mzuri ili tuanze maandalizi ya mapema”.