Sunday, March 30, 2014

VPL:YANGA SC YAPINGWA 2-1 MKWAKWANI AZAM FC AILAMBA SIMBA 2-1

Jumamosi Machi 29
Ashanti United 2 JKT Oljoro 1
Jumapili Machi 30
Azam FC 2 Simba 1
Mgambo JKT 2 Yanga 1
Mbeya City 1 Tanzania Prisons 0
Kagera Sugar 0 v Ruvu Shooting 0
Mtibwa Sugar 3 v Coastal Union 1
JKT Ruvu 3 v Rhino Rangers 1
MABINGWA Watetezi Yanga Leo huko katika dimba la Mkwakwani Tanga walifungwa Bao 2-1 na Mgambo JKT iliyokuwa ikicheza Mtu 10 baada ya Mchezaji wao Mohamed Neto kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu katika Dakika ya 30 kwa kile kilichodaiwa kukutwa na Hirizi na kipigo hicho inaelekea kinapeleka Ubingwa kwa Azam FC ambao Leo wameichapa Simba Bao 2-1.
Huko Mkwakwani, Mgambo JKT walipata Bao lao la Kwanza Dakika ya Kwanza tu Mfungaji akiwa Fully Maganga na Yanga kusawazisha katika Dakika ya 50 kwa Penati ya Nadir Haroub "Cannavaro" lakini Penati nyingine iliyopigwa na Malima Busungu katika Dakika ya 69 iliwapa ushindi Mgambo JKT.
Jijini Dar es Salaam, Azam FC waliichapa Simba Bao 2-1 kwa Bao za Hamisi Mcha, Dakika ya 16, na John Bocco, Dakika ya 56 wakati Bao la Simba lilifungwa na Joseph Owino katika Dakika ya 45.
Matokeo haya yanaifanya Azam FC izidi kupaa kileleni wakiwa na Pointi 53 kwa Mechi 23 na kubakiza Mechi 3 huku Yanga wakiwa Nafasi ya Pili wakiwa na Pointi 46 kwa Mechi 22 na kubakisha Mechi 4.
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
PTS
1
Azam FC
23
15
8
0
31
53
2
Yanga SC
22
13
7
2
26
46
3
Mbeya City
23
12
9
2
13
45
4
Simba SC
23
9
9
5
15
36
5
Kagera Sugar
22
8
9
5
3
33
6
Mtibwa Sugar
22
7
8
7
1
29
7
Coastal Union
23
6
11
6
0
29
8
Ruvu Shooting
21
7
8
6
-4
29
9
JKT Ruvu
23
9
1
13
-13
28
10
Prison fc
22
3
10
9
-10
22
11
Mgambo JKT
22
5
6
11
-18
22
12
Ashanti united
22
5
6
11
-17
19
13
JKT Oljoro
23
2
9
12
-18
15
14
Rhino Rangers
23
2
7
14
-19
13
 
VPL-LIGI KUU VODACOM
RATIBA:
Jumamosi Machi 29
VPL_2013-2014-FPAshanti United v JKT Oljoro
Jumapili Machi 30
Mbeya City v Tanzania Prisons
Kagera Sugar v Ruvu Shooting
Mtibwa Sugar v Coastal Union
JKT Ruvu v Rhino Rangers
Azam FC v Simba
Mgambo JKT v Yanga

Saturday, March 29, 2014

MAN UNITED YAITANDIKA 4-1 ASTON VILLA, ROONEY ATUPIA MBILI NYAVUNI.

Je wajua  Furaha imerudi katika nafsi ya kocha David Moyes kufuatia Manchester United kuifunga mabao 4-1 Aston Villa Uwanja wa Old Trafford jioni hii katika mchezo wa Ligi Kuu ya England. 
Babu kubwa: Wayne Rooney amefunga mabao mawili leo Manchester United ikiifunga Aston Villa 4-1
Mabao mawili yaliyofungwa na Wayne Rooney dakika za 20 na 45 kwa penalti na mengine ya Juan Mata dakika ya 57 na Javier Hernandez dakika ya 90 yalitosha kuiongezea pointi United.
Villa ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Ashley Westwood dakika ya 13 kwa mpira wa adhabu.
United sasa inatimiza pointi54 baada ya kucheza mechi 32 na inaendelea kubaki nafasi ya saba nyuma ya Tottenham Hotspur yenye pointi 56 za mechi 31.

Inside out: As Mata turns inside Bacuna the defender takes the Spanish midfielders legs out
Juan Mata akipambana na Bacuna 
Cool and calm: Rooney powered the penalty into the side netting with precision leaving Guzan no chance
Rooney akifunga kwa penalti

SAMATTA NA ULIMWENGU TEGEMEZI KUIVUSHA MAZEMBE AFRIKA LEO.

Wanandinga wawili wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta na Thomas Emmanuel Ulimwengu leo wanatarajiwa kuiongoza klabu yao, TP Mazembe katika mchezo wa kuwania kutinga Nane Bora ya Ligi ya Mabingwa Afrika watakapoikaribisha Sewe Sport ya Ivory Coast Uwanja wa Mazembe mjini Lubumbashi, DRC. 
Samatta au ‘Sama Goal’ aliifungia bao muhimu la ugenini Jumapili iliyopita Mazembe ikifungwa 2-1 mjini Abidjan na leo wakiwa nyumbani watahitaji japo ushindi wa 1-0 ili kusonga mbele.
Kumbuka mwaka jana Mazembe ilitolewa katika hatua hii ya 16 Bora na Orlando Pirates ya Afrika Kusini iliyofika hadi fainali na kufungwa na Al Ahly ya Misri.
Mazembe iliangukia kwenye Kombe la Shirikisho ambako pia ilifika fainali na kufungwa na CS Sfaxien ya Tunisia.  
                            Mbwana Samatta
Timu hiyo ya Moise Katumbi safari hii imepania kurudi kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa na imejiandaa kiasi cha kutosha kujaribu kufuzu mtihani huo mgumu. Kila la heri Samatta na Ulimwengu pamoja na TP Mazembe.
Mechi nyingine za leo ni kati ya mabingwa watetezi, Al Ahly ya Misri dhidi ya Ahly Benghazi ya Libya itakayochezwa mjini Cairo, CS Sfaxien ya Tunisia itakayokuwa mwenyeji wa Horoya ya Guinea, Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini itaikaribisha AS Vita ya DRC.
Michuano hiyo itaendelea kesho wakati Zamalek ya Misri itakapokuwa mwenyeji wa Nkana ya Zambia, Coton Sport ya Cameroon na ES Setif ya Algeria, Esperance ya Tunisia na AS Bamako ya Mali, Al-Hilal ya Sudan na AC Leopards ya Kongo.