Saturday, April 19, 2014

ASHANT,JKT OLJORO, RHINO RANGERS MKONO WA KWAHERI ZASHUKA DARAJA



Ligi kuu Vodacom Tanzania bara leo imefikia tamati baada ya timu zote kusha dimbani katika viwanja saba hapa nchini ambapo Azam FC imekabidhiwa Kombe lao huko Azam Complex, Chamazi mara baada ya Mechi yao ya kukamilisha Ratiba ambayo waliifunga JKT Ruvu Bao 1-0.
Kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es Salaam, Watani wa Jadi, Yanga na Simba nao walikutana kwenye Dabi ya Kariakoo, isiyokuwa na maan
a yeyote mbali ya kukamilisha Ratiba, na kutoka Sare ya Bao 1-1.
Kwenye Mechi hiyo, iliyohudhuriwa na Watazamaji wachache tofauti na desturi, Simba walitangulia kufunga Bao katika Dakika ya 76 Mfungaji akiwa Haruna Chanongo na Yanga kusawazisha kwa Bao la Dakika ya 86 la Simon Msuva.
Mechi pekee iliyokuwa na umuhimu mkubwa ni ile iliyochezwa Uwanja wa Jamhri huko Morogoro kati ya Tanzania Prisons na Ashanti United na Prisons kuifunga Ashanti Bao 1-0 na wao kupona na kuishusha Daraja Ashanti ambao wa
naungana na JKT Oljoro na Rhino Rangers kuporomoka Daraja.
VPL, LIGI KUU VODACOM
Mechi za mwisho za Ligi
Ratiba/Matokeo:
Jumamosi Aprili 19
Rhino Rangers v Ruvu Shooting [Ali Hassan Mwinyi, Tabora]
Mbeya City 1 Mgambo JKT 0 [Sokoine, Mbeya]
Tanzania Prisons 1 Ashanti United 0 [Jamhuri, Morogoro]
JKT Ruvu 0 Azam FC [Azam 1 Complex, Chamazi]
JKT Oljoro 1 Mtibwa Sugar 1 [Sheikh Amri Abeid, Arusha]
Coastal Union 0 Kagera Sugar 1 [Mkwakwani, Tanga]
Yanga 1 Simba 1 [National Stadium, Dar es Salaam]
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Azam FC
26
18
8
0
51
15
36
62
2
Young Africans
26
16
8
2
61
19
42
56
3
Mbeya City
26
13
10
3
33
20
13
49
4
Simba SC
26
9
11
6
41
27
14
38
5
Kagera Sugar
26
9
11
6
23
20
3
38
6
Ruvu Shooting
25
9
8
8
26
32
-6
35
7
Mtibwa Sugar
26
7
10
9
30
31
-1
31
8
JKT Ruvu
26
10
1
15
23
40
-17
31
9
Coastal Union
26
6
11
9
17
20
-3
29
10
Mgambo JKT
26
6
8
12
18
35
-17
26
11
Tanzania Prisons
26
6
10
10
26
33
-7
28
12
Ashanti United
26
6
7
13
20
39
-19
25
13
JKT Oljoro
26
3
10
13
19
37
-18
19
14
Rhino Rangers
25
3
7
15
18
37
-19
16

SIMBA YANGA HAKUNA MBABE AZAM YAKABIDHIWA NDOO.

Goli la dakika ya 86 la Simon Msuva dakika ya 86, jioni hii limeinusuru Yanga SC kulala mbele ya wapinzani wake, Simba SC baada ya kupata sare ya 1-1 katika mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati Uwanja wa Azam Complex, Chamazi bao la Brian Umony limeipa Azam ushindi wa 1-0 dhidi ya JKT Ruvu.

Simba SC ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa Haroun Chanongo dakika ya 68 na kwa matokeo hayo, Azam inamaliza Ligi Kuu na pointi 62 wakati Yanga SC inamaliza na pointi 56 katika nafasi ya pili- ambapo sasa Azam FC ni mabingwa wapya ambao hawaja poteza mechi hata moja katika msimu wa Ligi Kuu  2013/2014.

Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ameikabidhi mkabidhi Kombe la ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni hii baada ya kuifunga bao 1-0 JKT Ruvu Uwanja wa Azam C
omplex, Chamazi, Dar es Salaam.


Mabingwa hao wakisherehekea na taji lao ambapo sherehe za ubingwa zimeanza jioni hii katika uwanja wa  Complex hadi usiku wa mana
ne

Mbali ya yotetimu zilizoshuka daraja msimu huu ni Ashanti United, Jkt Oljoro Pamoja na Rhino Rangers ambazo zimeaga mkono wa
kwaheri kuzipisha timu za Stends United ya shinyanga,Polisi Morogoro Pamoja na Ndanda fc ya Mtwara.

