Monday, April 15, 2013

TAARIFA ZA MAPATO KUTOKA TFF LEO.

MECHI YA AZAM, SIMBA YAINGIZA MIL 66/-
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Azam na Simba iliyochezwa jana (Aprili 14 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 66,855,000 kutokana na watazamaji 11,458. Viingilio katika mechi hiyo namba 155 iliyomalizika kwa timu hizo kutoka sare ya mabao 2-2 vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 15,587,177.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 10,198,220.34. Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,925,683.45, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 4,755,410.07, Kamati ya Ligi sh. 4,755,410.07, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,377,705.03 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,849,326.14.



WATAZAMAJI 11,021 WAZISHUHUDIA YANGA, OLJORO
Watazamaji 11,021 walikata tiketi kushuhudia mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Oljoro JKT iliyochezwa juzi (Aprili 13 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kuingiza sh. 63,170,000. Viingilio katika mechi hiyo namba 156 iliyomalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 14,853,252.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 9,636,101.69. Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,552,501.25, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 4,531,500.75, Kamati ya Ligi sh. 4,531,500.75, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,265,750.37 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,762,250.29.
MASHABIKI WAWILI NCHINI BRAZIL WAUWAWA
VYOMBO vya habari katika nchi ya Brazil vimerioti kuwa mashabiki wawili wa soka nchini humo wamepigwa risasi na kufa wakati wakielekea katika Uwanja wa Castelao Arena uliopo katika mji wa Fortaleza. Kwa mujibu wa taarifa hizo mashabiki hao walikuwa wakielekea kuishangilia timu ya Ceara ambayo ilikuwa ikicheza na wenyeji Fortaleza kabla ya vijana hao kuanzisha vurugu kwa kuwarushia mawe wapinzani wao ambao nao walijibu mapigo na kupelekea vifi vyao. Taarifa hizo ziliendelea kudai kuwa tukio hilo lilitokea maeneo ya karibu na uwanja huo ambao ni mojawapo ya viwanja vitakavyotumika kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia 2014. Katika mchezo huo ambao ulizua tafrani hiyo Ceara walifanikiwa kuwafunga mahasimu wao Fertaleza kwa bao 1-0.v

Saturday, April 13, 2013

YANGA YAINYUKA OLJORO 3- MTUNGI HATIMAYE YAIVUA UBINGWA SIMBA""
KATIKA  dimba la Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga wameitandika JKT Oljoro kwa Bao 3-0 na kuzidi kukwea kileleni mwa VPL, Ligi Kuu Vodacom, wakiwa Pointi 6 mbele ya Timu ya Pili Azam FC.

Ushindi wa leo pia umeivua rasmi Simba Ubingwa kwa vile wana Pointi 35 na wamebakiza Mechi 5 na hata wakishinda zote watafikisha Pointi 50 ambazo Yanga wameshazipita.
WAFUNGAJI
MAGOLI:
-Dakika ya 5 Nadir Haroub ‘Cannavaro’
-Dakika ya 19 Simon Msuva
-Dakika ya 43 Hamis Kiiza
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
VPL itaendelea kesho Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kwa bigi mechi kati ya Simba na Azam FC na kipigo kwa Azam FC kitaipa nafasi Yanga kutwaa Ubingwa.
MATOKEO VPL LEO


