Mwenyekiti wa Young Africans Bw Yusuf Manji akiongea na wanachama, wazee na waandishi wa habari leo makuu ya klabu ya Yanga
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu leo, Manji
amesema yameongelewa mengi sana kwa kipindi cha mwezi mmoja ambao
hakuwepo nchini kwa ajili ya kazi zake binafsi lakini sasa amerejea na
maandalizi ya msimu ujao yameshaanza.
Kuondoka kwa Kavumbagu ni
kutokana na kuchelewa kwa majibu ya TFF juu ya idadi ya wachezaji wageni
kwa msimu mpya, huku Domayo ambae tangu mwaka jana aliombwa kuongeza
mkataba alikua akisema anamsubiria mjomba wake ndipo aweze kufanya
hivyo.
Pamoja na kuondoka kwa
wachezaji hao bado kwa kushirikiana na kocha Hans watahakikisha Yanga
inaendelea kutisha msimu ujao na kufanya vizuri kwenye mashindano ya
kimataifa, Hans aliahidi kuleta wachezaji wazuri watakaoisaidia Yanga
siku alipokua akiiongea na waandishi wa habari kuwaaga.

1.
Ally Kamtande, 2. Isiaka Dude, 3. Hamisi Matandula, 4.Waziri Jitu
Ramadhani, 5.Mohamed Kigali Ndimba , 6. Selaman Hassan Migali
Mkutano
mkuu wa mabadiliko ya katiba utafanyika terehe mosi Juni, 2014 katika
Ukumbi wa Oysterbay Police Mess na wanachama wote wanaombwa kulipia ada
zao ili waweze kuhuhudhira mkutano huo wakiwa hai.
Suala la
ujenzi wa Uwanja wa Kisasa eneo la Jangwani bado lipo pale pale, kikubwa
kinachosubirwa ni majibu ya serikali juu ya maombi ya eneo la ziada,
kwani Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam alisema suala hilo lipo ukingoni na
mda si mrefu.