MAKAMU wa rais wa klabu
ya Santos ya Brazil, Odilio Rodrigues amedai kwamba wamekataa ofa ya klabu
ya Barcelona ya Hispania kutaka kumsajili mshambuliaji wao nyota Neymar
kwa mara ya pili. Katika
siku za hivi karibuni Barcelona ndiyo pekee wameonyesha nia ya kumhitaji
mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Brazil na kuripoti kuwa walitaka
kuwapa Santos euro milioni 20 ili waweze kumiliki haki za mchezaji huyo
kwa asilimia 55. Wakati
mahasimu wao nao Real madrid wakiongeza mbio ya kumfukuzia mshambuliaji huyo,
Barcelona walitoa kiasi hicho ili waweze kumaliza suala hilo lakini
Rodrigues amesisitiza kuwa hawana haraka ya kumuuza Neymar kwa kiasi
kidogo kuliko wanachotaka. Rodrigues
alithibitisha kuwa ni kweli walipata ofa ya Barcelona kwa mara ya pili
lakini waliikataa kwasababu hawakufikia kiwango walichokuwa
wakikihitaji. Neymar
katika siku karibu ameweka wazi nia yake ya kubakia Santos mpaka baada
ya michuano ya Kombe la Dunia 2014, ingawa uhamisho wa kwenda barani
Ulaya katika kipindi hiki cha usajili unaonekana kama unaweza kuwepo.Thursday, May 23, 2013
CLUB YA SANTOS YAKATAA OFA YA PILI YA BARCA
MAKAMU wa rais wa klabu
ya Santos ya Brazil, Odilio Rodrigues amedai kwamba wamekataa ofa ya klabu
ya Barcelona ya Hispania kutaka kumsajili mshambuliaji wao nyota Neymar
kwa mara ya pili. Katika
siku za hivi karibuni Barcelona ndiyo pekee wameonyesha nia ya kumhitaji
mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Brazil na kuripoti kuwa walitaka
kuwapa Santos euro milioni 20 ili waweze kumiliki haki za mchezaji huyo
kwa asilimia 55. Wakati
mahasimu wao nao Real madrid wakiongeza mbio ya kumfukuzia mshambuliaji huyo,
Barcelona walitoa kiasi hicho ili waweze kumaliza suala hilo lakini
Rodrigues amesisitiza kuwa hawana haraka ya kumuuza Neymar kwa kiasi
kidogo kuliko wanachotaka. Rodrigues
alithibitisha kuwa ni kweli walipata ofa ya Barcelona kwa mara ya pili
lakini waliikataa kwasababu hawakufikia kiwango walichokuwa
wakikihitaji. Neymar
katika siku karibu ameweka wazi nia yake ya kubakia Santos mpaka baada
ya michuano ya Kombe la Dunia 2014, ingawa uhamisho wa kwenda barani
Ulaya katika kipindi hiki cha usajili unaonekana kama unaweza kuwepo.FA CHADAI KUWA CARROL AJITOA TIMU YA TAIFA KUTOKANA NA MAJERUHI.
CHAMA cha Soka nchini Uingereza {FA} kimedai kuwa mshambuliaji wa kimataifa wa nchi hiyo, Andy Carroll amejitoa katika timu ya taifa kutokana na kuwa majeruhi. Carroll mwenye umri wa miaka 24 amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya kisigino baada ya kocha wa timu ya taifa Roy Hodgson kumuita katika kikosi chake ambacho kitacheza mechi mbili za kimataifa za kirafiki kati ya Ireland Mei 29 na Brazil Juni 2 katika Uwanja wa Maracana jijini Rio de Janeiro. Mshambuliaji huyo wa Liverpool amekuwa akicheza kwa mkopo katika klabu ya West Ham United msimu uliopita huku vyombo vya habari nchini Uingereza vikiripoti kuwa klabu hiyo imekubali kumchukua moja kwa moja kwa ada ya paundi milioni 15. Carroll anaungana na nahodha wa Liverpool Steven Gerrard na kiungo wa Arsenal Jack Wilshere kukosa mechi hizo za kujipima nguvu kabla ya mechi za kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2014 dhidi ya Moldova na Ukraine Septemba mwaka huu.KOCHA WA LIVERPOOL RODGERS HANA MPANGO WA KUMUUZA SUAREZ.
