Wakizungumza na mkali wa dimba mkaoni hapa baadhi ya walimbwende hao wamesema wamejiandaa vizuri kuhakikisha wanakonga Nyoyo za wadau mbalimbali watakao jitokeza katika kushuhudia mvutano huo.
Aidha mamiss hao walikuwa katika ziara ya Makamu wa Rais, Dk Mohammed Ghalib Bilal kuzindua mradi wa uwekezaji wa viwanda katika eneo pongwe jijini hapamapema leo asubuhi. Katika uzinduzi huo awali Rais Dk. Jakaya Kikwete ndiye aliyetarajiwa kuja kuzindua mradi huo, lakini badala yake amekuja Dk Bilal.
Hivyo katika shindano hilo mshindi wa kwanza anatarajiwa kujinyakulia kitita cha sh.laki tano 500,000 huku msanii wa muziki wa kizazi kipya, Tunda Man, akiongoza kwa upande wa Burudani, katika shindano litakalofanyika Jumamosi katika uwanja wa Mkwakwani.
Akizungumza na mkali wa dimba jijini hapa Mkurugenzi wa Kampuni ya DATK Intertainment Asha Kigundula,amesema kuwa maandalizi ya shindano hilo yapo vizuri kwa asilimia 100% ambapo zawadi kwa mshindi wa pili atajinyakulia kitita cha shilingi 300,000.
Mshindi wa tatu atazawadiwa kitita cha shilingi 250, 000 wakati mshindi wa nne na tano wakipata sh.200, 000 kila mmoja na warembo wengine watakaosalia watapata kitita cha sh.laki moja moja kila mmoja 100,000 kama kifuta jasho pamoja na zawadi kwa mrembo mwenye nidhamu ili kuweza kuboresha shindano hilo.
Hivyo katika shindano hilo mshindi wa kwanza anatarajiwa kujinyakulia kitita cha sh.laki tano 500,000 huku msanii wa muziki wa kizazi kipya, Tunda Man, akiongoza kwa upande wa Burudani, katika shindano litakalofanyika Jumamosi katika uwanja wa Mkwakwani.
Akizungumza na mkali wa dimba jijini hapa Mkurugenzi wa Kampuni ya DATK Intertainment Asha Kigundula,amesema kuwa maandalizi ya shindano hilo yapo vizuri kwa asilimia 100% ambapo zawadi kwa mshindi wa pili atajinyakulia kitita cha shilingi 300,000.

Kwa upande wa Burudani msanii wa kizazi kipya, Tunda Man, ataongoza safu ya burudani, ambapo itakuwa na wasanii mbalimbali wakiwemo Dr John, Nabisha kutoka kundi la THT, Fady Dady na wasanii chipukizi kutoka mkoani hapa.
Warembo hao ni Hawa Ramadhani (18),Hazina Mbaga (19)Like Abdulraman (19), Irene Thomas(20), Tatu Athumani (19), Winfrida Gutram (21)Lulu Mbonela (19) ,Hazina Daniel (19),Lulu Matawalo(22),Judithi Moleli (21),Neema Jonas na Hawa Twaybu(21)
Wakati huo huo Warembo hao wanaowania Taji la Mlimbwende wameiomba Halmashuri ya Jiji la Tanga kuifanyia marekebisho barabara inayokwenda katika mapango ya Amboni ili iweza kuwa nzuri na ipitike kirahisi nyakati zote.