Thursday, May 23, 2013

GARCIA AMUOMBA RADHI MCHEZAJI NAMBA MOJA TIGER WOODS

MCHEZAJI machachali wa  mchezo wa gofu, Sergio Garcia ameomba radhi kwa kauli yake ambayo inaweza kuonekana kama ya kibaguzi kwenda kwa nyota wa mchezo huo anayeshika namba moja kwa ubora Tiger Woods. Garcia mwenye umri wa miaka 33 aliulizwa kama ataweza kula chakula cha jioni na Woods ili kuzungumzia tofauti zao za hivi karibuni na mchezaji huyo kutania kuwa atamuandalia kuku wa kukaanga nyota huyo. Kuku wa kukaanga ni chakula kinachohusishwa na watu weusi huko Marekani haswa wale wanaotoka kusini mwa nchi hiyo. Garcia aliomba radhi kwa kauli hiyo kama imeeleweka vibaya akidai kuwa hakumaanisha chochote kuhusu ubaguzi wa rangi kwa nyota huyo ambao ambaye asili yake ni mweusi.

MURRAY AJITOA MICHUANO YA WAZI UFARANSA:

MCHEZAJI nyota maarufu wa tenisi kutoka Uingereza Andy Murray amejitoa katika michuano ya wazi ya Ufaransa kutokana na maumivu ya mgongo yaliyopelekea kushindwa kuendelea kucheza katika michuano ya wazi ya Italia. Murray ambaye anashika namba mbili katika orodha za ubora Duniani kwa upande wa wanaume amejitoa katika michuano hiyo baada ya kushauriwa na madaktari wake na anatarajia kurejea tena uwanjani katika michuano ya Wimbledon katikati ya mwezi ujao. Nyota huyo ambaye ni bingwa wa michuano ya wazi ya Marekani amesema umekuwa ni uamuzi mgumu kufanya kwani huwa anapenda kucheza jijini Paris lakini imekuwa nje ya uwezo wake kwasababu ya ushauri wa kiafya aliopewa. Murray aliwaomba radhi waandaaji wa michuano hiyo na kuwashukuru mashabiki wake kwa kumtumia ujumbe wa kumuunga mkono na sasa kazi kubwa aliyokuwa nayo ni kuhakikisha anapona na kurejea haraka uwanjani.

Wednesday, May 22, 2013

MWAMUZI WA AFRIKA KUSINI KUICHEZESHA STARS MOROCCO.


Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua mwamuzi kutoka Afrika Kusini kuchezesha mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na wenyeji Morocco (Lions of the Atlas).

Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco kwenye Uwanja wa Grand kuanzia saa 3 kamili usiku kwa saa za Morocco. Mwamuzi atakayechezesha mechi hiyo ni Fraser Daniel Bennett.

Bennett atasaidiwa na Thusi Zakhele Siwela pia wa Afrika Kusini, wakati mwamuzi msaidizi namba mbili atakuwa ni Marwa Range kutoka Kenya. Mwamuzi wa akiba (fourth official) ni Lwandile Mfiki wa Afrika Kusini.

Kamishna wa mechi hiyo ni Robert Mangollo-M’voulou wa Gabon wakati mtathimini wa waamuzi (referee assessor) ni Charles Masembe kutoka Uganda.

Taifa Stars ambayo iko chini ya Kocha Kim Poulsen, na ikidhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari iko kambini katika hoteli ya Tansoma ikiendelea kujinoa kwa ajili ya mechi hiyo ambapo kabla itajipima na Sudan (Nile Crocodiles) Juni 2 mwaka huu jijini Addis Ababa, Ethiopia.