BOSI wa majogoo wa jiji la londo Liverpool Brendan Rodgers amesema hana mpango wa kumuuza mshambuliaji nyota wa klabu hiyo Luis Suarez. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uruguay alikosa mechi nne za Liverpool mwishoni mwa msimu huu baada ya kufungiwa mechi 10 kwa kumng’ata beki wa Chelsea Branislav Ivanovic lakini alimaliza katika nafasi ya tatu katika orodha ya wafungaji wa Ligi Kuu nchini Uingereza akiwa na mabao 23. Liverpool haijafuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya toka mwaka 2009 lakini pamoja na vilabu vikubwa kummezea mate Suarez, kocha huyo ana imani kwamba ataweza kumbakisha mchezaji huyo kwa msimu ujao. Rodgers amesema kwasasa wanajipanga kutengeneza kikosi chao kwa ajili ya msimu ujao na Suarez ni sehemu ya kikosi hicho ingawa amekiri kwamba zipo baadhi ya klabu kubwa zinazomtaka.
GARCIA AMUOMBA RADHI MCHEZAJI NAMBA MOJA TIGER WOODS
MCHEZAJI machachali wa mchezo wa gofu, Sergio Garcia ameomba radhi kwa kauli yake ambayo inaweza kuonekana kama ya kibaguzi kwenda kwa nyota wa mchezo huo anayeshika namba moja kwa ubora Tiger Woods. Garcia mwenye umri wa miaka 33 aliulizwa kama ataweza kula chakula cha jioni na Woods ili kuzungumzia tofauti zao za hivi karibuni na mchezaji huyo kutania kuwa atamuandalia kuku wa kukaanga nyota huyo. Kuku wa kukaanga ni chakula kinachohusishwa na watu weusi huko Marekani haswa wale wanaotoka kusini mwa nchi hiyo. Garcia aliomba radhi kwa kauli hiyo kama imeeleweka vibaya akidai kuwa hakumaanisha chochote kuhusu ubaguzi wa rangi kwa nyota huyo ambao ambaye asili yake ni mweusi.
MURRAY AJITOA MICHUANO YA WAZI UFARANSA:
MCHEZAJI nyota maarufu wa tenisi kutoka Uingereza Andy Murray amejitoa katika michuano ya wazi ya Ufaransa kutokana na maumivu ya mgongo yaliyopelekea kushindwa kuendelea kucheza katika michuano ya wazi ya Italia. Murray ambaye anashika namba mbili katika orodha za ubora Duniani kwa upande wa wanaume amejitoa katika michuano hiyo baada ya kushauriwa na madaktari wake na anatarajia kurejea tena uwanjani katika michuano ya Wimbledon katikati ya mwezi ujao. Nyota huyo ambaye ni bingwa wa michuano ya wazi ya Marekani amesema umekuwa ni uamuzi mgumu kufanya kwani huwa anapenda kucheza jijini Paris lakini imekuwa nje ya uwezo wake kwasababu ya ushauri wa kiafya aliopewa. Murray aliwaomba radhi waandaaji wa michuano hiyo na kuwashukuru mashabiki wake kwa kumtumia ujumbe wa kumuunga mkono na sasa kazi kubwa aliyokuwa nayo ni kuhakikisha anapona na kurejea haraka uwanjani.
Wednesday, May 22, 2013
MWAMUZI WA AFRIKA KUSINI KUICHEZESHA STARS MOROCCO.
Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua mwamuzi kutoka Afrika Kusini kuchezesha mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na wenyeji Morocco (Lions of the Atlas).
Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco kwenye Uwanja wa Grand kuanzia saa 3 kamili usiku kwa saa za Morocco. Mwamuzi atakayechezesha mechi hiyo ni Fraser Daniel Bennett.
Bennett atasaidiwa na Thusi Zakhele Siwela pia wa Afrika Kusini, wakati mwamuzi msaidizi namba mbili atakuwa ni Marwa Range kutoka Kenya. Mwamuzi wa akiba (fourth official) ni Lwandile Mfiki wa Afrika Kusini.
