Mechi hiyo itapigwa jijini Johannesburg na baada ya hapo Simba itaanza safari ya kurejea jijini Dar
es Salaam kwa ajili ya mechi dhidi ya watani wake Yanga, Oktoba 18.
Wekundu hao tayari Simba wamecheza
mechi mbili za kirafiki, dhidi ya Orlando Pirates ambayo ilitoka sare ya ya
bila kufungana kabla ya kupata kipigo cha mabao 4-2 kutoka kwa Wits.
Dewji ambaye yuko
Johannesburg, Afrika Kusini ambako kikosi cha Simba kimeweka kambi, amesema
bado kuna mambo mengi yanapaswa kubadilishwa.