Ratiba ya mazoezi kwa timu hiyo ni kama ifuatavyo;

Mei 22                 Saa 10 jioni                             Uwanja wa Karume
Mei 23                 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni   Uwanja wa Karume
Mei 23                 Saa 10 jioni                             Uwanja wa Karume


Mei 25                 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni     Uwanja wa Karume
Mei 26                 Saa 3 asubuhi                            Uwanja wa Karume


MSIMAMO WA KUNDI C:


                     P W D L GF GA Pts
Ivory Coast 3 2 1 0 7 2 7
Tanzania 3 2 0 1 5 4 6
Morocco 3 0 2 1 4 6 2
Gambia 3 0 1 2 2 6 1


REKODI YA KIM POULSEN STARS
Mei 26, 2012
Tanzania 0 – 0 Malawi (Kirafiki)
Juni 2, 2012
Ivory Coast 2 – 0 Tanzania (Kufuzu Kombe la Dunia)
Juni 10, 2012
Tanzania 2 – 1 Gambia (Kufuzu Kombe la Dunia)
Juni 17, 2012
Msumbiji 1 – 1 Tanzania  (Tanzania ilitolewa
kwa penalti kufuzu Mataifa ya Afrika)
Agosti 15, 2012
Botswana 3 – 3 Tanzania (Kirafiki)
Novemba 14, 2012
Tanzania 1-0 Kenya (Kirafiki)
Desemba 22, 2012
Tanzania 1-0 Zambia (Kirafiki)
Januari 11, 2013
Tanzania 1-2 Ethiopia (Kirafiki)
Februari 6, 2013
Tanzania 1-0 Cameroon (Kirafiki)
Machi 22, 2013
Tanzania 3-1 Morocco (Kufuzu Kombe la Dunia)



MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga atakuwa na mkutano na waandishi wa habari. Mkutano huo utafanyika kesho (Mei 23 mwaka huu) saa 5 kamili asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa TFF.



Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

KAGAME CUP KUCHEZWA SUDAN JUNI 18-JULAI 21 JE YANGA ITATWAA KAGEME CUP MARA TATU MFULULIZO.

MASHINDANO ya 39 ya kusaka Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati CECAFA KAGAME CUP 2013 yatachezwa huko Sudan kuanzia Juni 18 hadi Julai 2 na Mabingwa Watetezi Yanga wamepangwa Kundi C na wataanza kwa kucheza na Express ya Uganda hapo Juni 20 Mjini Al Fasher, Mji Mkuu wa Darfur ya Kaskazini.
Jana huko Mjini Khartoum, Sudan ndio ilifanyika Droo ya Timu 13 kupangwa Makundi matatu na Droo hiyo ilisimamiwa na Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye, na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kagame Cup, Raoul Gisanura, wa kutoka Rwanda.
KUNDI A:
Merrickh El Fasher (Sudan), Simba (TZ), Al Mann (Somalia), APR (Rwanda).
KUNDI B:
Hilal Kadougli (Sudan), Ahli Shandi (Sudan), Al Nasr (S.Sudan), Tusker (Kenya), Super Falcon (Zanzibar).
KUNDI C:
Yanga (Tanzania), Express FC (Uganda), Vital O (Burundi), AS Port (Djibouti)
Mashindano haya yatachezwa kwa Wiki mbili katika Miji ya Kaskazini ya Sudan, Al Fasher na Kadugli, South Kordufan State, na Yanga, ambao ni Mabingwa Watetezi, wanawania kutwaa Ubingwa huu kwa mara ya 3 mfululizo.
 President of Rwanda
    paul kagame
Close up profile picture of Paul Kagame, seated at the 2009 World Economic ForumZanzibar wanawakilishwa na Super Falcon ambao walitwaa Ubingwa wa Zanzibar Msimu wa 2011/12 lakini hivi sasa, huko Visiwani, wameshashushwa Daraja.
Super Falcon wataanza kucheza Juni 18 na Tusker ys Kenya huko Kadugli, South Kordufan State, Sudan.
Mashindano haya yanadhaminiwa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame, na zawadi ni Dola 60,000.
RATIBA KAMILI  BAADAE




