Friday, December 26, 2014

SIMBA YAANGUKIA PUA TAIFA YAPIGWA KIMOJA NA KAGERA SUGAR

RATIBA NA MATOKEO LIGI KUU
Ijumaa Desemba 26
Simba 0 v Kagera Sugar 1
Mfungaji Atupele Greeni
LIGI KUU VODACOM:
RATIBA
Jumamosi Desemba 27
Mtibwa Sugar v Stand United               
Prisons v Coastal Union             
JKT Ruvu v Ruvu Shootings
Jumapili Desemba 28
Mbeya City v Ndanda FC            
Polisi Moro v Mgambo JKT          
Yanga v Azam FC             
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Mtibwa Sugar
7
4
3
0
10
3
7
15
2
Yanga
7
4
1
2
9
4
5
13
3
Azam FC
7
4
1
2
8
4
4
13
4
Kagera Sugar
8
2
4
1
6
3
3
13
5
Coastal Union
7
3
2
2
8
6
2
11
6
JKT Ruvu
7
3
1
3
7
7
0
10
7
Simba
8
1
6
0
7
6
1
9
8
Polisi Moro
7
3
2
2
6
7
-1
9
9
Mgambo JKT
7
3
0
4
4
7
-3
9
10
Stand United
7
2
3
2
5
9
-4
9
11
Ruvu Shooting
7
2
1
4
4
7
-3
7
12
Tanzania Prisons
7
1
3
3
5
6
-1
6
13
Ndanda FC
7
2
0
5
8
12
-4
6
14
Mbeya City
7
1
2
4
3
5
-2
5
MATOKEO- Mechi zilizopita:
Jumapili Novemba 9
Simba 1 Ruvu Shootings 0          
JKT Ruvu 2 Ndanda FC 0
Jumamosi Novemba 8
Stand United 1 Mbeya City 0       
Yanga 2 Mgambo JKT 0             
Mtibwa Sugar 1 Kagera Sugar 1            
Azam FC 2 Coastal Union 1                 
Polisi Moro 1 Prisons 0
Jumapili Novemba 2
Mgambo JKT 2 Mbeya City 1
Jumamosi Novemba 1
Kagera Sugar 0 Yanga 1
Coastal Union 1 Ruvu Shooting 0
LIGI-KUU-VODACOM-MPYANdanda FC 1 Azam FC 0
Mtibwa Sugar 1 Simba 1
JKT Ruvu 1 Polisi Moro 2
Stand United 1 Prisons 1
Jumapili Oktoba 26
Mbeya City 0 Mtibwa Sugar 2
Jumamosi Oktoba 25
Stand United 0 Yanga 3
Azam FC 0 JKT Ruvu 1
Prisons 1 Simba 1
Kagera Sugar 1 Coastal Union 1
Ruvu Shooting 1 Polisi Moro 0
Ndanda FC 0 Mgambo JKT
Jumapili Oktoba 19
Prisons 1 JKT Ruvu 2
Jumamosi Oktoba 18
Polisi Moro 0 Mtibwa Sugar 0
Ndanda FC 1 Ruvu Shooting 3
Kagera Sugar 0 Stand United 0
Coastal Union 2 Mgambo JKT 0
Mbeya City 0 Azam FC 1
Yanga 0 Simba 0
Jumapili Oktoba 5
Yanga 2 JKT Ruvu 1
Mtibwa Sugar 1 Mgambo JKT 0
Jumamosi Oktoba 4
Polisi Moro 1 Kagera Sugar 1
Coastal Union 2 Ndanda FC 1
Simba 1 Stand United 1
Prisons 0 Azam FC 0
Ruvu Shootings 0 Mbeya City 0
Septemba 28
JKT Ruvu 0 Kagera Sugar 2
Yanga 2 Prisons 1
Septemba 27
Simba 1 Polisi Moro 1
Azam FC 2 Ruvu Shooting 0        
Mbeya City 1 Coastal Union 0
Mgambo JKT 0 Stand United 1
Mtibwa Sugar 3 Ndanda FC 1
Septemba 21
Simba 2 Coastal Union 2
Septemba 20
Azam FC 3 Polisi Moro 1
Mtibwa Sugar 2 Yanga 0
Stand United 1 Ndanda FC 4
Mgambo JKT 1 Kagera Sugar 0
Ruvu Shooting 0 Tanzania Prisons 2
Mbeya City 0 JKT Ruvu 0