19 WAITWA TAIFA STARS KUUNGANA NA 16 KUTOKA MABORESHO

19 WENGINE WATAJWA TAIFA STARS
Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Salum Mayanga ametangaza wachezaji wengine 23 watakaoingia kambini kesho (Aprili 20 mwaka huu) kuungana na 16 waliotajwa awali kujiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Burundi itakayochezwa Aprili 26 mwaka huu.
Wachezaji walioitwa ni makipa Aishi Manula (Azam), Deogratias Munishi (Yanga) na Mwadili Ali (Azam). Mabeki ni Abdi Banda (Coastal Union), Aidan Michael (Ruvu Shooting), Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Hassan Mwasapili (Mbeya City), Kelvin Yondani na Said Moradi (Azam).
Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Frank Domayo (Yanga), Himid Mao (Azam) na Jonas Mkude (Simba).
Washambuliaji ni Athanas Mdamu (Alliance), Haruna Chanongo (Simba), Juma Liuzio (Mtibwa Sugar), Khamis Mcha (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngasa (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Markhiya, Qatar), Ramadhan Singano (Simba), Simon Msuva (Yanga) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC).
Wachezaji walioitwa kutoka katika kikosi cha maboresho ni kipa Benedicto Tinoko Mlekwa (Mara), mabeki wa kati; Emma Namwondo Simwanda (Temeke) na Joram Nason Mgeveje (Iringa). Walinzi wa pembeni ni Omari Ally Kindamba (Temeke), Edward Peter Mayunga (Kaskazini Pemba) na Shiraz Abdallah Sozigwa (Ilala).
Viungo ni Yusuf Suleiman Mlipili (Temeke), Said Juma Ally (Mjini Magharibi), Abubakar Ally Mohamed (Kusini Unguja), Hashim Ramadhan Magona (Shinyanga), Omari Athumani Nyenje (Mtwara) na Chunga Said Zito (Manyara).
Washambuliaji ni Mohammed Seif Saidi (Kusini Pemba), Ayoub Kasim Lipati (Ilala), Abdurahman Othman Ally (Mjini Magharibi), Paul Michael Bundara (Ilala). Wachezaji wa U 20 ni Mbwana Mshindo Musa (Tanga) na Bayaga Athanas Fabian (Mbeya).
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itaingia kambini kwenye hoteli ya Kunduchi Beach.
MICHUANO YA BEACH SOCCER YAIVA
Michuano ya mpira wa miguu ya ufukweni (Beach Soccer) inazinduliwa rasmi kesho (Aprili 20 mwaka huu) kwenye ufukwe wa Escape One uliopo Mikocheni, Dar es Salaam na kushirikisha timu 13.
Uzinduzi huo utaanza saa 5 asubuhi na mechi zitachezwa hadi saa 11 jioni. Michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya kwanza nchini inashirikisha timu 13 kutoka vyuo mbalimbali vya jijini Dar es Salaam.
Vyuo hivyo ni Chuo Kikuu cha Ardhi (AU), Chuo Kikuu cha St. Joseph Tanzania (SJUIT), Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam (TUDARCO), Chuo cha Ustawi wa Jamii (ISW), Chuo cha Uandishi wa Habari Dar es Salaam (DSJ) na Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.
Vingine ni Chuo cha Utumishi wa Umma Magogoni, Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Chuo cha Utawala wa Kodi (ITA) na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).
Michuano hiyo itakuwa inachezwa Jumamosi na Jumapili kwenye fukwe za Escape One na Gorilla Beach iliyopo Kigamboni, Dar es Salaam.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Friday, April 18, 2014

BUNDESLIGA KESHO KILINGENI KESHO

RATIBA
Jumamosi Aprili 19
BV Borussia Dortmund v FSV Mainz 05
SV Werder Bremen v TSG Hoffenheim
SC Freiburg v Borussia Mönchengladbach
Eintr. Braunschweig v Bayern Munich
FC Augsburg v Hertha Berlin
Hamburger SV v VfL Wolfsburg
Jumapili Aprili 20
FC Nuremberg v Bayer 04 Leverkusen
VfB Stuttgart v Schalke 04
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GDS
PTS
1
Bayern Munich
30
25
3
2
82
20
62
78
2
BV Borussia Dortmund
30
19
4
7
67
32
35
61
3
Schalke 04
30
17
7
6
56
38
18
58
4
Bayer 04 Leverkusen
30
16
3
11
50
37
13
51
5
VfL Wolfsburg
30
15
5
10
53
45
8
50
6
Borussia Mönchengladbach
30
14
7
9
52
35
17
49
7
FSV Mainz 05
30
14
5
11
44
45
-1
47
8
FC Augsburg
30
12
6
12
41
45
-4
42
9
TSG Hoffenheim
30
10
10
10
66
63
3
40
10
Hertha Berlin
30
10
7
13
38
42
-4
37
11
Eintracht Frankfurt
30
9
8
13
37
50
-13
35
12
SV Werder Bremen
30
8
9
13
34
58
-24
33
13
Hannover 96
30
9
5
16
38
55
-17
32
14
SC Freiburg
30
8
8
14
35
52
-17
32
15
VfB Stuttgart
30
7
7
16
45
58
-13
28
16
Hamburger SV
30
7
6
17
46
62
-16
27
17
FC Nuremberg
30
5
11
14
35
58
-23
26
18
Eintr. Braunschweig
30
6
7
17
28
52
-24
25