MABINGWA
watetezi ligi ya Mabingwa Ulaya, Bayern Munich, jana Usiku wamefanikiwa kupambana na kupata Sare ya Bao 1-1 waliposhuka dimbani Uwanjani Old Trafford kupambana na Mabingwa wa England Man United katika Mechi ya
Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI na Bayern kumaliza Mtu 10
baada ya Kiungo wao mahiri, Bastian Schweinsteiger, kutolewa kwa Kadi
Nyekundu kufuatia Kadi za Njano mbili.

Mapema kwenye Dakika ya 3, Welbeck
alifanikiwa kufunga Bao safi lakini Refa Carlos Velasco Carballo kutoka
Spain alilikataa na kuwaacha Wachambuzi wengi kukuna vichwa vyao kwanini
Bao hilo lilikataliwa.
Hadi Mapumziko Mechi hii ilikuwa 0-0.
Bayern walisawazisha katika Dakika ya 66
baada ya Krosi ya kumkuta Mario Mandzukic aliemsogezea Bastian
Schweinsteiger na kufunga.
Katika Mechi ya Marudiano, mbali ya
kumkosa Bastian Schweinsteiger pia itamkosa Javi Martinez baada Mchezaji
huyo kuzoa Kadi ya Njano ambayo itamfanya akose Mechi ya Marudiano.
Timu hizi zitarudiana huko Allianz Arena Jijini Munich hapo Jumatano Aprili 9.
VIKOSI:
MANCHESTER UNITED: De Gea; Jones, Ferdinand, Vidic, Büttner; Valencia, Carrick, Fellaini, Giggs, Welbeck; Rooney
Akiba: Lindegaard, Hernandez, Nani, Young, Fletcher, Januzaj, Kagawa.
BAYERN MUNICH: Neuer; Rafinha, Boateng, Martinez, Alaba; Lahm; Robben, Kroos, Schweinsteiger, Ribéry; Muller
Akiba: Starke, Van Buyten, Mandzukic, Shaqiri, Pizarro, Gotze, Hojbjerg.
REFA: Carlos Velasco Carballo (Spain).
Robo Fainali
Mechi za Kwanza
Jumanne Aprili 1
Barcelona 1 Atletico Madrid 1
Manchester United 1 Bayern Munich 1
Katika mtanange mwingine usiku wa jana kwa mara ya 4 Msimu huu, Barcelona na
Atletico Madrid zimetoka tena Sare ya bao 1-1 Uwanjani Nou
Camp katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Licha ya Barca kutawala Kipindi cha
Kwanza, hadi Mapumziko Bao zilikuwa 0-0 na kila Timu ilipata pigo baada
kupata Majeruhi kwa Barca kulazimika kumtoa Pique na kumuingiza Bartra
na Atletico kumtoa Diego Costa na Ribas Diego kuwa mbadala.
Kipindi cha Pili, Atletico walitangulia
kuingia wavuni katika Dakika ya 57 kwa Bao la Ribas Diego na Neymar kusawazisha
katika Dakika ya 71.
Timu hizi zitarudiana huko Estadio Vicente Calderon hapo Jumatano Aprili 9.
VIKOSI:
BARCELONA: Pinto; Alves, Piqué, Mascherano, Alba; Busquets, Xavi; Cesc, Iniesta, Neymar; Messi
ATLÉTICO MADRID: Courtois; Juanfran, Godin Miranda, Filipe Luis; Tiago, Gabi; Arda Turan, Villa, Koke; Diego Costa
Akiba: Aranzubia, Alderweireld, Insua, Mario Suarez, Cristian Rodriguez, Sosa, Diego.
REFA: Felix Brych (Germany)
Jumatano Aprili 2
Paris Saint-Germain v Chelsea
Marudiano
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Jumanne Aprili 8
Chelsea v Paris Saint-Germain
Borussia Dortmund v Real Madrid
Jumatano Aprili 9
-DROO YA NUSU FAINALI: 11 Aprili
-Mechi kuchezwa 22 & 23 Aprili na Marudiano 29 & 30 Aprili
-FAINALI: Estádio da Luz, Lisbon, Portugal 24 Mei 2014.
WASHINDI [Miaka ya karibu]:
MSIMU | MSHINDI | NCHI | MSHINDI WA PILI | NCHI | GOLI |
2012-13 | Bayern Munich | Germany | Borussia Dortmund | Germany | 2-1 |
2011-12 | Chelsea | England | Bayern Munich | Germany | 1-1 (4–3) |
2010-11 | Barcelona | Spain | Manchester United | England | 3-1 |
2009-10 | Internazionale | Italy | Bayern Munich | Germany | 2-0 |
2008-09 | Barcelona | Spain | Manchester United | England | 2-0 |
2007-08 | Man United | England | Chelsea | England | 1-1 (6–5) |
UEFA CHAMPIONZ LIGI
WAFUNGAJI BORA 2013/14:
C. Ronaldo-Real Madrid Goli 13
Zlatan Ibrahimovic-PSG Goli 10 [Penati 1]
Messi-Barcelona Goli 8 [Penati 2]
Diego Costa-Atletico Madrid Goli 7
Sergio Agüero-Manchester City Goli 6 [Penati 2]