Yanga 3-0 Jkt oljoro
T/prison 2-0 Ruvu shooting


MSIMAMO:
NA
TIMU
p
W
D
L
GD
PTS
1
YANGA
21
15
4
2
28
52
2
Azam FC
23
14
4
4
22
47
3
Kagera Sugar
22
10
7
5
7
37
4
Simba
22
9
8
4
12
36
5
Mtibwa Sugar
23
8
9
6
2
33
6
Coastal Union
22
8
8
6
3
32
7
Ruvu Shooting
21
8
6
7
2
30
8
JKT Oljoro
22
7
7
8
-1
28
9
T/prison
21
4
10
9
-11
26
10
Jkt mgambo
21
7
3
9
-6
24
11
Toto African
24
4
10
1O
-11
22
12
JKT Ruvu
22
6
4
12
-16
22
13
African lyon
23
5
4
14
-19
21
14
Polisi  moro
23
3
10
10
-10
19
MATATIZO YA KIUFUNDI YAKWAMISHA SUPER WEEK ‘LIVE’
Mechi tano kati ya sita za Super Week za Ligi Kuu ya Vodacom zilizokuwa zioneshwe moja kwa moja (live) na Kituo cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini sasa hazitaoneshwa kutokana na matatizo ya kiufundi.
TFF_LOGO12Kwa mujibu wa Mtayarishaji Mtendaji (Executive Producer) wa SuperSport Kanda ya Afrika, Max Tshunungwa ambaye yuko nchini, wameshindwa kuonesha mechi hizo kutokana na matatizo ya kiufundi katika magari yao ya kurushia matangazo (OB van) yanayohudumia Afrika Mashariki- Kenya, Tanzania na Uganda.
Mechi hizo ni kati ya Azam na African Lyon, Yanga na Oljoro JKT, Azam na Simba, Coastal Union na JKT Ruvu na Mgambo Shooting na Yanga itakayochezwa Aprili 17 mwaka huu jijini Tanga.
Tatizo hilo pia limeathiri mechi za Ligi Kuu ya Kenya (KPL) ambazo hazitaonekana wikiendi hii. SuperSport ndiyo yenye haki za matangazo ya televisheni kwa ligi hiyo ya Kenya.
Tshunungwa amekutana na Sekretarieti ya TFF na Kamati ya Ligi kuelezea tatizo hilo. SuperSport kwa kushirikiana na Kamati ya Ligi na TFF watapanga mechi nyingine za Super Week kabla ya ligi kumalizika msimu huu.
Pia TFF, Kamati ya Ligi na SuperSport watakuwa na mkutano mfupi wa waandishi wa habari wakati wa mapumziko kwenye mechi ya leo kati ya Yanga na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Friday, April 12, 2013

UJUMBE WA FIFA KUWASILI APRILI 15
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linapenda kuwatangazia wadau wa mpira wa miguu kuwa ujumbe wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) utawasili nchini Jumatatu (Aprili 15 mwaka huu) kwa ajili ya kushughulikia mchakato wa uchaguzi mkuu wa TFF.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka FIFA, ujumbe huo utaongozwa na Mkuu wa Idara ya Uanachama ya FIFA, Primo Covarro na utafanya kazi kwa siku tatu kuanzia siku ya ujio na kuondoka Aprili 18 mwaka huu.

Ukiwa nchini, ujumbe huo utakutana na wagombea uongozi walioathiriwa na uamuzi wa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF ambao waliomba mashauri yao yaangaliwe upya, wagombea ambao walikata rufani FIFA, Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Kamati ya Rufani na Sekretarieti ya TFF.

Wajumbe hao wangependa kukutana na waziri anayehusika na michezo, hivyo TFF imeiandikia Wizara ikipendekeza kuwa ujumbe huo ukutane na Waziri na wakuu wengine wa michezo Aprili 16 mwaka huu 2013 kabla ya kuanza kazi zao.

Wagombea watakaosikilizwa na ujumbe huo wa FIFA ni:
1.   Farid Salim Mbaraka Nahdi: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alienguliwa na Kamati ya Uchaguzi na baadaye rufani yake kwa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF kutupwa na hali kadhalika ombi lake la kutaka shauri lake liangaliwe upya, kukataliwa.

2.   Elliud Peter Mvella: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF na kukata rufani Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF kabla ya maombi yake ya kutaka shauri lake kuangaliwa upya, kukataliwa.


3.   Mbasha Matutu: Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi na kukata rufani ambayo pia ilitupwa kabla ya kuomba shauri lake liangaliwe upya, ombi ambalo lilikataliwa.

4.   Hamad Yahya: Mgombea wa nafasi ya uenyekiti wa Bodi ya Ligi ambaye alipitishwa na Kamati ya Uchaguzi, lakini mwekaji pingamizi akakata rufani ambayo ilikubaliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF na kuondolewa. Aliomba shauri lake liangaliwe upya, lakini Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF ikatupa ombi lake.

