Monday, April 21, 2014

WANACHAMA WA CLUB YA COASTAL UNION WATOA NENO KUHUSU UONGOZI WAO.


Coastal union  ambayo imemaliza Ligi Kuu Bara ikishika nafasi ya tisa na alama 29 ambapo ilikuwa sio matarajio ya wanachama wa club hiyo nao wametoa neno.
Wanachama ambao wa club hiyo kutoka jiji la Tanga walitoa ujumbe kwa uongozi wao wakionyesha kupinga mambo kadhaa yanayoonekana kutokwenda sawa.
Lakini kilichoonyesha kweli mambo hayo hayako vizuri ni wachezaji kwenda kuwaunga mkono wanachama hao mara baada ya mechi hiyo kwisha.
Uongozi wa Coastal Union, umekuwa ukishutumiwa kukataa kutoa kadi mpya za wachama, huku Kassim El Siagi ambaye ni katibu mkuu akielezwa kuwa chanzo.
Siagi amekuwa akisisitiza kwamba lazima kabla ya kuwakubali wanachama wapya, basi wawahakiki kwanza kwa kuwajadili.
Lakini katiba ya Coastal Union haina kipengele hicho.