Wednesday, April 2, 2014

Nahodha wa timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes), Aishi Manula amesema wamejipanga kwa ajili ya kupata ushindi kwenye mechi dhidi ya Kenya itakayochezwa Jumapili (Aprili 6 mwaka huu) katika mji wa Machakos.

Akizungumza leo (Aprili 2 mwaka huu) kwenye hafla ya kukabidhiwa bendera kwa timu hiyo kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Manula ambaye pia anaidakia timu ya Azam alisema lengo lao ni kufanya vizuri kwenye mechi hiyo.

Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Michezo, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juliana Yasoda akikabidhi bendera hiyo, aliwataka wachezaji hao kujituma na kutanguliza uzalendo mbele bila kusahau kuwa mchezo wa mpira wa miguu ni ushirikiano.

Alisema Tanzania ina wachezaji wengi wenye vipaji, hivyo waliopata fursa ya kuwemo Ngorongoro Heroes wakati huu wajue kuwa wamepata bahati, na wanatakiwa kufahamu kuwa wao ni wawakilishi wa Tanzania, na Watanzania wana kiu ya kusikia matokeo ya mechi hiyo.

Ngorongoro Heroes inayofundishwa na John Simkoko inaondoka kesho (Aprili 3 mwaka huu) saa 4.30 asubuhi kwa ndege ya Kenya Airways, na mara baada ya kuwasili itakwenda moja kwa moja kwenye hoteli ya Garden iliyopo Machakos ambayo ndiyo imepangiwa kufikia na Shirikisho la Mpira wa Miguu Kenya (FKF).

Wachezaji waliopo kwenye msafara huo unaoongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF), Ayoub Nyenzi ni Abrahman Mohamed, Aishi Manula, Ally Idd, Ally Mwale, Athanas Mdamu, Ayoub Semtawa, Bryson Raphael na Edward Manyama.

Wengine ni Gadiel Michael, Hamad Juma, Hassan Mbande, Ibrahim Ahmada, Idd Ally, Kelvin Friday, Michael Mpesa, Mohamed Ibrahim, Mudhathir Yahya, Pato Ngonyani, Peter Manyika na Salum Mineli.

TIMU YA WATOTO WA MITAANI YACHACHAFYA BRAZIL
Timu ya Watoto wa Mitaani ya Tanzania kutoka Kituo cha Mwanza inaendelea vizuri katika mashindano ya Kombe la Dunia kwa Watoto wa Mitaani yanayoendelea Rio de Janeiro nchini Brazil ambapo katika mchezo wake wa kwanza ilitoka sare ya mabao 2-2 na Burundi.

Juzi (Machi 31 mwaka huu), timu hiyo inayoongozwa na mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kutoka Mkoa wa Mwanza, John Kadutu ilicheza mechi mbili. Katika mechi ya kwanza iliifunga Argentina mabao 3-0 na baadaye ikailaza Nicaragua mabao 2-0.

Michuano hiyo ya siku kumi inashirikisha timu kumi. Mbali ya Tanzania, nyingine ni
Argentina, Burundi, India, Kenya, Liberia, Marekani, Mauritius, Misri na Pakistan. Kwa wasichana ni Afrika Kusini, Brazil, El Salvador, Indonesia, Msumbiji, Nicaragua, Philippines, Uingereza na Zimbabwe.

UCL:MAN UNITED YAOMYESHA UBABE DHIDI YA BAYERN MUNICH.

