Thursday, May 2, 2013

BALE ATEULIWA MCHEZAJI BORA NA WANAHABARI WA MICHEZO


Baada  Juzi kufanikiwa kutwaa Tuzo mbili za PFA, Professional Footballers' Association, za Mchezaji Bora wa Mwaka pamoja na Mchezaji Bora Kijana wa Mwaka Gareth Bale tena ameteuliwa kuwa Mchezaji Bora wa Mwaka na FWA, Football Writers' Association, na

Katika Msimu huu, Bale ameifungia Tottenham Mabao 19 katika mechi zake 29 za Ligi.
WASHINDI WALIOPITA WA FWA:
-2003: Thierry Henry
-2004: Thierry Henry
-2005: Frank Lampard
-2006: Thierry Henry
-2007: Cristiano Ronaldo
-2008: Cristiano Ronaldo
-2009: Steven Gerrard
-2010: Wayne Rooney
-2011: Scott Parker
-2012: Robin van Persie
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>


WASHINDI WALIOPITA WA TUZO MBILI PFA/
FWA KWA MPIGO:
-1980: Terry McDermott
-1983: Kenny Dalglish
-1984: Ian Rush
-1986: Gary Lineker
-1987: Clive Allen
-1988: John Barnes
-1998: Dennis Bergkamp
-1999: David Ginola
-2000: Roy Keane
-2001: Teddy Sheringham
-2003: Thierry Henry
-2004: Thierry Henry
-2007: Cristiano Ronaldo
-2008: Cristiano Ronaldo
-2010: Wayne Rooney
-2011: Robin van Persie
Kikosi cha Mwaka cha Ligi Kuu ya Uingereza ni hiki:
David de Gea (Manchester United), Pablo Zabaleta (Manchester City), 
Jan Vertonghen (Tottenham Hotspur), Rio Ferdinand (Manchester United),
 Leighton Baines (Everton), Michael Carrick (Manchester United), 
Juan Mata (Chelsea), Gareth Bale (Tottenham Hotspur),
 Luis Suarez (Liverpool), Eden Hazard (Chelsea),
 Robin van Persie (Manchester United).d), 
Juan Mata (Chelsea), Gareth Bale (Tottenham Hotspur),
 Luis Suarez (Liverpool), Eden Hazard (Chelsea), 
Robin van Persie (Manchester United).

RONALDINHO KATIKA ULIMWENGU WA SOKA

Ronaldinho
Taarifa kuhusu yeye
Full name
Ronaldo de Assis Moreira
Date of birth
21 March 1980 (age 33)
Place of birth
Height
1.83 m (6 ft 0 in)[1]
Playing position
Timu ya sasa
Current club
Number
10
Timu ya ujana
1987–1998
Timu ya wakubwa 
Years
Team
Mechi
(Goli
1998–2001
52
(21)
2001–2003
55
(17)
2003–2008
145
(70)
2008–2010
76
(20)
2011–2012
33
(15)
2012–
32
(9)
Timu ya taifa
1996
6
(2)
1999
5
(3)
2000–2008
27
(18)
1999–
96
(33)

CLUB MATAJI
Grêmio
·         South Cup (1): 1999
·         Rio Grande do Sul State Championship (1): 1999
Paris Saint-Germain
·         UEFA Intertoto Cup (1): 2001
Barcelona
·         La Liga (2): 2004–05, 2005–06
·         Supercopa de España (2): 2005, 2006
·         UEFA Champions League (1): 2005–06
AC Milan
·         Serie A (1): 2010–11
Flamengo
·         Taça Guanabara (1): 2011
·         Taça Rio (1): 2011
·         Campeonato Carioca (1): 2011


TIMU YA TAIFA Brazil

·         Copa América (1): 1999
·         FIFA World Cup (1): 2002
·         FIFA Confederations Cup (1): 2005
·         Superclásico de las Américas (1): 2011
Brazil U23
·         CONMEBOL Men Pre-Olympic Tournament (1): 1999
·         Olympic Bronze Medal (1): 2008
Brazil U17
·         FIFA U-17 World Championship (1): 1997
TUZO BINAFSI
1.Kombe la Shirikisho Golden boy : 1999
2. Kombe la Shirikisho la Golden ball: 1999
3.Rio Grande do Sul Hali michuano ya mfungaji bora: 1999
4. CONMEBOL Wanaume Kabla ya Olimpiki mashindano mfungaji bora: 2000
5. Kombe la Dunia All-Star Team: 2002
6.FIFA miaka 100
7. Balon di’o tuzo (2): 2003-04, 2005-06
8.La Liga Ibero-American Mchezaji wa Mwaka (1): 2004
9. FIFA World Mchezaji wa Mwaka (2): 2004, 2005
10.Ballon d'Or (1): 2005
11. FIFPro World Mchezaji wa Mwaka (2): 2005, 2006
12. UEFA mfungaji bora wa club (1): 2004-05
13. UEFA Club Mchezaji wa Mwaka (1): 2005-06
14.UEFA Timu ya Mwaka (3): 2003-04, 2004-05, 2005-06
15.FIFPro World XI (3): 2004-05, 2005-06, 2006-07
16 Golden mfungaji bora (1): 2009

