Katika taarifa iliyoripotiwa na vyombo vya habari nchini Hispania vimeripoti kuwa wachezaji sita wa timu ya taifa ya Hispania wameibiwa fedha zao katika vyumba walivyofikia katika hoteli moja jijini Recife wakati wanacheza mchezo wao ufunguzi wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Uruguay. Mojawapo ya wachezaji waliokumbwa na zahama hilo ni beki wa Barcelona, Gerard Pique ambaye aligundua kaibiwa wakati aliporejea chumbani kwake baada ya mchezo dhidi ya Uruguay ambao walishinda kwa mabao 2-1. Msemaji wa Shirikisho la Soka Dunia-FIFA, Pekka Odriozola alikiri kupata taarifa hizo lakini wameziachia mamlaka husika kushughulikia na kisha kuwaletea taarifa kamili. Hispania ambao wako kundi B jana wamefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo kwa ushindi mkubwa baada ya kuitandika Tahiti kwa mabao 10-0 wakati wawakilishi pekee wa Afrika kwenye mashindano hayo walishindwa kujihakikishia nafasi ya kusonga mbele baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Uruguay.
Friday, June 21, 2013
Thursday, June 20, 2013
BRAZIL YAFANYA KWELI KOMBE LA MABARA-
TIMU ya taifa ya Brazil imeendeleza wimbi la ushindi katika mechi yake ya pili ya Kombe la Mabara ambapo mshambuliaji mpya wa FC Barcelona Neymar akiifungia timu yake bao safi kunako dakika ya 10 ya kipindi cha kwanza kabla ya kumtengenezea nafasi ya kufunga bao la pili Jo.
Brazil imeichalaza Mexico mabao 2-0 ambapo sasa imefanikiwa kufikisha ponti sita na kuzidi kuziweka katika nafasi nzuri na kuongoza Kundi A.
katika goli hili hilo Daniel Alves alipiga krosi safi kutoka kulia ambapo ilimfikia Neymar akaitokea kwa mbele ya beki wa Mexico, kabla ya kuhadaa na kumtungua kipa Jose Corona dakika ya tisa na dakika ya 90 akampa pande Jo kufunga la pili.
Katika mchezo huo uliokuwa chini refa Howard Webb wa Uingereza, kikosi cha Brazil kilikuwa: Cesar, Alves, Silva, Luiz, Marcelo, Luiz Gustavo, Paulinho, Oscar/Hernanes dk62, Hulk/Lucas Moura dk78, Neymar na Fred.
Mexico: Corona, Rodriguez, Salcido, Torrado, Dos Santos, Henandez, Moreno, Guardado, Torres/Barrera dk70, Mier na Flores/Herrera dk68.
MSIMAMO KUNDI A
NA
|
TIMU
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
PTS
|
1
|
Brazil
|
2
|
2
|
0
|
0
|
5
|
0
|
5
|
6
|
2
|
Italy
|
2
|
2
|
0
|
0
|
6
|
4
|
2
|
6
|
3
|
Mexico
|
2
|
0
|
0
|
2
|
1
|
4
|
-3
|
0
|
4
|
Japan
|
2
|
0
|
0
|
2
|
3
|
7
|
-4
|
0
|
MSIMAMO KUNDI B
NA
|
TIMU
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
PTS
|
1
|
Nigeria
|
1
|
1
|
0
|
0
|
6
|
1
|
5
|
3
|
2
|
Hispain
|
1
|
1
|
0
|
0
|
2
|
1
|
1
|
3
|
3
|
Uruguay
|
1
|
0
|
0
|
1
|
1
|
2
|
-1
|
0
|
4
|
Tahiti
|
1
|
0
|
0
|
1
|
1
|
6
|
-5
|
0
|
RATIBA LEO
Alhamis Juni 20
Saa 4 usiku
Spain vs Tahiti
Saa 7 usiku
Nigeria vs Uruguay
TAFAKARI YA LEO NA EDEN HAZARD KATIKA HARAKATI ZA ULIMWENGU WA SOKA.
