Friday, April 26, 2013

REAL MADRID KUUMANA USO KWA USO NA MAN U JUNI 2
Mabingwa wa kandanda katika jiji la londond Manchester United na Real Madrid,zinataraji kukutana katika dimba la Uwanja Old Trafford Juni 2 kucheza Mechi maalum itakayoshirikisha Manguli wa Klabu hizo ili kusaidia Mfuko wa Hisani wa Klabu ya Manchester United uitwao RED HEART UNITED.
Mechi hiyo inafuatia ile iliyochezwa Tarehe 3 Juni 2012 huko Santiago Bernabeu kati ya Timu hizi iliyochezwa na Mastaa wa zamani wa Timu hizi ili kutunisha Mfuko wa Hisani wa Real Madrid.
Kwenye Mechi itakayochezwa Juni 2 Uwanjani Old Trafford, kutakuwa na utangulizi wa Shoo Laivu ya Muziki itakayoshirikisha JLS na Amelia Lily.
Kikosi cha Man United kitakuwa chini ya Meneja Bryan Robson ambae aliwahi kuwa Nahodha wa Man United na watawania kulipa kisasi cha kufungwa 3-2 huko Madrid Mwaka jana na safari hii kimeongezwa nguvu kwa kuwepo Mabeki imara toka Norway Ronny Johnsen na Henning Berg ambao walitamba sana Old Trafford enzi zao.
Pia Wachezaji wengine wataongezeka
Man United: Edwin van der Sar, Raimond van der Gouw; Clayton Blackmore, Denis Irwin, Jaap Stam, Lee Martin, Ronny Johnsen, Henning Berg; Jesper Blomqvist, Lee Sharpe, Quinton Fortune; Andy Cole, Dion Dublin, Teddy Sheringham, Dwight Yorke.
Real Madrid: Pedro Contreras; Fernando Hierro, Ivan Helguera, Manolo Sanchis, Christian Karembeu; Claude Makelele, Zinedine Zidane, Steve McManaman, Fernando Redondo, Luis Figo, Guti, Jose Amavisca; Ruud van Nistelrooy, Emilio Butragueno, Alfonso Perez.
USO KWQA USO  3 JUNI 2012:
REAL MADRID 3 MAN UNITED 2
Santiago Bernabeu Stadium
Watazamaji: 65,000
MAGOLI:
Real Madrid:
-Morientes
-Figo
-Redondo
Manchester United
-Lee Sharpe
-Teddy Sheringham
VIKOSI:
Real Madrid: Buyo, Chendo, Roberto Carlos, Hierro, Sanchis, Zidane, Redondo, Butragueño, Morientes, Martin Vazquez, Figo
Man United: Van der Sar, Lee Martin, Irwin, Fortune, Johnsen, Dublin, Cole, Sheringham, Lee Sharpe, Blomqvist, Yorke
MBOMA AWANIA UKOCHA TUIMU YA TAIFA CAMAROON
Ancien du PSG Aristide Arthode Deuhla-Patrick Mboma.JPGCHEZAJI wa zamani wa kimataifa wa Cameroon, Patrick Mboma ameonyesha nia yake ya kuifundisha timu ya taifa ya nchi hiyo na anakusudia kutuma maombi yake Shirikisho la Soka la Cameroon-Fecafoot siku moja baada ya Waziri wa Michezo Adoum Garoua kulitaka shirikisho hilo kufanya mchakato wa kupata kocha mpya. Mshambuliaji huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 42 alikuwemo katika kikosi cha nchi hiyo ambacho kilinyakuwa Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2000 na 2002 na pia kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika. Hata hivyo Mboma hajawahi kufundisha timu yoyote na wadau wa soka nchini humo wamedai kuwa mshambuliaji huyo wa zamani wa Paris Saint Germain na Parma hana uzoefu wa kutosha wa kumuwezesha kupewa nafasi ya kuinoa timu hiyo. Lakini pamoja na wadau kuponda uwezo wake Mboma amesema haimkatishi tamaa na atatuma maombi yake kuiwinda nafasi hiyo.

Kuhusu yeye
Full nameHenri Patrick M'Boma Dem
Date of birthNovember 15, 1970 (age 42)
Place of birthDoualaCameroon
Height1.85 m (6 ft 1 in)
Playing positionStriker
Timu alizocheza
YearsTeamApps(Gls)
1990–1992Paris Saint-Germain0(0)
1992–1994Châteauroux48(22)
1994–1995Paris Saint-Germain8(1)
1995–1996Metz17(4)
1996–1997Paris Saint-Germain8(1)
1997–1998Gamba Osaka34(29)
1998–2000Cagliari40(15)
2000–2001Parma24(5)
2002→ Sunderland (mkopo)9(1)
2002–2003Al-Ittihad28(12)
2003–2004Tokyo Verdy 196935(17)
2004–2005Vissel Kobe10(2)
Total261(109)
Timu ya taifa"
1995–2004Cameroon57(33)
TUZO-AWARDS
3.African Nations Cup top scorer: 2002
Cameroon national team
YearAppsGoals
199510
199611
1997106
199881
199943
200099
200194
2002105
200310
200444
Total5733

[edit]

RUVU SHOOTING, SIMBA SASA KUCHEZA MEI 5
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Ruvu Shooting na Simba iliyokuwa ichezwe leo (Aprili 25 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam sasa itafanyika Mei 5 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.