WASHINDI WALIOPITA:
MWAKA
NCHI YA KLABU
BINGWA NA
MSHINDI WA PILI
NCHI YA KLABU
MWENYEJI
1.1967
Abaluhya ya Kenya 
2.Sunderland
Tanzania
-----------------
1974
Tanzania
Simba
Abaluhya
Kenya
-------------------
Tanzania
1975
Tanzania
Young Africans
2–0
Simba
Tanzania
Zanzibar
1976
Kenya
Luo Union
2–1
Young Africans
Tanzania
Uganda
1977
Kenya
Luo Union
2–1
Horsed
Somalia
Tanzania
1978
Uganda
Kampala City
0–0 [Penati 3-2]
Simba
Tanzania
Uganda
1979
Kenya
Abaluhya
1–0
Kampala City
Uganda
Somalia
1980
Kenya
Gor Mahia
3–2
Abaluhya
Kenya
Malawi
1981
Kenya
Gor Mahia
1–0
Simba
Tanzania
Kenya
1982
Kenya
A.F.C. Leopards
1–0
Rio Tinto
Zimbabwe
Kenya
1983
Kenya
A.F.C. Leopards
2–1
ADMARC Tigers
Malawi
Zanzibar
1984
Kenya
A.F.C. Leopards
2–1
Gor Mahia
Kenya
Kenya
1985
Kenya
Gor Mahia
2–0
A.F.C. Leopards
Kenya
Sudan
1986
Sudan
Al-Merrikh
2–2 [Penati 4-2]
Young Africans
Tanzania
Tanzania
1987
Uganda
Villa
1–0
Al-Merrikh
Sudan
Uganda
1988
Kenya
Kenya Breweries
2–0
Al-Merrikh
Sudan
Sudan
1989
Kenya
Kenya Breweries
3–0
Coastal Union
Tanzania
Kenya
1991

Tanzania
Simba
3–0
Villa
Uganda
Tanzania
1992
Tanzania
Simba
1–1 [Penati 5-4]
Young Africans
Tanzania
Zanzibar
1993
Tanzania
Young Africans
2–1
Villa
Uganda
Uganda
1994
Sudan
Al-Merrikh
2–1
Express
Uganda
Sudan
1995
Tanzania
Simba
1–1 [Penati 5-3]
Express
Uganda
Tanzania
1996
Tanzania
Simba
1–0
Armée Patriotique
Rwanda
Tanzania
1997
Kenya
A.F.C. Leopards
1–0
Kenya Breweries
Kenya
Kenya
1998
Rwanda
Rayon Sports
2–1
Mlandege
Zanzibar
Zanzibar
1999
Tanzania
Young Africans
1–1 [Penati 4-1]
Villa
Uganda
Uganda
2000
Kenya
Tusker
3–1
Armée Patriotique
Rwanda
Rwanda
2001
Kenya
Tusker
0–0 [Penati 3-0]
Oserian
Kenya
Kenya
2002
Tanzania
Simba
1–0
Prince Louis
Burundi
Zanzibar
2003
Uganda
Villa
1–0
Simba
Tanzania
Uganda
2004
Rwanda
Armée Patriotique
3–1
Ulinzi Stars
Kenya
Rwanda
2005
Uganda
Villa
3–0
Armée Patriotique
Rwanda
Tanzania
2006
Uganda
Police
2–1
Moro United
Tanzania
Tanzania
2007
Rwanda
Armée Patriotique
2–1
URA
Uganda
Rwanda
2008
Kenya
Tusker
2–1
URA
Uganda
Tanzania
2009
Rwanda
ATRACO
1–0
Al-Merrikh
Sudan
Sudan
2011

Tanzania
Young Africans
1–0
Simba
Tanzania
Tanzania
2012
Tanzania
Young Africans
2–0
Azam
Tanzania
Tanzania
FAHAMU:
-Mashindano ya Mwaka 1967 hayakuwa rasmi
-Mashindano hayakufanyika kati ya Miaka ya 1968 hadi 1973, Mwaka 1990 & 2010.
-1974 Mashindano yalisimama.