EUROPA LIGI-NUSU FAINALI: JE LEO CHELSEA KUTINGA FAINALI

[Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 5 Usiku, Bongo Taimu]

MARUDIANO
Alhamisi Mei 2
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
Benfica v Fenerbahce [0-1]
Chelsea v FC Basel [1-2]
FAINALI
AMSTERDAM ARENA
MEI 15
Benfica/Fenerbahce v Chelsea/FC Basel 
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
FAINALI WATOTO WA BABA MMOJA
RATIBA/MATOKEO:
MARUDIANO
Jumanne Aprili 30
[Kwenye Mabano Jumla Magoli Mechi 2]
Real Madrid 2 Borussia Dortmund 0 [3-4]
Jumatano Mei 1
Barcelona 0 Bayern Munich 3 [0-7]
MAGOLI:
Barcelona 0
Bayern Munich 3
-Arjen Robben Dakika ya 32
-Pique 72 [Kajifunga Mwenyewe]
-Thomas Mueller 76
FAINALI
25 Mei 2013
UWANJA wa WEMBLEY, London.
Borrussia Dortmund v Bayern Munich

MAAGIZO YA FIFA KUHUSU UCHAGUZI WA TFF


Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limelitaka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuanza upya mchakato wa uchaguzi baada ya kubaini kasoro iliyotokana na ukosefu wa kutokuwepo vyombo vya kushughulikia ukiukwaji wa maadili. FIFA ambayo ilituma ujumbe wake katikati ya mwezi uliopita kufanya utafiti kuhusu mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa TFF ambao ulisimamishwa baada ya baadhi ya wagombea kulalamika, imetaka uchaguzi ufanyike kabla ya tarehe 30 Oktoba 2013, lakini ukitanguliwa na mabadiliko ya katiba ambayo yatahusisha uundwaji wa vyombo vya kushughulikia ukiukwaji wa maadili. Rais wa TFF, Leodegar Tenga aliwaambia waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa shirikisho hilo kuwa suala la Tanzania lilijadiliwa kwenye kikao cha Kamati ya Dharura ya FIFA kilichofanyika tarehe 28 Aprili 2013 na maamuzi yake kutumwa juzi kwa barua iliyosainiwa na KatibuMkuuwa FIFA, Jerome Valcke. Baada ya kupokea barua hiyo, Rais wa TFF alifunga safari kwenda Dodoma jana kukutana na Mheshimiwa Waziri na Naibu wake pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT). “Matarajio yetu sote yalikuwa kupokea majina ya waliopitishwa ili tufanye uchaguzi. Kinyume chake tumepokea maagizo hayo. Hata hivyo tumeona kuwa hili ni jambo la kheri kwa vile siyo tu haki itatendeka bali pia itaonekana imetendeka.” alisema Tenga, ambaye alishatangaza kuwa hatagombea tena urais baada ya kuliongoza Shirikisho kwa vipindi viwili vya miaka minne kila kimoja. “Lengo letu ni kuhakikisha maagizo hayo yanatekelezwa na uchaguzi kufanyika mapema iwezekanvyo kabla ya tarehe iliyotolewa. Yale mambo nayoweza kufanyika kwa pamoja yatafanyika ili tuharakishe utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na FIFA." Uchaguzi wa TFF ulipangwa kufanyik tarehe 23 na 24 Februari 2013 na ulikuwa ukielekea ukingoni, lakini baadhi ya wagombea walienguliwa katika hatua ya mwisho na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF na ndipo walipo andika barua FIFA kuomba iingilie kati. Rais Tenga alisema kuwa ujumbe wa FIFA ulikutana na pande zote zilizoathiriwa na mchakato wa uchaguzi na kwamba baada ya kukusanya taarifa hizo, maagizohayo ya FIFA sasa yatakuwa ni suluhisho la matatizo ya muda mrefu katika uendeshaji wa mpira wa miguu nchini.