Mabadiliko hayo yametokana na Serikali kuutumia uwanja kwa ajili ya maandalizi ya sherehe za Muungano ambazo kitaifa zitafanyika kesho (Aprili 26 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawaomba radhi washabiki kwa usumbufu uliojitokeza kutokana na mabadiliko hayo na ghafla. Ratiba ya mechi nyingine za VPL zinabaki kama zilivyo.

Ligi hiyo inaendelea kesho (Aprili 26 mwaka huu) kwa mechi kati ya Coastal Union na Azam itakayochezwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wakati Jumapili (Aprili 28 mwaka huu) itakuwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni Simba dhidi ya Polisi Morogoro.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

OLIVER USO KWA USO NA FA
MSHAMBULIAJI wa Arsenal, Oliver Giroud amekishambulia Chama cha Soka nchini Uingereza-FA baada ya uamuzi wake wa kutupilia rufani yake ya kupinga kadi nyekundu aliyopewa. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa alitolewa nje na mwamuzi Andre Marriner kwa kumchezea vibaya Stanislav Manolev wakati wa mchezo baina ya Arsenal na Fulham Jumamosi iliyopita hivyo kupelekea kufungiwa mechi tatu kwasababu ya kupewa kadi nyekundu ya moja kwa moja. Giroud mwenye umri wa miaka 26 amekuwa akijitetea kwamba aliteleza bahati mbaya kwenye tukio hilo na baada ya rufani yake kutupiliwa mbali amewakosoa FA kwa hatua waliyochukua. Giroud amesema ameshangazwa na hatua iliyochukuliwa na FA dhidi yake, sio kwamba imemuumiza ila anadhabu sheria za Uingereza zimekuwa kali sana ukilingasha na makosa yanayofanywa.

Thursday, April 25, 2013

TIMU ZA HISPAIN HOI BUNDASLIGA NOMA KWELI KWELI"TAZAMA MAMBO YALIVYOKUWA"

Katika mechi ya usiku  huu mchezaji aliye katika kiwango bora kabisa Robert Lewandowski  yameipa Borussia Dortmund ushindi wa 4-1 dhidi ya Real Madrid katika Nusu Fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya nchini Ujerumani.
Mabao ya mshambuliaji huyo wa Poland yameipa  Dortmund kujiweka katika nafasi nzuri ya kutingaa fainali ya klabu za bundasliga pekee  itakayopigwa Uwanja wa Wembley mwezi ujao, kufuatia jana Bayern Munich kuichapa 4-0 Barcelona nchini Ujerumani pia.
Lewandowski alifunga bao la kwanza dakika ya nane, kabla ya Cristiano Ronaldo kuisawazishia Real dakika ya 43.
Lakini lewandowski akaonyesha makali yake katika kipindi cha pili na kufunga mabao matatu zaidi dakika za 50, 55 na 67 kwa penalti.
Kocha wa Real, Mreno Jose Mourinho ambaye hakutegemea kipigo hicho kitakatifu, sasa real madrid inatakiwa  kutengeneza mipango ya kushinda 3-0 katika mchezo wa marudiano wiki ijayo, ili kuwapiku Dortmund.




UCL-NUSU FAINALI
RATIBA:
MARUDIANO
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
Jumanne Aprili 30
Real Madrid v Borussia Dortmund [1-4]
Jumatano Mei 1
Barcelona v Bayern Munich [0-4]
FAINALI
25 Mei 2013

UWANJA wa WEMBLEY, London.

Wednesday, April 24, 2013

TAFAKARI YA LEO 
TOMATH MULLER 
Taarifa kamili
Jina kamili”
Thomas Müller
Kuzaliwa”
13 September 1989 (age 23)
Mahali”
Weilheim, West Germany
Urefu”
1.86 m (6 ft 1 in)
Nafasi anayocheza”
Timu ya sasa
Current club
Number
25
Timu za vijana*
1993–2000
TSV Pähl
2000–2008
Timu ya Ukubwa*
Years
Team
Mechi
(Goli)
2008–2009
35
(16)
2008–sasa
131
(44)
Timu ya Taifa
2004–2005
6
(4)
2007
1
(0)
2008
1
(1)
2009–2010
6
(1)
2010–
41
(13)