Sunday, May 11, 2014

NIGERIA YAITANDIKA 2-0 NGORONGORO HEROES TAIFA

Timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20,Ngorongoro Heroes jioni hii imeambulia kipigo cha mabao 2-0 dhidi ya Nigeria uwanja wa taifa jijini dare s salaam katika Mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kwa vijana wa 20 ambapo kwa matokeo hayo yamempa kazi ngumu kocha mkuu John Simkoko kusonga mbele.
Ngorongora walipata nafasi kadhaa za kufunga kipindi cha kwanza, lakini bado ugonjwa wa kutotumia nafasi muhimu unazidi kuitafuna timu hii

Mshambuliaji Saady Kipanga alishindwa kuonesha makeke yake baada ya kupoteza nafasi kadhaa za kufunga.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika milango ya timu zote ilikuwa migumu, huku kipa namba moja wa Heroes, Aishi Manula akiumia.
Kipindi cha pili, Manula alishindwa kurejea uwanjani na kumpisha kipa namba mbili, Peter Manyika.
Katika Kipindi hicho cha pili Ngorongoro waliingia kizembe na kujikuta wakifungwa mabao mawili na kumaliza mechi kwa kipigo cha nyumbani cha mabao mawili kwa sifuri.