Kamishna wa mechi hiyo ni Robert Mangollo-M’voulou wa Gabon wakati mtathimini wa waamuzi (referee assessor) ni Charles Masembe kutoka Uganda.
Taifa Stars ambayo iko chini ya Kocha Kim Poulsen, na ikidhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari iko kambini katika hoteli ya Tansoma ikiendelea kujinoa kwa ajili ya mechi hiyo ambapo kabla itajipima na Sudan (Nile Crocodiles) Juni 2 mwaka huu jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Ratiba ya mazoezi kwa timu hiyo ni kama ifuatavyo;
Mei 22 Saa 10 jioni Uwanja wa Karume
Mei 23 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni Uwanja wa Karume
Mei 23 Saa 10 jioni Uwanja wa Karume
Mei 25 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni Uwanja wa Karume
Mei 26 Saa 3 asubuhi Uwanja wa Karume
MSIMAMO WA KUNDI C:
P W D L GF GA Pts
Ivory Coast 3 2 1 0 7 2 7
Tanzania 3 2 0 1 5 4 6
Morocco 3 0 2 1 4 6 2
Gambia 3 0 1 2 2 6 1
REKODI YA KIM POULSEN STARS
Mei 26, 2012
Tanzania 0 – 0 Malawi (Kirafiki)
Juni 2, 2012
Ivory Coast 2 – 0 Tanzania (Kufuzu Kombe la Dunia)
Juni 10, 2012
Tanzania 2 – 1 Gambia (Kufuzu Kombe la Dunia)
Juni 17, 2012
Msumbiji 1 – 1 Tanzania (Tanzania ilitolewa
kwa penalti kufuzu Mataifa ya Afrika)
Agosti 15, 2012
Botswana 3 – 3 Tanzania (Kirafiki)
Novemba 14, 2012
Tanzania 1-0 Kenya (Kirafiki)
Desemba 22, 2012
Tanzania 1-0 Zambia (Kirafiki)
Januari 11, 2013
Tanzania 1-2 Ethiopia (Kirafiki)
Februari 6, 2013
Tanzania 1-0 Cameroon (Kirafiki)
Machi 22, 2013
Tanzania 3-1 Morocco (Kufuzu Kombe la Dunia)
MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga atakuwa na mkutano na waandishi wa habari. Mkutano huo utafanyika kesho (Mei 23 mwaka huu) saa 5 kamili asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa TFF.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
KAGAME CUP KUCHEZWA SUDAN JUNI 18-JULAI 21 JE YANGA ITATWAA KAGEME CUP MARA TATU MFULULIZO.
MASHINDANO ya 39 ya kusaka Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati CECAFA KAGAME CUP 2013 yatachezwa huko Sudan kuanzia Juni 18 hadi Julai 2 na Mabingwa Watetezi Yanga wamepangwa Kundi C na wataanza kwa kucheza na Express ya Uganda hapo Juni 20 Mjini Al Fasher, Mji Mkuu wa Darfur ya Kaskazini.
Jana huko Mjini Khartoum, Sudan ndio ilifanyika Droo ya Timu 13 kupangwa Makundi matatu na Droo hiyo ilisimamiwa na Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye, na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kagame Cup, Raoul Gisanura, wa kutoka Rwanda.
KUNDI A:
Merrickh El Fasher (Sudan), Simba (TZ), Al Mann (Somalia), APR (Rwanda).
KUNDI B:
Hilal Kadougli (Sudan), Ahli Shandi (Sudan), Al Nasr (S.Sudan), Tusker (Kenya), Super Falcon (Zanzibar).
KUNDI C:
Yanga (Tanzania), Express FC (Uganda), Vital O (Burundi), AS Port (Djibouti)
Mashindano haya yatachezwa kwa Wiki mbili katika Miji ya Kaskazini ya Sudan, Al Fasher na Kadugli, South Kordufan State, na Yanga, ambao ni Mabingwa Watetezi, wanawania kutwaa Ubingwa huu kwa mara ya 3 mfululizo.
President of Rwanda
paul kagame
President of Rwanda
paul kagame
Super Falcon wataanza kucheza Juni 18 na Tusker ys Kenya huko Kadugli, South Kordufan State, Sudan.
Mashindano haya yanadhaminiwa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame, na zawadi ni Dola 60,000.
