Mchezaji Mahiri Gareth Bale ameweka wazi na kusema kuwa Mchezaji
mwenzake wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo, ni Mtu mwema sana tofauti na
baadhi ya Watu wanavyomchukulia.
Bale alijiunga Real Madrid akitokea
Tottenham Mwaka Jana kwa Dau la Euro Milioni 100 likipiku Dau la Ronaldo
aliponunuliwa toka Man United la Euro Milioni 94.
Bale pia amekiri Luka Modric, ambae walikuwa nae Tottenham na kuhamia
Real Mwaka mmoja kabla, amekuwa mkarimu sana kwake.
Bale ameeleza: “Tulikuwa na Luka Miaka
mitano Spurs na tulikuwa na uhusiano mzuri sana na hili limenisaidia
nilip

Bale pia amesema kuwepo kwa Watu maarufu
kama kina Zinedine Zidane, ambae yupo chini ya Meneja wa Real Madrid,
Carlo Ancelotti, kumemwinua sana.
Mbali ya kuisaidia Real Madrid kutwaa
Copa del Rey Msimu huu baada ya kufunga Bao la Pili, la ushindi na la
ajabu dhidi ya Barcelona Mwezi uliopita, Bale pia ana nafasi kubwa hapo
Mei 24 kutwaa Ubingwa wa Ulaya wakati Real Madrid itakapokutana na
Atletico Madrid huko Lisbon, Ure
no kwenye Fainali ya UEFA CHAMPIOZ LIGI.