Sunday, May 11, 2014
RUVU SHOOTING YAMNASA MCHEZAJI TOKA KAGERA SUGAR.
Club ya Ruvu Shooting ya mkoani pwani imefanikiwa kumnsa mchezaji mahiri wa timu ya Kagera sugar nafasi ya midfild
kwa kipindi cha misimu miwili iliyopita, Zuberi Kasim Dabi ambapo amesaini dili la
mkataba wa miaka miwili kuichezea timu hiyo ya Pwani.
Dabi amesaini mkataba huo Ijumaa hii, Mei 9, 2014 katika ofisi za Ruvu shooting zilizoko Mlandizi, Pwani mbele ya uongozi wa timu hiyo ukiongozwa na Mwenyekiti wake, Kanali Charles Mbuge.
Dabi kabla ya kujiunga na Kagera sugar amewahi pia kuzichezea timu za Villa Squad ya Dar es salaam, Polisi Morogoro ambayo musimu huu imefanikiwa kupanda daraja, kucheza ligi kuu.
Ruvu shooting ipo katika mchakato mkali na mkubwa kukisuka kikosi chake kwa kusajili wachezaji wenye uwezo kama kocha wake mkuu Tom Olaba alivyoshauri.
Wakati Ruvu shooting wakisajili wachezaji wa timu kubwa, tayari kikosi hicho kimeivunja timu ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 na kutangaza kukiunda upya kwa kuwafanyia majaribio wachezaji vijana kati ya Mei 15-28, majaribio ambayo yatafanyika katika uwanja wa Mabatini, Mlandizi
Dabi amesaini mkataba huo Ijumaa hii, Mei 9, 2014 katika ofisi za Ruvu shooting zilizoko Mlandizi, Pwani mbele ya uongozi wa timu hiyo ukiongozwa na Mwenyekiti wake, Kanali Charles Mbuge.
Dabi kabla ya kujiunga na Kagera sugar amewahi pia kuzichezea timu za Villa Squad ya Dar es salaam, Polisi Morogoro ambayo musimu huu imefanikiwa kupanda daraja, kucheza ligi kuu.
Ruvu shooting ipo katika mchakato mkali na mkubwa kukisuka kikosi chake kwa kusajili wachezaji wenye uwezo kama kocha wake mkuu Tom Olaba alivyoshauri.
Wakati Ruvu shooting wakisajili wachezaji wa timu kubwa, tayari kikosi hicho kimeivunja timu ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 na kutangaza kukiunda upya kwa kuwafanyia majaribio wachezaji vijana kati ya Mei 15-28, majaribio ambayo yatafanyika katika uwanja wa Mabatini, Mlandizi
M/KITI WA YANGA YUSUPH MANJI AUNGURUMA MBELE YA WAANDISHI WA HABARI.
Mwenyekiti wa Young Africans Bw Yusuf Manji akiongea na wanachama, wazee na waandishi wa habari leo makuu ya klabu ya Yanga
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu leo, Manji
amesema yameongelewa mengi sana kwa kipindi cha mwezi mmoja ambao
hakuwepo nchini kwa ajili ya kazi zake binafsi lakini sasa amerejea na
maandalizi ya msimu ujao yameshaanza.
Kuondoka kwa Kavumbagu ni
kutokana na kuchelewa kwa majibu ya TFF juu ya idadi ya wachezaji wageni
kwa msimu mpya, huku Domayo ambae tangu mwaka jana aliombwa kuongeza
mkataba alikua akisema anamsubiria mjomba wake ndipo aweze kufanya
hivyo.
Pamoja na kuondoka kwa
wachezaji hao bado kwa kushirikiana na kocha Hans watahakikisha Yanga
inaendelea kutisha msimu ujao na kufanya vizuri kwenye mashindano ya
kimataifa, Hans aliahidi kuleta wachezaji wazuri watakaoisaidia Yanga
siku alipokua akiiongea na waandishi wa habari kuwaaga.

