Thursday, May 1, 2014

TFF WASHAURI KUTOKATA TAMAA NA STARS YA MABORESHO.

SHIRIKISHO la soka Tanzania limeshauriwa kutokata tamaa na mpango wake wa maboresho ya Taifa Stars kupitia mkakati wake wa kusaka vipaji mikoani ulioanzishwa hivi karibuni.

Taifa stars ya maboresho iliweka kambi mjini Tukuyu mkoani Mbeya na kwa mara ya kwanza ilionekana aprili 26 mwaka huu uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Burundi kuadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Mechi hii iliyowavutia wadau wengi wa soka kwa lengo la kuona vipaji vipya kutoka mikoani, Stars ilifungwa bao(3-0).

Taifa Stars ilikuwa imesheheni vipaji vipya vilivyopatikana katika mkakati wa maboresho ya Taifa stars ambapo jopo la makocha waliteuliwa na TFF na kuzunguka nchi nzima kusaka vijana wa kuingizwa katika timu.

Wakati mkakati huu ukitangazwa, wadau waliuchukuliwa kwa mitazamo miwili tofauti ambapo na kundi moja liliunga mkono na lingine likapinga kwa madai kuwa hautakuwa na tija kwa wakati huu ambao timu inajiandaa kufuza AFCON mwakani nchini Morocco.