TIMU ya AS FAR Rabat ya Morocco itakayoikabili Azam kwenye mechi ya Kombe la Shirikisho imetua jana (Aprili 17 mwaka huu) saa 7.30 mchana kwa ndege ya Qatar Airways.
Wapinzani hao wa Azam FC katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, AS FAR Rabat ya Morocco baada ya kuwasili jana Dar es Salaam wameanza na vituko kedekede.
kwanza wamijawa na wasiwasi tangu wanatua katika dimba la Uwanja wa Ndege na kutoa imani kwa wapinzani wao, wakikataa mapokezi na mwishowe kukataa hoteli waliyokodiwa na wenyeji wao, Sapphire Court.
Pamoja na kuambiwa hoteli hiyo imepitishwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) na timu zote zilizocheza na Azam katika mashindano hayo, zilifikia hapo, Al Nasir ya Sudan Kusini na Barack Young Controllers II ya Liberia, lakini wakagoma.
Wenyeji wakawaambia kama hawataki hoteli hiyo watajilipia popote watakapokwenda na Waarabu hao nao wakaonyesha jeuri ya fedha kwa kujipangia New Africa Hotel. Kaazi kweli kweli.
ukitafakari kwa undani zaidi ni moja ya dalili mbaya kwa Waarabu hao kugomea hoteli na visa vyote walivyofanya, hata hivyo ni hatari kwa Azam katika wakielekea Morocco kwa ajili ya mchezo wa marudiano.
Azam watakwatuana na timu hiyo ya far rabat {Waarabu hao} Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Tatu, kabla ya kurudiana wiki mbili baadaye Morocco na mshindi wa jumla ataingia kwenye droo ya kucheza na timu zilizotolewa katika Ligi ya Mabingwa kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho.
Azam FC ilifanikiwa kuingia Raundi ya Tatu ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika, baada ya kuichalaza magoli 2-1 Barack Young Contollers II ya Liberia.Ilianza kwa kushinda 2-1 mjini Monrovia kabla ya kulazimishwa sare ya bila kufungana Dar es Salaam.
Pamoja na kuambiwa hoteli hiyo imepitishwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) na timu zote zilizocheza na Azam katika mashindano hayo, zilifikia hapo, Al Nasir ya Sudan Kusini na Barack Young Controllers II ya Liberia, lakini wakagoma.
Wenyeji wakawaambia kama hawataki hoteli hiyo watajilipia popote watakapokwenda na Waarabu hao nao wakaonyesha jeuri ya fedha kwa kujipangia New Africa Hotel. Kaazi kweli kweli.
ukitafakari kwa undani zaidi ni moja ya dalili mbaya kwa Waarabu hao kugomea hoteli na visa vyote walivyofanya, hata hivyo ni hatari kwa Azam katika wakielekea Morocco kwa ajili ya mchezo wa marudiano.
Azam watakwatuana na timu hiyo ya far rabat {Waarabu hao} Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Tatu, kabla ya kurudiana wiki mbili baadaye Morocco na mshindi wa jumla ataingia kwenye droo ya kucheza na timu zilizotolewa katika Ligi ya Mabingwa kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho.
Azam FC ilifanikiwa kuingia Raundi ya Tatu ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika, baada ya kuichalaza magoli 2-1 Barack Young Contollers II ya Liberia.Ilianza kwa kushinda 2-1 mjini Monrovia kabla ya kulazimishwa sare ya bila kufungana Dar es Salaam.