TAIFA CUP WANAWAKE KUANZA JANUARI MOSI

Mashindano ya Taifa ya mpira wa miguu kwa wanawake (Taifa Cup Wanawake) yanazinduliwa rasmi Januari Mosi mwakani kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kwa mechi kati ya wenyeji Mwanza na Mara.
Mechi hiyo itakayoonyeshwa moja kwa moja na televisheni ya Azam itachezwa kuanzia saa 10 jioni. Mashindano hayo yanayodhaminiwa na kampuni ya Proin yatachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini katika hatua ya kwanza.
Januari 10 mwakani ndipo zitachezwa mechi kwa mikoa yote ambapo Geita itakuwa mwenyeji wa Kagera (Uwanja wa Geita), Tabora vs Kigoma (Ali Hassan Mwinyi), Simiyu vs Shinyanga (Uwanja wa Simiyu), Arusha vs Manyara (Sheikh Kaluta Amri Abeid), na Kilimanjaro vs Tanga (Uwanja wa Ushirika).
Mechi nyingine ni Lindi itaikaribisha Mtwara kwenye Uwanja wa Ilulu, Ruvuma vs Njombe (Uwanja wa Majimaji), Mbeya vs Iringa (Uwanja wa Sokoine), Katavi vs Rukwa (Uwanja wa Katavi), Dodoma vs Singida (Uwanja wa Jamhuri) na Pwani itakuwa mwenyeji wa Morogoro katika Uwanja wa Mabatini.
Timu hizo zitarudiana Januari 13 mwakani, ambapo baada ya matokeo ya nyumbani na ugenini timu iliyoshinda ndiyo itakayoingia hatua inayofuata ambayo pia itashirikisha mikoa ya kisoka ya Ilala, Kinondoni na Temeke.
Hatua hiyo, mechi zake za kwanza zitachezwa Januari 17 mwakani wakati zile za marudiano zitafanyika Januari 21 mwakani.
Baada ya hapo, hatua itakayofuata ni robo fainali, nusu fainali na fainali ambayo ndiyo itakayotoa bingwa wa michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya kwanza nchini.
Mdhamini atatoa jezi kwa timu zote zinazoshiriki kabla ya kuanza mashindano hayo.

LIGI KUU MECHI YA JKT RUVU, SHOOTING KUCHEZWA USIKU

Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara kati ya JKT Ruvu na Ruvu Shooting itachezwa kesho (Desemba 27 mwaka huu) usiku kwenye Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam.
Timu hizo zitapambana kuanzia saa 1 kamili usiku katika mechi hiyo itakayoonyeshwa moja kwa moja (live) na Azam Tv.
Viingilio katika mechi hiyo ni sh. 3,000 kwa jukwaa la kawaida na sh. 5,000 kwa upande wa jukwaa la VIP.
Tiketi za kushuhudia mechi hiyo ambazo ni za elektoniki tayari zimeanza kuuzwa kupitia maduka ya Fahari Huduma, M-PESA kwa kupiga *150*03*02# ambayo utapata namba ya kumbukumbu kwa ajili ya kufanya malipo kupitia hiyo hiyo M-PESA na baadaye kuchapa tiketi yako katika mashine maalumu zilizopo kwenye ATM za CRDB.
Pia mshabiki anaweza kununua tiketi kupitia CRDB Simbanking.
Mwamuzi Dominic Nyamisana kutoka Dodoma ndiye atakayechezesha mechi hiyo akisaidiwa na Abdallah Uhako (Arusha), Godwill Kihwili (Arusha) na Hashim Abdallah (Dar es Salaam).

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Saturday, December 20, 2014

MKUTANO MKUU WA TFF KUFANYIKA SINGIDA MACHI 14

Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana jana (Desemba 19 mwaka huu) jijini Dar es Salaam, imezingatia upungufu uliopo katika utekelezaji wa matumizi ya tiketi za elektroniki.

Hivyo, Kamati hiyo imeiagiza Sekretarieti ya TFF kuwasiliana na benki ya CRDB inayoendesha mfumo huo wa matumizi ya tiketi za elektroniki kuhusu upungufu huo na kuhakikisha unafanyiwa kazi.

MAREKEBISHO YA KATIBA YA TFF
Kamati ya Utendaji ya TFF imerejea mazungumzo kati yake na ujumbe wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) uliokuwa nchini ukiongozwa na Meneja wa Vyama Wanachama wa FIFA, James Johnson.  