TAARIFA KUHUSU YEYE | |||
---|---|---|---|
Full name | Eden Hazard | ||
Date of birth | 7 January 1991 (age 22) | ||
Place of birth | La Louvière, Belgium | ||
Height | 1.70 m (5 ft 7 in) | ||
Playing position | Winger | ||
TAARIFA KUHUSU CLUB | |||
Timu ya sasa | Chelsea | ||
Number | 17 | ||
TIMU ZA UJANA | |||
1995–2003 | Royal Stade Brainois | ||
2003–2005 | Tubize | ||
2005–2007 | Lille | ||
TIMU ZA UJANA | |||
Mwaka | Timu | Mechi | Goli |
2007–2012 | Lille | 147 | (36) |
2012– | Chelsea | 34 | (9) |
TIMU YA TAIFA | |||
2006 | Belgium U15 | 5 | (1) |
2006 | Belgium U16 | 4 | (2) |
2006–2008 | Belgium U17 | 17 | (2) |
2007–2009 | Belgium U19 | 11 | (6) |
2008– | Belgium | 37 | (5) |
TUZO NA VILABU
Lille fc
Ligue 1 (1): 2010-11
Coupe de France (1): 2010-11
Chelsea
UEFA Europa Ligi (1): 2012-13
TUZO BINAFSI
UNFP Ligue 1 Mchezaji wa Mwaka (2): 2010-11, 2011-12
UNFP Ligue 1 Mchezaji kijana wa Mwaka (2): 2008-09, 2009-10
UNFP Ligue 1 Timu ya Mwaka (3): 2009-10, 2010-11, 2011-12
UNFP Mchezaji wa Mwezi (3): Machi 2010, Machi 2011, [221] Machi 2012
Ligi Kuu ya PFA Timu ya Mwaka (1): 2012-13
Bravo tuzo (1): 2011
SERENA WILLIAMS AOMBA RADHI KATIKA GAZETI"
Mwanariadha nyota wa kike mahiri katika mchezo wa tenisi anayeshika namba moja katika orodha za ubora duniani kwa upande wanawake, Serena Williams ameomba radhi kwa kauli aliyoitoa katika gazeti la Rolling Stone kuhusiana na kesi ya ubakaji. Nyota huyo ambaye anatarajiwa kutetea ubingwa wake wa michuano ya Wimbledon alikaririwa na gezeti kuhusiana na kesi hiyo inayoendelea katika mji wa Steubenville, Ohio, Marekani. Katika kesi hiyo wachezaji wawili wa mpira wa miguu wa kimarekani wanatuhumiwa kumbaka msichana aliyelewa mwenye umri wa miaka 16 tukio ambalo walilifanya Machi mwaka huu. Gazeti hilo la Rolling Stone lilimkariri Williams akidai kuwa hamlaumu msichana huyo lakini kama una umri wa miaka 16 na unakunywa kiasi hicho wazazi wako wanatakiwa kukufundisha kwamba usipokee kinywaji kutoka kwa mtu usiyemfahamu.Kauli yake hilo ilishambuliwa na watu mbalimbali nchini humo mpaka kupelekea nyota kuomba radhi akidai kuwa hakumaanisha kama watu wanavyofikiri.
ANZHI MAKHACHKALA KUFUNGIWA NA UEFA.
Timu ya soka ya Anzhi Makhachkala ya Urusi kwa mara nyingine haitacheza mechi zake za Europa League msimu ujao mbali na uwanja wao wa nyumbani baada ya kufungiwa na Shirikisho la Soka barani-UEFA humo kwasababu za kiusalama. Katika taarifa ya UEFA iliyotumwa katika mtandao wake imedai kuwa baada ya kufanya utafiti wa usalama katika mji wa Kaskazini wa Caucasus ambao klabu hiyo inatoka wamegundua kuwepo usalama mdogo hivyo hawatoruhusu timu hiyo kucheza mechi zake nyumbani. UEFA imeitaka klabu hiyo kutafuta uwanja mbadala kwa ajili ya mechi zake za nyumbani za Europa League msimu wa 2013-2014. Anzhi walimaliza katika nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu nchini Urusi msimu uliopita na kukosa nafasi ya kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya.
Wednesday, June 19, 2013
BPL HADHARANI MAN U KUUMANA NA SWANSEA CITY
HATIMAYE RATIBA ya Ligi Kuu nchini Uingereza BPL kwa ajili ya msimu wa 2013-2014 imetoka huku mabingwa wa ligi hiyo Manchester United wakipangwa kufungua msimu na timu ya Swansea City. Ratiba hiyo itamshuhudia David Moyes akianza kibarua chake katika mechi ya kwanza kama bosi wa United dhidi ya timu hiyohiyo ambayo Sir Alex Ferguson alikutana nayo katika mchezo wake wa mwisho kabla ya kustaafu. Washindi wa pili wa ligi hiyo Manchester City watawakaribisha Newcastle United wakati Hull City ambayo imepanda daraja msimu huu itakuwa na safari ngumu pale watakapoifuata Chelsea, Stamford Bridge. Mechi nyingine Crystal Palace ambao nao wamepanda daraja msimu huu watawakaribisha Tottenham Hotspurs katika mchezo wa mahasimu wa jijini la London huku Arsenal wakiwakaribisha Aston Villa wakati Stoke City watakuwa wenyeji wa Liverpool. Nyingine ni Norwich watakuwa wenyeji wa Everton, Sunderland watakwaana na Fulham, West Bromwich na Southampton huku West Ham United wakichuana na Cardiff City.
PUYOL MBIONI KUFANYI UPOASUAJI WA GOTI LAKE"
Beki mahiri na mwenye nguvu za kukaba wa klabu ya Barcelona, Carles Puyol anatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa goti lake la kulia ambao utamuweka nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki tatu mpaka nne. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa katika mtandao wa klabu hiyo mchezaji huyo wa kimataifa wa Hispania anatarajiwa kufanyiwa upasuaji huo leo. Puyol mwenye umri wa miaka 35 amekuwa akisumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara katika miaka ya karibuni ukiwemo upasuaji wa mguu huohuo mara mbili, kuvunjika mfupa wa taya na pia kuteuka kiwiko cha mkono wake. Majeraha hayo yalimlazimu nyota huyo kukosa michuano ya Euro 2012 ambapo Hispania walitawadhwa mabingwa kwa mara ya pili mfululizo na pia kuenguliwa katika kikosi cha nchi hiyo kilichopo nchini Brazil kwa ajili ya michuano ya Kombe la Shirikisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)