MABINGWA watetezi ligi ya Mabingwa Ulaya, Bayern Munich, jana Usiku wamefanikiwa kupambana na kupata Sare ya Bao 1-1 waliposhuka dimbani Uwanjani Old Trafford kupambana na Mabingwa wa England Man United katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI na Bayern kumaliza Mtu 10 baada ya Kiungo wao mahiri, Bastian Schweinsteiger, kutolewa kwa Kadi Nyekundu kufuatia Kadi za Njano mbili.
Bayern walimiliki sana Mpira katika Kipindi cha Kwanza lakini ni Man United ndio waliokosa nafasi ya wazi wakati Danny Welbeck alipobaki yeye na Kipa Neuer na kujaribu kufunga kiufundi lakini Kipa huyo wa Germany akaokoa Bao la wazi.
Mapema kwenye Dakika ya 3, Welbeck alifanikiwa kufunga Bao safi lakini Refa Carlos Velasco Carballo kutoka Spain alilikataa na kuwaacha Wachambuzi wengi kukuna vichwa vyao kwanini Bao hilo lilikataliwa.
Hadi Mapumziko Mechi hii ilikuwa 0-0.
Kipindi cha Pili, Dakika ya 58, Man United walifunga Bao kwa Kichwa cha Nahodha wao Nemanja Vidic baada kuunganisha Kona ya Wayne Rooney.
Bayern walisawazisha katika Dakika ya 66 baada ya Krosi ya kumkuta Mario Mandzukic aliemsogezea Bastian Schweinsteiger na kufunga.
Katika Mechi ya Marudiano, mbali ya kumkosa Bastian Schweinsteiger pia itamkosa Javi Martinez baada Mchezaji huyo kuzoa Kadi ya Njano ambayo itamfanya akose Mechi ya Marudiano.
Timu hizi zitarudiana huko Allianz Arena Jijini Munich hapo Jumatano Aprili 9.
VIKOSI:
MANCHESTER UNITED: De Gea; Jones, Ferdinand, Vidic, Büttner; Valencia, Carrick, Fellaini, Giggs, Welbeck; Rooney
Akiba: Lindegaard, Hernandez, Nani, Young, Fletcher, Januzaj, Kagawa.
BAYERN MUNICH: Neuer; Rafinha, Boateng, Martinez, Alaba; Lahm; Robben, Kroos, Schweinsteiger, Ribéry; Muller
Akiba: Starke, Van Buyten, Mandzukic, Shaqiri, Pizarro, Gotze, Hojbjerg.
REFA: Carlos Velasco Carballo (Spain).
Robo Fainali
Mechi za Kwanza
Jumanne Aprili 1
Barcelona 1 Atletico Madrid 1
Manchester United 1 Bayern Munich 1
Katika mtanange mwingine usiku wa jana kwa mara ya 4 Msimu huu, Barcelona na Atletico Madrid zimetoka tena Sare ya bao 1-1 Uwanjani Nou Camp katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Licha ya Barca kutawala Kipindi cha Kwanza, hadi Mapumziko Bao zilikuwa 0-0 na kila Timu ilipata pigo baada kupata Majeruhi kwa Barca kulazimika kumtoa Pique na kumuingiza Bartra na Atletico kumtoa Diego Costa na Ribas Diego kuwa mbadala.
Kipindi cha Pili, Atletico walitangulia kuingia wavuni katika Dakika ya 57 kwa Bao la Ribas Diego na Neymar kusawazisha katika Dakika ya 71.
Timu hizi zitarudiana huko Estadio Vicente Calderon hapo Jumatano Aprili 9.
 VIKOSI:
BARCELONA: Pinto; Alves, Piqué, Mascherano, Alba; Busquets, Xavi; Cesc, Iniesta, Neymar; Messi
Akiba: Oier, Adriano, Song, Bartra, Sergi Roberto, Alexis, Pedro.
ATLÉTICO MADRID: Courtois; Juanfran, Godin Miranda, Filipe Luis; Tiago, Gabi; Arda Turan, Villa, Koke; Diego Costa
Akiba: Aranzubia, Alderweireld, Insua, Mario Suarez, Cristian Rodriguez, Sosa, Diego.
REFA: Felix Brych (Germany)
Jumatano Aprili 2
Real Madrid v Borussia Dortmund
Paris Saint-Germain v Chelsea
Marudiano
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Jumanne Aprili 8
Chelsea v Paris Saint-Germain
Borussia Dortmund v Real Madrid
Jumatano Aprili 9
-DROO YA NUSU FAINALI: 11 Aprili
-Mechi kuchezwa 22 & 23 Aprili na Marudiano 29 & 30 Aprili
-FAINALI: Estádio da Luz, Lisbon, Portugal 24 Mei 2014.
WASHINDI [Miaka ya karibu]:
MSIMU MSHINDI NCHI MSHINDI WA PILI NCHI GOLI
2012-13 Bayern Munich Germany Borussia Dortmund Germany 2-1
2011-12 Chelsea England Bayern Munich Germany 1-1 (4–3)
2010-11 Barcelona Spain Manchester United England 3-1
2009-10 Internazionale Italy Bayern Munich Germany 2-0
2008-09 Barcelona Spain Manchester United England 2-0
2007-08 Man United England Chelsea England 1-1 (6–5)
UEFA CHAMPIONZ LIGI
WAFUNGAJI BORA 2013/14:
C. Ronaldo-Real Madrid Goli 13
Zlatan Ibrahimovic-PSG Goli 10 [Penati 1]
Messi-Barcelona Goli 8 [Penati 2]
Diego Costa-Atletico Madrid Goli 7
Sergio Agüero-Manchester City Goli 6 [Penati 2]