Katika barua hiyo, FIFA imeiagizaTFF:

1. Kuunda vyombo sahihi (Kamati ya Maadili itakayokuwa na vyombo viwili ambavyo ni cha kutoa maamuzi ya awali na cha rufaa) ambavyo mamlaka yake yatakuwa ni kushughulikia masuala ya ukiukwaji wa maadili;

2. Kufanya mabadiliko ya katiba kwa kuzingatia uundwaji wa vyombo hivyo;

3. Kuanza upya kwa mchakato wa uchaguzi wa Kamati ya Utendaji kwa kufungua milango kwa wagombea ambao walishachukua fomu na wagombea wapya:
4. Shughuli hiyo ikamilike ifikapo tarehe 30 Oktoba 2013.
Katika kutekeleza hayo, TFF inatakiwa iitishe Mkutano Mkuu wa Dharura kwa ajili ya kufanya mabadiliko ya Katiba kwa ajili ya kuunda kamati hizo za maadili na Kanuni za Uchaguzi kabla ya kuendelea na Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Kamati Mpya ya Utendaji.
Katika maoni yake FIFA imeeleza kuwa katika mchakato, Kamati ya Uchaguzi ya TFF iliwaengua au kupitisha baadhi ya wagombea kwa kubaini kuwa walikiuka Ibara ya 9 (7) ya Kanuni za Uchaguzi na pia Ibaray a 29 (7) ya Katiba ya TFF ambavyo vinahusisha suala la kufungua kesi mahakamani, kufuja fedha za shirikisho na ukosefu wa uwajibikaji wa pamoja.
Hata hivyo, FIFA ilisema kuwa watu hao walitakiwa waadhibiwe kwanza na kamati husika (kamati za maadili) kabla ya kuenguliwa na kamati za uchaguzi za TFF.

Kutokana na ukosefu wa kamati za maadili matokeo yake, mmoja wa wagombea amekuwa akienguliwa kwenye uchaguzi kila anapombea bila ya kujua adhabu yake ni ya muda gani,” inasema barua hiyo ya FIFA.

Rais Tenga ameagiza kuitishwa kwa kikao cha dharura cha Kamati ya Utendaji ya TFF kupokea maagizo ya FIFA na kupanga ratiba ya utekelezaji wake kwa lengo la kuhakikisha kuwa mchakato huu unatekelezwa mapema iwezekanavyo.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mei 1, 2013
 MIKOA 18 YAPATA MABINGWA WA MIKOA
Mikoa 18 kati ya 27 ya kimpira tayari imeshapata mabingwa wao kwa ajili ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa itakayoanza Mei 12 mwaka huu chini ya usimamizi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Timu tatu za juu katika Ligi hiyo ya Mabingwa zitapanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao (2013/2014). Ligi ya FDL ina jumla ya timu 24 ambapo tatu katika ligi hiyo zilizoshuka daraja msimu huu ni Moro United ya Dar es Salaam, Small Kids ya Rukwa na Morani FC ya Manyara.

Mabingwa waliopatikana hadi sasa na mikoa yao kwenye mabano ni Abajalo SC (Dar es Salaam 2), Biharamulo FC (Kagera), Flamingo SC (Arusha), Friends Rangers (Dar es Salaam 3), Katavi Warriors (Katavi), Kiluvya United (Pwani), Kimondo FC (Mbeya) na Machava FC (Kilimanjaro).

Wengine ni Magic Pressure FC (Singida), Mbinga United (Ruvuma), Mji Njombe (Njombe), Polisi Jamii Bunda FC (Mara), Red Coast FC (Dar es Salaam 1), Rukwa United (Rukwa), Saigon FC (Kigoma), TECKFOLT FC ya Kilombero ambayo ni Shule ya Sekondari (Morogoro) na UDC FC ya Ukerewe (Mwanza).

Kila klabu inatakiwa kulipa ada ya ushiriki ambayo ni sh. 100,000 wakati usajili wa wachezaji wa timu hizo ni uleule uliofanyika katika Ligi ya Mkoa na unatakiwa kuwasilishwa TFF kwa ajili ya uthibitisho. TFF inapenda kusisitiza kuwa hakuna usajili mpya wa wachezaji kwa ajili ya ligi hiyo.

MTANZANIA AOMBEWA ITC ACHEZE NORWAY
Shirikisho la Mpira wa Miguu Norway (NFF) limetuma maombi ya kupatiwa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa mchezaji Mtanzania Godfrey Mlowoka ili aweze kucheza mpira nchini humo.

NFF inamuombea hati hiyo Mlowoka ili aweze kujiunga na klabu ya Ekne IL kama mchezaji wa ridhaa ambapo klabu yake ya zamani aliyokuwa akiichezea nchini imetajwa kuwa Sadani.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linafanyia kazi maombi hayo na mara taratibu zote zitakapokamilika hati hiyo ya uhamisho itatumwa nchini Norway.

AZAM YAENDELEA KUJINOA MOROCCO
Timu ya Azam ambayo iko jijini Rabat kwa ajili ya mechi ya marudiano ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho dhidi ya AS FAR Rabati ya huko inaendelea vizuri na mazoezi.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari Msaidizi wa Azam FC, Jaffer Idd maandalizi yanakwenda vizuri kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa Jumamosi (Mei 4 mwaka huu). Jaffer Idd anapatikana kwa namba +212671146092.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)