5.   Jamal Emily Malinzi: Mgombea wa nafasi ya urais wa TFF ambaye alipitishwa na Kamati ya Uchaguzi, lakini mwekaji pingamizi akakata rufani ambayo ilikubaliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF, hivyo kuondolewa kwenye mchakato. Aliomba shauri lake liangaliwe upya, lakini likakataliwa. Hata hivyo, alikuwa ameshakata rufani FIFA.

6.   Michael Wambura: Mgombea wa nafasi ya Makamu wa Rais wa TFF ambaye alikatwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF na rufani yake kukataliwa na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF. Hakuomba shauri lake liangaliwe upya, lakini alikata rufani FIFA.

Shirikisho linawaomba wote waliotajwa hapo juu kujiandaa kwa utetezi na maelezo ya kutosha na kwamba barua za kuwaita zinafuata. (Orodha ya waathiriwa na programu ya ujumbe wa FIFA imeambatanishwa)

YANGA, OLJORO KUUMANA MECHI ZA VPL
Ligi Kuu ya Vodacom inaendelea kesho (Aprili 13 mwaka huu) kwa mechi mbili zitakazochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, na Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Yanga itakuwa mwenyeji wa Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa wakati Uwanja wa Sokoine utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Tanzania Prisons na Ruvu Shooting.

Ligi hiyo itaendelea keshokutwa (Aprili 14 mwaka huu) kwa mechi kati ya wenyeji Azam na Simba. Mechi hiyo namba 155 itachezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

WASHELISHELI KUICHEZESHA AZAM CAF
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Shelisheli kuchezesha mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho kati ya Azam na AS FAR ya Morocco itakayofanyika Aprili 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Waamuzi hao ni Emile Fred atakayepuliza filimbi akisaidiwa na Steve Maire na Jean Ernesta. Mwamuzi wa mezani (fourth official) atakuwa Jean Claude Labrossa. Kamishna wa mechi hiyo ni Abbas Sendyowa kutoka Uganda.

Wakati huo huo, CAF imemteua Mtanzania Alfred Lwiza kuwa Kamishna wa mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho kati ya Liga Muculmana ya Msumbiji na Wydad Casablanca ya Morocco.

Mechi hiyo itakayochezwa kati ya Aprili 19,20 au 21 mwaka huu nchini Msumbiji itachezeshwa na waamuzi kutoka Zimbabwe wakiongozwa na Ruzive Ruzive.


Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Wednesday, April 10, 2013

KOCHA RHINO APIGWA FAINI, AFUNGIWA MECHI SITA
KAMATI ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imempiga faini ya sh. 400,000 na kumfungia mechi sita Kocha wa Rhino Rangers, Renatus Shija kwa kushiriki vitendo vinavyoashiria imani za ushirikina na kumdhihaki mwamuzi kwenye mechi za Ligi Daraja la Kwanza (FDL).

Adhabu hizo zimetolewa kwa mujibu wa kifungu cha 31(1)(a) na (b) cha Kanuni za FDL ambapo Kocha huyo aliyeipandisha daraja Rhino Rangers kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) alifanya vitendo hivyo kwenye mechi mbili tofauti.

Mechi hizo ni kati ya Kanembwa JKT na Rhino Rangers iliyochezwa Februari 23 mwaka huu Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma, na ile kati ya Rhino Rangers na Morani iliyochezwa Machi 17 mwaka huu Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.

Pia klabu ya Rhino Rangers imepigwa faini ya sh. 200,000 kutokana na Polisi Wanajeshi- MP kuwapiga walinzi milangoni kwenye mechi hiyo dhidi ya Kanembwa JKT ili kupisha washabiki wa timu hiyo waingie bure uwanjani.

Mchezaji wa timu ya Pamba ya Mwanza, Leonard Nahole amepigwa faini ya sh. 200,000 na kufungiwa mechi nne baada ya kumrushia chupa ya maji mwamuzi kwa madai amependelea kwenye mechi dhidi ya Polisi Tabora iliyochezwa Machi 16 mwaka huu.