Tuesday, May 21, 2013

PEREZ ATANABAISHA KUWA CLUB HIYO INAKAZI KUPATA KOCHA MPYA.

RAIS wa klabu ya Real Madrid, Florentino Perez ametanabaisha kuwa klabu hiyo ina Kazi nzito mrefu wa makocha akiwemo kocha Carlo Ancelotti wa Paris Saint-Germain-PSG ili kuziba pengo la Jose Mourinho ambaye anaondoka. Klabu hiyo iliweka wazi Jumatatu kuwa Mourinho ambaye ni raia wa Ureno ataondoka Santiago Bernabeu katika kipindi hiki cha majira ya kiangazi na kazi ya kutafuta mbadala wake tayari imeanza. Perez alithitisha kuwa tayari wameshazungumza na Ancelotti ambaye ameonyesha nia ya kuikacha PSG lakini klabu hiyo imeamua kumng’ang’ania kocha huyo Muitaliano. Mbali na kuzungumza na Ancelotti Perez pia amesema walizungumza na mkurugenzi mkuu wa PSG ili kuangalia uwezekano wa kumchukua Ancelotti lakini walikataa, hivyo wana siku chake za kufikiria suala hilo ingawa amedai kuwa wana orodha ya makocha wengi walioomba nafasi hiyo.

TOURE KOLO VS EBOUE WAKABILIWA NA KIFUNGO.

Wanandinga wa kimataifa wa Ivory Coast, Kolo Toure anayekipiga katika klabu ya Manchester City na Emmanuel Eboue wa klabu ya Galatasaray wanakabiliwa na adhabu ya kufungiwa kuitumikia timu ya taifa ya nchi hiyo kufuatia kauli walizozitoa katika vyombo vya habari kulishambulia Shirikisho la Soka la nchi hiyo. Wachezaji hao wawili wameenguliwa katika kikosi cha nchi hiyo ambacho kitapambana na Gambia na Tanzania katika mechi za kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2014. Hatua hiyo ya kuwaacha wachezaji hao ilifikiwa na kamati ya nidhamu ya shirikisho hilo kufuatia malalamiko yaliyofikishwa na kocha anayekinoa kikosi hicho Sabri Lamouchi. Ivory Coast inatarajia kuchuana Gambia Juni 8 mwaka huu kabla ya kupambana na Taifa Stars Juni 16 katika michezo ya kundi C ya kufuzu michuano ya Kombe la Dunia.

MICHO ATARAJI KUTAMBULISHWA TIMU YA TAIFA UGANA THE CRANES.

KOCHA wa zamani wa timu ya taifa ya Rwanda, Milutin Sredojevic Micho anatarajiwa kutangazwa kuwa kocha mpya timu ya taifa Uganda inayojulikana kama The Cranes. Micho ambaye ni raia wa Serbia anatarajiwa kutangazwa mbele ya waandishi wa habari katika makao makuu ya Shirikisho la Soka la Uganda-FUFA na kumaliza tetesi zilizozagaa karibu mwezi mzima baada ya kutimuliwa kwa Bobby Williamson mwezi uliopita. Micho mwenye umri wa miaka 43 alitimuliwa kuinoa Rwanda mwezi huohuo ambao Bobby naye alitimuliwa kuifundisha The Cranes na sababu za kutimuliwa kwao zinafanana kwani wote wawili timu zao zilikuwa zikifanya vibaya katika mechi za kufuzu michuano ya Kombe la Dunia. Changamoto ya kwanza atakayokutana nayo Micho ni kukirejesha kikosi hicho katika ari ya ushindani na kuhakikisha wanafanya vizuri katika mechi zao za kufuzu michuano ya Kombe la Dunia pamoja na ile ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani-CHAN.