RATIBA KAMILI BAADAE
WASHINDI WALIOPITA:
MWAKA
NCHI YA KLABU
BINGWA NA
MSHINDI WA PILI
NCHI YA KLABU
MWENYEJI
1.1967
Abaluhya ya Kenya
2.Sunderland
Tanzania
-----------------
1974
Tanzania
Simba
Abaluhya
Kenya
-------------------
Tanzania
Tanzania
1975
Tanzania
Young Africans
2–0
Simba
Tanzania
Zanzibar
1976
Kenya
Luo Union
2–1
Young Africans
Tanzania
Uganda
1977
Kenya
Luo Union
2–1
Horsed
Somalia
Tanzania
1978
Uganda
Kampala City
0–0 [Penati 3-2]
Simba
Tanzania
Uganda
1979
Kenya
Abaluhya
1–0
Kampala City
Uganda
Somalia
1980
Kenya
Gor Mahia
3–2
Abaluhya
Kenya
Malawi
1981
Kenya
Gor Mahia
1–0
Simba
Tanzania
Kenya
1982
Kenya
A.F.C. Leopards
1–0
Rio Tinto
Zimbabwe
Kenya
1983
Kenya
A.F.C. Leopards
2–1
ADMARC Tigers
Malawi
Zanzibar
1984
Kenya
A.F.C. Leopards
2–1
Gor Mahia
Kenya
Kenya
1985
Kenya
Gor Mahia
2–0
A.F.C. Leopards
Kenya
Sudan
1986
Sudan
Al-Merrikh
2–2 [Penati 4-2]
Young Africans
Tanzania
Tanzania
1987
Uganda
Villa
1–0
Al-Merrikh
Sudan
Uganda
1988
Kenya
Kenya Breweries
2–0
Al-Merrikh
Sudan
Sudan
1989
Kenya
Kenya Breweries
3–0
Coastal Union
Tanzania
Kenya
1991
Tanzania
Simba
3–0
Villa
Uganda
Tanzania
1992
Tanzania
Simba
1–1 [Penati 5-4]
Young Africans
Tanzania
Zanzibar
1993
Tanzania
Young Africans
2–1
Villa
Uganda
Uganda
1994
Sudan
Al-Merrikh
2–1
Express
Uganda
Sudan
1995
Tanzania
Simba
1–1 [Penati 5-3]
Express
Uganda
Tanzania
1996
Tanzania
Simba
1–0
Armée Patriotique
Rwanda
Tanzania
1997
Kenya
A.F.C. Leopards
1–0
Kenya Breweries
Kenya
Kenya
1998
Rwanda
Rayon Sports
2–1
Mlandege
Zanzibar
Zanzibar
1999
Tanzania
Young Africans
1–1 [Penati 4-1]
Villa
Uganda
Uganda
2000
Kenya
Tusker
3–1
Armée Patriotique
Rwanda
Rwanda
2001
Kenya
Tusker
0–0 [Penati 3-0]
Oserian
Kenya
Kenya
2002
Tanzania
Simba
1–0
Prince Louis
Burundi
Zanzibar
2003
Uganda
Villa
1–0
Simba
Tanzania
Uganda
2004
Rwanda
Armée Patriotique
3–1
Ulinzi Stars
Kenya
Rwanda
2005
Uganda
Villa
3–0
Armée Patriotique
Rwanda
Tanzania
2006
Uganda
Police
2–1
Moro United
Tanzania
Tanzania
2007
Rwanda
Armée Patriotique
2–1
URA
Uganda
Rwanda
2008
Kenya
Tusker
2–1
URA
Uganda
Tanzania
2009
Rwanda
ATRACO
1–0
Al-Merrikh
Sudan
Sudan
2011
Tanzania
Young Africans
1–0
Simba
Tanzania
Tanzania
2012
Tanzania
Young Africans
2–0
Azam
Tanzania
Tanzania
FAHAMU:
-Mashindano ya Mwaka 1967 hayakuwa rasmi
-Mashindano hayakufanyika kati ya Miaka ya 1968 hadi 1973, Mwaka 1990 & 2010.
-1974 Mashindano yalisimama.
Subscribe to:
Posts (Atom)