Mazungumzo hayo kuhusu Katiba ya TFF yalifanyika Desemba 18 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Kamati ya Utendaji inasubiri rasimu ya Katiba hiyo kutoka FIFA ili iweze kufanya utaratibu wa kuwaarifu wanachama wake juu ya maudhui ya rasimu hiyo.

Shughuli ya FIFA kurekebisha katiba za nchi wanachama wake inaendelea duniani kote, na kwa Afrika kazi hiyo imekamilika katika nchi za Namibia, Zimbabwe na Malawi.

USHIRIKIANO KATI YA TFF NA SAFA
Kamati ya Utendaji imepitia na kupitisha makubaliano ya ushirikiano kati ya TFF na Chama cha Mpira wa Miguu Afrika Kusini (SAFA).

Makubaliano hayo ni ushirikiano katika nyanja za mpira wa miguu wa vijana, maendeleo ya waamuzi, ufundi, menejimenti ya matukio (event management) na utafutaji udhamini (sponsorship).

KANUNI ZA LESENI ZA KLABU (CLUB LICENSING REGULATIONS)
Kamati ya Utendaji imejadili rasimu ya Kanuni za Leseni za Klabu (Club Licensing Regulations), na kuagiza Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ifanye marekebisho ya mwisho, kabla ya kanuni hizo kusainiwa na kuanza kutumika.

UANZISHAJI MFUKO WA MAENDELEO YA MPIRA WA MIGUU (FDF)
Kamati ya Utendaji imepokea taarifa ya maendeleo ya mchakato wa uanzishwaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (Football Development Fund- FDF).

Imeipongeza Kamati ya Mfuko huo inayoongozwa na Rais wa zamani wa TFF, Leodegar Tenga, na kuitaka fanye jitihada za kukamilisha rasimu ya kanuni za uendeshaji mfuko huo.

Mbali ya Tenga, wajumbe wengine wa mfuko huo ni Ayoub Chamshama, Ephraim Mafuru, Frederick Mwakalebela, Tarimba Abbas na Zarina Madabida. Sekretarieti ya mfuko huo inaundwa na Henry Tandau ambaye ni Katibu, Wakili Emmanuel Muga na Boniface Wambura.

FDF ambao ni mfuko utakaokuwa unajitegemea utakuwa unashughulika na maendeleo ya mpira wa miguu kwa vijana, na nyanja nyingine za maendeleo kwa mchezo huo.

MKUTANO MKUU KUFANYIKA SINGIDA MACHI 14
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imepanga Mkutano Mkuu wa Kawaida wa mwaka ufanyike Machi 14 na 15 mwakani mjini Singida.

MGOGORO NDANI YA ZFA
Kamati ya Utendaji imepokea kwa masikitiko taarifa za masuala ya mpira wa miguu Zanzibar kupelekwa mahakamani.

Kwa mujibu wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kitendo hicho ni kinyume cha taratibu za uendeshaji mpira wa miguu ambazo zinakataza masuala ya mchezo huo kupelekwa katika mahakama za kawaida.
Kamati ya Utendaji inatoa rai kwa pande zote mbili zinazohusika na mgogoro huo kukaa kwenye meza ya mazungumzo ili kumaliza tofauti zao.

Kamati ya Utendaji imejitolea kutuma ujumbe wake Zanzibar ili ukutane na pande zinazohusika katika mgogoro huo.

Ni muhimu usuluhisho upatikane haraka ili tuweze kujua hatma ya washiriki wetu kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Tuesday, December 16, 2014

MICHUANO YA COPA COCA-COLA YAENDELEA KUTIMUA VUMBI.

Michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 ngazi ya Taifa inaendelea leo jioni (Desemba 16 mwaka huu) kwa mechi mbili zitakazochezwa jijini Dar es Salaam na mkoani Pwani.


Uwanja wa Nyumbu uliopo mkoani Pwani utazikutanisha timu za Mjini Magharibi na Dodoma katika mechi ya kundi B, wakati kundi C kutakuwa na mechi kati ya Arusha na Mwanza itakayochezwa Uwanja wa Tanganyika Packers uliopo Kawe jijini Dar es Salaam.

Wakati kesho (Desemba 17 mwaka huu) ikiwa ni mapumziko, michuano hiyo itaingia hatua ya robo fainali keshokutwa (Desemba 18 mwaka huu) kwenye viwanja hivyo hivyo.