1.
Ally Kamtande, 2. Isiaka Dude, 3. Hamisi Matandula, 4.Waziri Jitu
Ramadhani, 5.Mohamed Kigali Ndimba , 6. Selaman Hassan Migali
Mkutano
mkuu wa mabadiliko ya katiba utafanyika terehe mosi Juni, 2014 katika
Ukumbi wa Oysterbay Police Mess na wanachama wote wanaombwa kulipia ada
zao ili waweze kuhuhudhira mkutano huo wakiwa hai.
Suala la
ujenzi wa Uwanja wa Kisasa eneo la Jangwani bado lipo pale pale, kikubwa
kinachosubirwa ni majibu ya serikali juu ya maombi ya eneo la ziada,
kwani Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam alisema suala hilo lipo ukingoni na
mda si mrefu.
Friday, May 9, 2014
MAKOCHA NGORONGORO HEROES, EAGLES KUTETA
Makocha wa timu za Tanzania (Ngorongoro Heroes), John Simkoko na Nigeria (Flying Eagles), Manu Garba wanakutana na waandishi wa habari kuzungumzia mikakati yao kwa ajili ya mechi ya Jumapili.

Mechi
hiyo ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye
umri chini ya miaka 20 itafanyika Jumapili (Mei 11 mwaka huu) saa 10
kamili jioni katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
RCL YAANZA KUTIMUA VUMBI KATIKA VITUO VITATU
Na Boniface Wambura, Dar es salaam
Michuano ya Ligi ya Mabingwa wa
Mikoa (RCL) inayoshirikisha timu 27 inaanza kutimua vumbi kesho (Mei 10
mwaka huu) katika vituo vitatu vya Morogoro, Mbeya na Shinyanga kwa
mechi mbili kila siku.
Kundi A ambalo mechi zake zinachezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, African Sports ya Tanga itacheza na Kiluvya United FC ya Pwani saa 8 mchana wakati saa 10 jioni ni Mji Mkuu FC (CDA) ya Dodoma dhidi ya Pachoto Shooting Stars ya Mtwara.
Jumapili (Mei 11 mwaka huu) katika
kundi hilo kutakuwa na mechi kati ya Bulyanhulu FC (Shinyanga) na
Kariakoo SC (Lindi) itakayoanza saa 8 mchana wakati saa 10 jioni ni Navy
FC (Dar es Salaam) na Abajalo FC pia ya Dar es Salaam.
Kundi B katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya litaanza ligi kwa mechi kati ya Ujenzi (Rukwa) na Volcano FC (Morogoro) saa 8 mchana wakati saa 10 jioni ni AFC ya Arusha na Panone FC ya Kilimanjaro.
Mei 11 mwaka huu saa 8 mchana ni Mpanda United ya Katavi na Magereza ya Iringa wakati Tanzanite (Manyara) na Njombe Mji (Njombe) zenyewe zitaumana kuanzia saa 10 jioni.
Simiyu United ya Simiyu na Mvuvumwa FC (Kigoma) ndizo zitakazoanza kucheza saa 8 mchana katika kundi C linalotumia Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga. Saa 10 jioni ni mechi kati ya Wenda FC ya Mbeya na mabingwa wa Mkoa wa Kagera, Eleven Stars FC.
Jumapili (Mei 11 mwaka huu), mechi za kundi hilo zitakuwa Singida United (Singida) na Mbao FC ya Mwanza kuanzia saa 8 mchana wakati jioni ni pambano kati ya mabingwa wa Mkoa wa Mara, JKT Rwamkoma FC na Geita Veterans FC ya Geita.
Ligi hiyo itamalizika Juni 2 mwaka huu ambapo timu itakayoongoza kila kundi itapanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu wa 2014/2015.
Kundi A ambalo mechi zake zinachezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, African Sports ya Tanga itacheza na Kiluvya United FC ya Pwani saa 8 mchana wakati saa 10 jioni ni Mji Mkuu FC (CDA) ya Dodoma dhidi ya Pachoto Shooting Stars ya Mtwara.