Nao wachezaji Joseph Mapalala, Yohana Mirobo, Noel Makunja, Mkome Pastory na Rudenzi Kilinga wa Polisi Mara wamepigwa faini ya sh. 200,000 kila mmoja na kufungiwa mechi tatu kwa kufanya vitendo vinavyoshiria ushirikina na kumkimbiza mwamuzi kwenye mechi dhidi ya Morani iliyochezwa Machi 9 mwaka huu. Adhabu za wachezaji hao ni kwa mujibu wa kifungu cha 27(1)(g) cha Kanuni za FDL.

Klabu ya Villa Squad imepigwa faini ya sh. 150,000 kwa kuchelewa uwanjani kwenye mechi yake dhidi ya Ashanti United wakati Majimaji imepigwa faini ya sh. 200,000 kutokana na washabiki wake kufanya vurugu kwenye mechi dhidi ya Mbeya City iliyochezwa Uwanja wa Majimaji.

Vilevile Msimamizi wa Uwanja wa Majimaji aliyetambulika kwa jina moja la Mapunda aliwatukana waamuzi kwenye mechi hiyo, na suala lake litafikishwa kwenye Kamati ya Nidhamu ya TFF kwa ajili ya hatua za kinidhamu.

Pia uongozi wa Uwanja wa Mafinga unaotumiwa na timu ya daraja la kwanza ya Kurugenzi umetakiwa kuufanyia marekebisho, vinginevyo hautatumika kwa mechi za FDL msimu ujao.

MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kesho (Aprili 11 mwaka huu) litakuwa na Mkutano na Waandishi wa Habari. Mkutano huo utafanyika saa 5 asubuhi kwenye ofisi za TFF.
Boniface Wambura
Ofisa Habari

UEFA KUANZISHA ADHABU MPYA

SHIRIKISHO la Soka barani Ulaya-UEFA limepanga kuanzisha adhabu mpya kali ya kupambana na ubaguzi wa rangi ambap wachezaji watakaokutwa na hatia ya kufanya vitendo hivyo watafungiwa si chini mechi 10. Katika Mkuu wa UEFA Gianni Infantino amesema pia watafunga viwanja kwa muda viwanja ambavyo mashabiki wake watafanya tukio kama hilo kwa mara ya kwanza na kuufunga kabisa kama mashabiki wa timu husika watarudia tukio hilo kwa mara ya pili pamoja na faini ya fedha nyingi. Adhabu hizo mpya ambazo zilizungumziwa katika kikao cha kamati ya utendaji ya UEFA kilichokutana jana kitahusisha mechi zote za mashindano barani Ulaya. Infantino alifafanua kuwa kama mashabiki wa klabu fulani watakutwa na hatia ya kufanya vitendo hivyo basi upande wa uwanja uliohusika na tukio hilo utafungwa lakini kama tatizo ilikijirudia basi mashabiki wote watazuiwa kuingia uwanjani na kutozwa faini itakayofikia dola 65,300.

MCHEZA gofu namba moja duniani, Tiger Woods amesema yuko katika kiwango kizuri tayari kukata ukame wa miaka mitano kupita bila kushinda taji kubwa la Masters wiki hii. Woods ndio anapewa nafasi kubwa ya kunyakuwa zawadi ya Koti ya Bluu toka alipofanya hivyo mwaka 2005 na taji la kwanza kubwa toka mwaka 2008 baada ya kurejea kileleni mwa orodha ya wachezaji bora wa mchezo huo kwa kushinda mataji matatu mwaka huu. Nyota huyo alianguka mpaka katika nafasi ya 58 mwaka 2011 kufuatia kukumbwa na kashfa katika maisha yake binafsi na pia kusumbuliwa na majeruhi. Akihojiwa Woods mwenye umri wa miaka 37 amesema kwasasa anajisikia kurejesha makali yake ya zamani hivyo anategemea kufanya vizuri zaidi mwaka huu.