Kundi B katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya litaanza ligi kwa mechi kati ya Ujenzi (Rukwa) na Volcano FC (Morogoro) saa 8 mchana wakati saa 10 jioni ni AFC ya Arusha na Panone FC ya Kilimanjaro.
Mei 11 mwaka huu saa 8 mchana ni Mpanda United ya Katavi na Magereza ya Iringa wakati Tanzanite (Manyara) na Njombe Mji (Njombe) zenyewe zitaumana kuanzia saa 10 jioni.
Simiyu United ya Simiyu na Mvuvumwa FC (Kigoma) ndizo zitakazoanza kucheza saa 8 mchana katika kundi C linalotumia Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga. Saa 10 jioni ni mechi kati ya Wenda FC ya Mbeya na mabingwa wa Mkoa wa Kagera, Eleven Stars FC.
Jumapili (Mei 11 mwaka huu), mechi za kundi hilo zitakuwa Singida United (Singida) na Mbao FC ya Mwanza kuanzia saa 8 mchana wakati jioni ni pambano kati ya mabingwa wa Mkoa wa Mara, JKT Rwamkoma FC na Geita Veterans FC ya Geita.
Ligi hiyo itamalizika Juni 2 mwaka huu ambapo timu itakayoongoza kila kundi itapanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu wa 2014/2015.
Thursday, May 8, 2014
MABADILIKO YA KATIBA YANGA SC JUNI MOSI MWAKA HUU
Uongozi wa klabu ya Young
Africans Sports Club umeitisha mkutano mkuu wa wanachama wa mabadiliko
ya Katiba ili wanachama waweze kutoa maamuzi kwenye baadhi ya vipengele
vilivyoongezwa kabla ya kuelekea kwenye mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa
viongozi.

“Tumekua na mawasiliano na TFF
juu ya kuongezwa baadhi ya vipengele kwenye Katiba yetu kabla ya kufanya
uchaguzi mkuu wa viongozi, baada ya hapo ni nafasi kwa wanachama wa
Yanga sasa kukutana na kuweza kupitisha hivyo vipengele vitakavyoongezwa
kwenye Katiba Mpya” alisema Beno.
Aidha Beno amesema wanachama
wakishapitisha/kukubaliana juu ya hivyo vipengele ndipo uoungozi
utawasilisha mapendekezo hayo kwa TFF ambayo ikishayabariki,
yatapelekewa kwa Msajili nae akiyapitisha ndipo itakua tayari ni Katiba
halali ambayo itatumika kwwenye uchaguzi mkuu.
“Nawaomba wanachama wa Yanga
wajitokeze kwa wingi kwenye mkutano wa mabadiliko juni mosi 2014 ili
waweze kupitisha hivyo vipengele ambavyo vitapelekea kuwa na Katiba Mpya
itakayotumika kwa shughuli za kila siku za klabu ya Yanga SC” aliongea
Beno.
Eneo na Ukumbi utakapofanyika mkutano huo Juni Mosi 2014 utatangazwa hivi karibuni mara baada ya taratibu zote kukamilika.
Chanzo: Tovuti ya Yanga
PLUIJM ABWAGA MANYANGA YANGA SC, ATIMKIA HUKO UARABUNI
KOCHA mkuu
wa Young Africans, Mholanzi, Hans Van der Pluijm amepata kazi mpya
nchini Saudi Arabia na tayari ameshaaga rasmi mchana huu kwa wachezaji
wake, viongozi, wapenzi na wanachama wa klabu hiyo.
Pluijm
aliyejiunga na Yanga mapema januari mwaka huu umepata shavu hilo katika
klabu ya Al Shoalah FC inayoshiriki ligi kuu soka nchini Saudi Arabia.

Yanga
chini ya Pluijm ilimaliza katika nafasi ya pili, huku Azam fc chini ya
kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog wakibeba taji lao la kwanza tangu
wapande ligi kuu msimu wa 2008/2009.
Pluijm
alirithi mikoba ya mholanzi mwenzake, Ernie Brandts aliyetimuliwa mwezi
desemba mwaka jana baada ya kufungwa mabao 3-1 na Simba katika mechi ya
Nani Mtani Jembe.
Subscribe to:
Posts (Atom)